< 2 Timothée 3 >

1 Or sache ceci, qu'aux derniers jours il surviendra des temps fâcheux.
Lakini yakupasa ufahamu jambo hili, kwamba siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari.
2 Car les hommes seront idolâtres d'eux-mêmes, avares, vains, orgueilleux, blasphémateurs, désobéissants à leurs pères et à leurs mères, ingrats, profanes;
Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kumkufuru Mungu, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio watakatifu,
3 Sans affection naturelle, sans fidélité, calomniateurs, incontinents, cruels, haïssant les gens de bien;
wasio na upendo, wasiopenda kupatanishwa, wasingiziaji, wasiozuia tamaa zao, wakatili, wasiopenda mema,
4 Traîtres, téméraires, enflés [d'orgueil], amateurs des voluptés, plutôt que de Dieu.
wasaliti, wakaidi, waliojaa majivuno, wapendao anasa zaidi kuliko kumpenda Mungu:
5 Ayant l'apparence de la piété, mais en ayant renié la force: éloigne-toi donc de telles gens.
wakiwa na mfano wa utauwa kwa nje, lakini wakizikana nguvu za Mungu. Jiepushe na watu wa namna hiyo.
6 Or d'entre ceux-ci sont ceux qui se glissent dans les maisons, et qui tiennent captives les femmes chargées de péchés, et agitées de diverses convoitises;
Miongoni mwao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu na kuwachukua mateka wanawake wajinga, waliolemewa na dhambi zao na kuyumbishwa na aina zote za tamaa mbaya.
7 Qui apprennent toujours, mais qui ne peuvent jamais parvenir à la pleine connaissance de la vérité.
Wakijifunza siku zote lakini kamwe wasiweze kufikia ujuzi wa kweli.
8 Et comme Jannès et Jambrès ont résisté à Moise, ceux-ci de même résistent à la vérité; [étant des] gens qui ont l'esprit corrompu, et qui sont réprouvés quant à la foi.
Kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Mose, vivyo hivyo watu hawa hupingana na ile kweli. Hawa ni watu wenye akili zilizopotoka, ambao wamekataliwa kwa mambo ya imani.
9 Mais ils n'avanceront pas plus avant: car leur folie sera manifestée à tous, comme le fut celle de ceux-là.
Lakini hawataendelea sana, kwa sababu upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama ulivyokuwa dhahiri upumbavu wa hao watu wawili.
10 Mais pour toi, tu as pleinement compris ma doctrine, ma conduite, mon intention, ma foi, ma douceur, ma charité, ma patience.
Lakini wewe umeyajua mafundisho yangu, mwenendo, makusudi, imani, uvumilivu, upendo, ustahimilivu,
11 Et tu [sais] les persécutions et les afflictions qui me sont arrivées à Antioche, à Iconie, et à Lystre, quelles persécutions, [dis-je], j'ai soutenues, et [comment] le Seigneur m'a délivré de toutes.
mateso na taabu, yaani mambo yote yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Listra, mateso yote niliyostahimili, lakini Bwana aliniokoa katika hayo yote.
12 Or tous ceux aussi qui veulent vivre selon la piété en Jésus-Christ, souffriront persécution.
Naam, yeyote anayetaka kuishi maisha ya utauwa ndani ya Kristo Yesu atateswa.
13 Mais les hommes méchants et séducteurs iront en empirant, séduisant, et étant séduits.
Lakini watu waovu na wadanganyaji watazidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.
14 Mais toi, demeure ferme dans les choses que tu as apprises, et qui t'ont été confiées, sachant de qui tu les as apprises;
Bali wewe, udumu katika yale uliyojifunza na kuyaamini kwa uthabiti, ukitambua ya kuwa ulijifunza hayo kutoka kwa nani,
15 Vu même que dès ton enfance tu as la connaissance des saintes Lettres, qui te peuvent rendre sage à salut, par la foi en Jésus-Christ.
na jinsi ambavyo tangu utoto umeyajua Maandiko matakatifu, ambayo yanaweza kukuhekimisha upate wokovu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.
16 Toute l'Ecriture est divinement inspirée, et utile pour enseigner, pour convaincre, pour corriger, et pour instruire selon la justice;
Kila Andiko limevuviwa na Mungu na lafaa kwa mafundisho, kwa kuwaonya watu makosa yao, kwa kuwaongoza na kwa kuwafundisha katika haki,
17 Afin que l'homme de Dieu soit accompli, et parfaitement instruit pour toute bonne œuvre.
ili mtu wa Mungu awe amekamilishwa, apate kutenda kila kazi njema.

< 2 Timothée 3 >