< Amos 5 >

1 Ecoutez cette parole, qui est la complainte que je prononce à haute voix touchant vous, maison d'Israël!
Sikia neno hili, ee nyumba ya Israeli, ombolezo hili ninalifanya kuwahusu ninyi:
2 Elle est tombée, elle ne se relèvera plus, la vierge d'Israël; elle est abandonnée sur la terre, il n'y a personne qui la relève.
“Bikira Israeli ameanguka, kamwe hatainuka tena, ameachwa pweke katika nchi yake, hakuna yeyote wa kumwinua.”
3 Car ainsi a dit le Seigneur l'Eternel, à la maison d'Israël: La ville de laquelle il en sortait mille, n'en aura de reste que cent; et celle de laquelle il en sortait cent, n'en aura de reste que dix.
Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “Wakati mmoja wa miji yako utakapopeleka watu elfu moja vitani kwa ajili ya Israeli, mia moja tu watarudi; wakati mji utakapopeleka mia moja, kumi tu ndio watarudi hai.”
4 Car ainsi a dit l'Eternel à la maison d'Israël: Cherchez-moi, et vous vivrez.
Hili ndilo Bwana asemalo kwa nyumba ya Israeli: “Nitafuteni mpate kuishi;
5 Et ne cherchez point Béthel, et n'entrez point dans Guilgal, et ne passez point à Béer-Sébah; car Guilgal sera entièrement transportée en captivité, et Béthel sera détruite.
msitafute Betheli, msiende Gilgali, msisafiri kwenda Beer-Sheba. Kwa maana kwa hakika Gilgali itakwenda uhamishoni, na Betheli itafanywa kuwa si kitu.”
6 Cherchez l'Eternel, et vous vivrez, de peur qu'il ne saisisse la maison de Joseph, comme un feu qui la consumera, sans qu'il y ait personne qui l'éteigne à Béthel.
Mtafuteni Bwana mpate kuishi, au atafagia nyumba ya Yosefu kama moto; utawateketeza, nayo Betheli haitakuwa na yeyote wa kuuzima.
7 Parce qu'ils changent le jugement en absinthe, et qu'ils renversent la justice.
Ninyi ambao mnageuza haki kuwa uchungu na kuiangusha haki chini
8 [Cherchez] celui qui a fait la Poussinière et l'Orion, qui change les plus noires ténèbres en aube du jour, et qui fait devenir le jour obscur comme la nuit; qui appelle les eaux de la mer, et les répand sur le dessus de la terre, le nom duquel est l'Eternel.
(yeye ambaye alifanya Kilimia na Orioni, ambaye hugeuza giza kuwa mapambazuko na mchana kuwa usiku, ambaye huyaita maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake;
9 Qui renforce le fourrageur par-dessus l'homme fort, tellement que le fourrageur entrera dans la forteresse.
yeye hufanya maangamizo kwenye ngome na kufanya mji uliozungushiwa ngome kuwa ukiwa),
10 Ils haïssent à la porte ceux qui les reprennent, et ils ont en abomination celui qui parle en intégrité.
mnamchukia yule akemeaye mahakamani, na kumdharau yule ambaye husema kweli.
11 C'est pourquoi à cause que vous opprimez le pauvre, et lui enlevez la charge de froment, vous avez bâti des maisons de pierre de taille; mais vous n'y habiterez point; vous avez planté des vignes bonnes à souhait; mais vous n'en boirez point le vin.
Mnamgandamiza maskini na kumlazimisha awape nafaka. Kwa hiyo, ingawa mmejenga majumba ya mawe ya fahari, hamtaishi ndani yake; ingawa mmepanda mashamba mazuri ya mizabibu, hamtakunywa divai yake.
12 Car j'ai connu vos crimes, ils sont en grand nombre, et vos péchés se sont multipliés: vous êtes des oppresseurs du juste, et des preneurs de rançon, et vous pervertissez à la porte le droit des pauvres.
Kwa kuwa ninajua hesabu ya makosa yenu na ukubwa wa dhambi zenu. Mmewaonea wenye haki na kupokea rushwa na kuzuia haki ya maskini mahakamani.
13 C'est pourquoi l'homme prudent se tiendra dans le silence en ce temps-là; car le temps est mauvais.
Kwa hiyo mtu mwenye busara hunyamaza kimya nyakati kama hizo, kwa kuwa nyakati ni mbaya.
14 Cherchez le bien, et non pas le mal, afin que vous viviez; et ainsi l'Eternel, le Dieu des armées, sera avec vous, comme vous l'avez dit.
Tafuteni mema, wala si mabaya, ili mpate kuishi. Ndipo Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote atakuwa pamoja nanyi, kama msemavyo yupo nanyi.
15 Haïssez le mal, et aimez le bien, et établissez le jugement à la porte; l'Eternel le Dieu des armées, aura peut-être pitié du reste de Joseph.
Yachukieni maovu, yapendeni mema; dumisheni haki mahakamani. Yamkini Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote atawahurumia mabaki ya Yosefu.
16 C'est pourquoi l'Eternel le Dieu des armées, le Seigneur dit ainsi; Il y aura lamentation par toutes les places, et on criera par toutes les rues Hélas! Hélas! Et on appellera au deuil le laboureur, et à la lamentation ceux qui en savent le métier.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, asemalo: “Kutakuwepo maombolezo katika barabara zote na vilio vya uchungu katika njia kuu zote. Wakulima wataitwa kuja kulia, na waombolezaji waje kuomboleza.
17 Et il y aura lamentation par toutes les vignes; car je passerai tout au travers de toi, a dit l'Eternel.
Kutakuwepo kuomboleza katika mashamba yote ya mizabibu, kwa kuwa nitapita katikati yenu,” asema Bwana.
18 Malheur à vous qui désirez le jour de l'Eternel; De quoi vous [servira] le jour de l'Eternel? Ce sont des ténèbres, et non pas une lumière.
Ole wenu ninyi mnaoitamani siku ya Bwana! Kwa nini mnaitamani siku ya Bwana? Siku hiyo itakuwa giza, si nuru.
19 C'est comme si un homme s'enfuyait de devant un lion, et qu'un ours le rencontrât, ou qu'il entrât en la maison, et appuyât sa main sur la paroi, et qu'un serpent le mordît.
Itakuwa kama vile mtu aliyemkimbia simba kumbe akakutana na dubu, kama vile mtu aliyeingia nyumbani mwake na kuupumzisha mkono wake kwenye ukuta, kumbe akaumwa na nyoka.
20 Le jour de l'Eternel ne sont-ce pas des ténèbres, et non une lumière? Et l'obscurité n'est-elle point en lui, et non la clarté?
Je, siku ya Bwana haitakuwa giza, na si nuru: giza nene, bila mwonzi wa mwanga?
21 Je hais et rejette vos fêtes solennelles, et je ne flairerai point [l'odeur de vos parfums] dans vos assemblées solennelles.
“Ninachukia, ninazidharau sikukuu zenu za dini; siwezi kuvumilia makusanyiko yenu.
22 Que si vous m'offrez des holocaustes et des gâteaux, je ne les accepterai point; et je ne regarderai point les oblations de prospérités que vous ferez de vos bêtes grasses.
Hata ingawa mnaniletea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka za nafaka, sitazikubali. Ingawa mnaniletea sadaka nzuri za amani, sitazitambua.
23 Ote de devant moi le bruit de tes chansons, car je n'écouterai point la mélodie de tes musettes.
Niondoleeni kelele za nyimbo zenu! Sitasikiliza sauti za vinubi vyenu.
24 Mais le jugement roulera comme de l'eau, et la justice comme un torrent impétueux.
Lakini acheni haki itiririke kama mto, na uadilifu uwe kama kijito kisichokauka!
25 Est-ce à moi, maison d'Israël, que vous avez offert des sacrifices et des gâteaux dans le désert pendant quarante ans?
“Je, mliniletea dhabihu na sadaka kwa miaka arobaini kule jangwani, ee nyumba ya Israeli?
26 Au contraire vous avez porté le tabernacle de votre Moloc, [et] Kijun vos images, et l'étoile de vos dieux, que vous vous êtes faits.
Mmeyainua madhabahu ya mfalme wenu, Sikuthi mungu wenu mtawala, na Kiuni mungu wenu wa nyota, ambao mliwatengeneza wenyewe.
27 C'est pourquoi je vous transporterai au-delà de Damas, a dit l'Eternel, duquel le nom est le Dieu des armées.
Kwa sababu hiyo nitawapeleka uhamishoni mbali kupita Dameski,” asema Bwana, ambaye jina lake ni Mungu Mwenye Nguvu Zote.

< Amos 5 >