< Colossiens 4 >
1 Maîtres, rendez le droit et l'équité à vos serviteurs, sachant que vous avez aussi un Seigneur dans les Cieux.
Ninyi mabwana, watendeeni watumwa wenu yaliyo haki na yanayostahili, mkitambua ya kwamba ninyi pia mnaye Bwana mbinguni.
2 Persévérez dans la prière, veillant dans cet exercice avec des actions de grâces:
Dumuni sana katika maombi, mkikesha katika hayo pamoja na kushukuru.
3 Priez aussi tous ensemble pour nous, afin que Dieu nous ouvre la porte de la parole, pour annoncer le mystère de Christ, pour lequel aussi je suis prisonnier.
Pia tuombeeni na sisi ili Mungu atufungulie mlango wa kunena, ili tupate kuitangaza siri ya Kristo, ambayo kwa ajili yake pia mimi nimefungwa.
4 Afin que je le manifeste selon qu'il faut que j'en parle.
Ombeni ili nipate kuitangaza Injili kwa udhahiri kama ipasavyo kunena.
5 Conduisez-vous sagement envers ceux de dehors, rachetant le temps.
Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati.
6 Que votre parole soit toujours assaisonnée de sel avec grâce, afin que vous sachiez comment vous avez à répondre à chacun.
Maneno yenu yawe yamejaa neema siku zote, yanayofaa, ili mjue jinsi iwapasavyo na inavyofaa kumjibu kila mtu.
7 Tychique, notre frère bien-aimé, et fidèle Ministre, et compagnon de service en [notre]Seigneur, vous fera savoir tout mon état.
Tikiko atawaambia habari zangu zote. Yeye ni ndugu mpendwa, mtendakazi mwaminifu na mtumishi mwenzangu katika Bwana.
8 Je l'ai envoyé vers vous expressément, afin qu'il connaisse quel est votre état, et qu'il console vos cœurs;
Nimemtuma kwenu kwa madhumuni haya ili mpate kufahamu hali yetu, na pia awatie moyo.
9 Avec Onésime notre fidèle et bien-aimé frère, qui est des vôtres, ils vous avertiront de toutes les affaires de deçà.
Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpendwa na mwaminifu, ambaye ni mmoja wenu. Watawaambia mambo yote yanayotendeka hapa kwetu.
10 Aristarque, qui est prisonnier avec moi, vous salue aussi, et Marc qui est le cousin de Barnabas, touchant lequel vous avez reçu un ordre: s'il vient à vous, recevez-le,
Aristarko aliye mfungwa pamoja nami anawasalimu, vivyo hivyo Marko, binamu yake Barnaba. (Mmeshapata maagizo yanayomhusu; akija kwenu, mpokeeni.)
11 Et Jésus, appelé Juste, qui sont de la Circoncision; ceux-ci qui sont mes compagnons d'œuvre au Royaume de Dieu, sont [aussi] les seuls qui m'ont été en consolation.
Yesu, yeye aitwaye Yusto, pia anawasalimu. Hawa peke yao ndio Wayahudi miongoni mwa watendakazi wenzangu kwa ajili ya Ufalme wa Mungu, nao wamekuwa faraja kwangu.
12 Epaphras, qui est des vôtres, Serviteur de Christ, vous salue, combattant toujours pour vous par ses prières, afin que vous demeuriez parfaits et accomplis en toute la volonté de Dieu.
Epafra, ambaye ni mmoja wenu na mtumishi wa Kristo Yesu, anawasalimu. Yeye siku zote anawaombea kwa bidii kwamba msimame imara katika mapenzi yote ya Mungu, mkiwa wakamilifu na thabiti.
13 Car je lui rends témoignage qu'il a un grand zèle pour vous, et pour ceux de Laodicée, et pour ceux d'Hiérapolis.
Ninashuhudia kumhusu kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, na kwa ajili ya ndugu wa Laodikia na wale wa Hierapoli.
14 Luc, le médecin bien-aimé, vous salue; et Démas aussi.
Rafiki yetu mpenzi Luka yule tabibu, pamoja na Dema, wanawasalimu.
15 Saluez les frères qui sont à Laodicée, et Nymphas, avec l'Eglise qui est en sa maison.
Wasalimuni ndugu wote wa Laodikia, na pia Nimfa, pamoja na kanisa linalokutana katika nyumba yake.
16 Et quand cette Lettre aura été lue entre vous, faites qu'elle soit aussi lue dans l'Eglise des Laodiciens; et vous aussi lisez celle qui [est venue] de Laodicée.
Baada ya barua hii kusomwa kwenu, hakikisheni kwamba inasomwa pia katika kanisa la Walaodikia. Nanyi pia msome barua inayotoka Laodikia.
17 Et dites à Archippe: prends garde à l'administration que tu as reçue en [notre] Seigneur, afin que tu l'accomplisses.
Mwambieni Arkipo hivi: “Hakikisha kuwa unakamilisha ile huduma uliyopokea katika Bwana.”
18 La salutation est de la propre main de moi Paul. Souvenez-vous de mes liens. Que la grâce soit avec vous! Amen!
Mimi, Paulo, naandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Kumbukeni minyororo yangu. Neema iwe nanyi. Amen.