< Colossiens 2 >
1 Or je veux que vous sachiez combien est grand le combat que j'ai pour vous, et pour ceux qui [sont] à Laodicée, et pour tous ceux qui n'ont point vu ma présence en la chair;
Kwa kuwa nataka mfahamu jinsi ambavyo nimekuwa na taabu nyingi kwa ajili yenu, kwa wote walioko Laodikia na kwa wote ambao hawajaona uso wangu katika mwili.
2 Afin que leurs cœurs soient consolés, étant unis ensemble dans la charité, et dans toutes les richesses d'une pleine certitude d'intelligence, pour la connaissance du mystère de notre Dieu et Père, et de Christ.
Nafanya kazi ili kwamba mioyo yao iweze kufarijiwa kwa kuletwa pamoja katika upendo na katika utajiri wote wa wingi wa uhakika kamili wa maarifa, katika kuijua siri ya kweli ya Mungu, ambaye ni Kristo.
3 En qui se trouvent tous les trésors de sagesse et de science.
Katika Yeye hazina zote za hekima na maarifa zimefichwa.
4 Or je dis ceci afin que personne ne vous trompe par des discours séduisants.
Nasema hivi ili kwamba mtu yeyote asije akawafanyia hila kwa hotuba yenye ushawishi.
5 Car quoique je sois absent de corps, toutefois je suis avec vous en esprit, me réjouissant, et voyant votre ordre et la fermeté de votre foi, que vous avez en Christ.
Na ingawa sipo pamoja nanyi katika mwili, lakini nipo nanyi katika roho. Ninafurahi kuona utaratibu wenu mzuri na nguvu ya imani yenu katika Kristo.
6 Ainsi donc que vous avez reçu le Seigneur Jésus-Christ, marchez en lui;
Kama mlivyompokea Kristo Bwana, tembeeni katika yeye.
7 Etant enracinés et édifiés en lui, et fortifiés en la foi, selon que vous avez été enseignés, abondant en elle avec action de grâces.
Mwimarishwe katika yeye, mjengwe katika yeye, mwimarishwe katika imani kama tu mlivyofundishwa, na kufungwa katika shukrani nyingi.
8 Prenez garde que personne ne vous gagne par la philosophie, et par de vains raisonnements conformes à la tradition des hommes et aux éléments du monde et non point à la [doctrine] de Christ.
Angalieni ya kwamba mtu yeyote asiwanase kwa falsafa na maneno matupu ya udanganyifu kulingana na mapokeo ya wanadamu, kulingana na kanuni za kidunia, na sio kulingana na Kristo.
9 Car toute la plénitude de la Divinité habite en lui corporellement.
Kwa kuwa katika yeye ukamilifu wote wa Mungu unaishi katika mwili.
10 Et vous êtes rendus accomplis en lui; qui est le Chef de toute principauté et puissance;
Nanyi mmejazwa katika yeye. Yeye ni kichwa cha kila uweza na mamlaka.
11 En qui aussi vous êtes circoncis d'une Circoncision faite sans main, qui consiste à dépouiller le corps des péchés de la chair, ce [qui est] la Circoncision de Christ;
Katika yeye pia mlitahiriwa kwa tohara isiyofanywa na wanadamu katika kuondolewa mwili wa nyama, lakini ni katika tohara ya Kristo.
12 Etant ensevelis avec lui par le Baptême; en qui aussi vous êtes ensemble ressuscités par la foi de l'efficace de Dieu, qui l'a ressuscité des morts.
Mlizikwa pamoja naye katika ubatizo. Na kwa njia ya imani katika yeye mlifufuliwa kwa uweza wa Mungu, aliyemfufua kutoka kwa wafu.
13 Et lorsque vous étiez morts dans vos offenses, et dans le prépuce de votre chair, il vous a vivifiés ensemble avec lui, vous ayant gratuitement pardonné toutes vos offenses.
Na mlipokuwa mmekufa katika makosa yenu na kutokutahiriwa kwa miili yenu, aliwafanya hai pamoja naye na kutusamehe makosa yetu yote.
14 En ayant effacé l'obligation [qui était] contre nous, laquelle consistait en des ordonnances, et nous était contraire, et laquelle il a entièrement abolie, l'ayant attachée à la croix.
Alifuta kumbukumbu ya madeni iliyoandikwa, na taratibu zilizokuwa kinyume nasi. Aliiondoa yote na kuigongomea msalabani.
15 Ayant dépouillé les principautés et les puissances, qu'il a produites en public triomphant d'elles en la croix.
Aliziondoa nguvu na mamlaka. Aliyaweka wazi na kuyafanya kuwa sherehe ya ushidi kwa njia ya msalaba wake.
16 Que personne donc ne vous condamne pour le manger ou pour le boire, ou pour la distinction d'un jour de Fête, ou [pour un jour] de nouvelle lune, ou pour les sabbats.
Kwa hiyo, mtu yeyote asiwahukumu ninyi katika kula au katika kunywa, au kuhusu siku ya sikukuu au mwezi mpya, au siku za Sabato.
17 Lesquelles choses sont l'ombre de celles qui étaient à venir, mais le corps en est en Christ.
Hivi ni vivuli vya mambo yajayo, lakini kiini ni Kristo.
18 Que personne ne vous maîtrise à son plaisir par humilité d'esprit, et par le service des Anges, s'ingérant dans des choses qu'il n'a point vues, étant témérairement enflé du sens de sa chair.
Mtu awaye yote asinyang'anywe tuzo yake kwa kutamani unyenyekevu na kwa kuabudu malaika. Mtu wa jinsi hiyo huingia katika mambo aliyoyaona na kushawishiwa na mawazo yake ya kimwili.
19 Et ne retenant point le Chef, duquel tout le Corps étant fourni et ajusté ensemble par les jointures et les liaisons, croît d'un accroissement de Dieu.
Yeye hakishikilii kichwa. Ni kutoka katika kichwa kwamba mwili wote kupitia viungo vyake na mifupa huungwa na kushikamanishwa kwa pamoja; na hukua kwa ukuaji utolewao na Mungu.
20 Si donc vous êtes morts avec Christ, quant aux rudiments du monde, pourquoi vous charge-t-on d'ordonnances, comme si vous viviez au monde?
Ikiwa mlikufa pamoja na Kristo kwa tabia za dunia, mbona mnaishi kama mnawajibika kwa dunia:
21 [Savoir], Ne mange, Ne goûte, Ne touche point.
“Msishike, wala kuonja, wala kugusa”?
22 Qui sont toutes choses périssables par l'usage, [et établies] suivant les commandements et les doctrines des hommes.
Haya yote yameamuriwa kwa ajili ya uharibifu ujao na matumizi, kutokana na maelekezo na mafundisho ya wanadamu.
23 [Et] qui ont pourtant quelque apparence de sagesse en dévotion volontaire, et en humilité d'esprit, et en ce qu'elles n'épargnent nullement le corps, et n'ont aucun égard au rassasiement de la chair.
Sheria hizi zina hekima ya dini zilizotengenezwa kwa ubinafsi na unyenyekevu na mateso ya mwili. Lakini hazina thamani dhidi ya tamaa za mwili.