< 2 Samuel 24 >

1 Or la colère de l'Eternel s'embrasa encore contre Israël; parce que David fut incité contr'eux à dire: Va, dénombre Israël et Juda.
Hasira ya Bwana ikawaka tena dhidi ya Israeli, naye akamchochea Daudi dhidi yao, akisema, “Nenda ukawahesabu Israeli na Yuda.”
2 Le Roi donc dit à Joab, chef de l'armée, lequel il avait avec soi: Passe maintenant par toutes les Tribus d'Israël, depuis Dan jusqu'à Beersébah, et dénombre le peuple, afin que j'en sache le nombre.
Kwa hiyo mfalme akamwambia Yoabu, pamoja na majemadari wa jeshi aliokuwa nao, “Nendeni kwa makabila yote ya Israeli kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na mwandikishe watu wapiganaji, ili niweze kujua idadi yao.”
3 Mais Joab répondit au Roi: Que l'Eternel ton Dieu veuille augmenter ton peuple autant, et cent fois autant qu'il est maintenant; et que les yeux du Roi mon Seigneur le voient! mais pourquoi le Roi mon Seigneur prend-il plaisir à cela?
Lakini Yoabu akamjibu mfalme, “Bwana Mungu wako na azidishe jeshi mara mia, nayo macho ya bwana wangu mfalme na yaone hili. Lakini kwa nini bwana wangu mfalme anataka kufanya kitu cha namna hii?”
4 Néanmoins la parole du Roi l'emporta sur Joab, et sur les Chefs de l'armée; et Joab et les chefs de l'armée sortirent de la présence du Roi pour dénombrer le peuple, [savoir] Israël.
Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu pamoja na majemadari wa jeshi, kwa hiyo wakaondoka mbele ya mfalme kuandikisha wapiganaji wa Israeli.
5 Ils passèrent donc le Jourdain, et se campèrent en Haroher, à main droite de la ville, qui est au milieu du torrent de Gad, et vers Jahzer.
Baada ya kuvuka Yordani, walipiga kambi karibu na Aroeri, kusini ya mji ulioko kwenye bonde jembamba, ndipo wakipitia Gadi, wakaenda hadi Yazeri.
6 Et ils vinrent en Galaad, et dans la terre de ceux qui habitent au bas [pays] d'Hodsi, et vinrent à Dan-Jahan, et ensuite aux environs de Sidon.
Walikwenda hadi Gileadi na pia eneo la Tahtimu-Hodshi, wakaendelea hadi Dani-Yaani na kuzunguka kuelekea Sidoni.
7 Et ils vinrent jusqu'à la forteresse de Tsor, et dans toutes les villes des Héviens, et des Cananéens, et sortirent vers le Midi de Juda à Beersébah.
Kisha wakaenda kuelekea ngome ya Tiro pamoja na miji yote ya Wahivi na ya Wakanaani. Mwishoni, walikwenda mpaka Beer-Sheba katika Negebu ya Yuda.
8 Ainsi ils traversèrent tout le pays, et revinrent à Jérusalem au bout de neuf mois et vingt jours.
Baada ya kupita katika nchi nzima, walirudi Yerusalemu baada ya miezi tisa na siku ishirini.
9 Et Joab donna au Roi le rolle du dénombrement du peuple; et il y eut de ceux d'Israël huit cent mille hommes de guerre tirant l'épée, et de ceux de Juda cinq cent mille hommes.
Yoabu akatoa hesabu ya wapiganaji kwa mfalme: Katika Israeli kulikuwako watu 800,000 wenye uwezo wa kupigana, na katika Yuda watu 500,000.
10 Alors David fut touché en son cœur, après qu'il eut fait ainsi dénombrer le peuple; et David dit à l'Eternel: J'ai commis un grand péché en faisant cela, mais, je te prie, ô Eternel! pardonne l'iniquité de ton serviteur; car j'ai agi très-follement.
Dhamiri ya Daudi ilishtuka baada ya kuwahesabu wapiganaji, naye akamwambia Bwana, “Nimefanya dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Ee Bwana, sasa ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
11 Après cela David se leva dès le matin, et la parole de l'Eternel fut [adressée] à Gad le Prophète, qui était le Voyant de David, en disant:
Kabla Daudi hajaamka kesho yake asubuhi, neno la Bwana lilikuwa limemjia Gadi nabii, aliyekuwa mwonaji wa Daudi, kusema:
12 Va, et dis à David: Ainsi a dit l'Eternel: J'apporte trois choses contre toi; choisis l'une des trois, afin que je te la fasse.
“Nenda ukamwambie Daudi, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
13 Gad vint donc vers David, et lui fit entendre cela en disant: Que veux-tu qui t'arrive: ou sept ans de famine sur ton pays; ou que durant trois mois tu fuies devant tes ennemis, et qu'ils te poursuivent; ou que durant trois jours la mortalité soit en ton pays? Avises-y maintenant, et regarde ce que tu veux que je réponde à celui qui m'a envoyé.
Basi Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Je, ije njaa ya miaka mitatu katika nchi yako? Au miezi mitatu ya kukimbia adui zako wakikufuatia? Au siku tatu za tauni katika nchi yako? Basi sasa, fikiri juu ya hilo na uamue jinsi nitakavyomjibu huyo aliyenituma.”
14 Et David répondit à Gad: Je suis dans une très-grande angoisse. Je te prie que nous tombions entre les mains de l'Eternel, car ses compassions sont en grand nombre; et que je ne tombe point entre les mains des hommes.
Daudi akamjibu Gadi, “Nitataabika sana. Afadhali tuangukie mikononi mwa Bwana, kwa maana rehema zake ni kuu, lakini usiniache nianguke mikononi mwa wanadamu.”
15 L'Eternel donc envoya la mortalité en Israël, depuis le matin jusqu'au temps de l'assignation; et il mourut du peuple depuis Dan jusqu'à Beersébah, soixante-dix mille hommes.
Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli kuanzia asubuhi mpaka mwisho wa muda ulioamriwa, wakafa watu 70,000 kuanzia Dani hadi Beer-Sheba.
16 Mais quand l'Ange eut étendu sa main sur Jérusalem pour la ravager, l'Eternel se repentit de ce mal-là et dit à l'Ange qui faisait le dégât parmi le peuple: C'est assez, retire à cette heure ta main. Or l'Ange de l'Eternel était auprès de l'aire d'Arauna Jébusien.
Malaika aliponyoosha mkono wake ili kuangamiza Yerusalemu, Bwana akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anawadhuru watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna, Myebusi.
17 Car David voyant l'Ange qui frappait le peuple, parla à l'Eternel, et dit: Voici, c'est moi qui ai péché, c'est moi qui ai commis l'iniquité, mais ces brebis qu'ont-elles fait? Je te prie que ta main soit contre moi, et contre la maison de mon père.
Ikawa Daudi alipomwona huyo malaika aliyekuwa akiwaua watu, akamwambia Bwana, “Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Mkono wako uwe juu yangu na nyumba yangu.”
18 Et en ce jour-là Gad vint vers David, et lui dit: Monte, et dresse un autel à l'Eternel dans l'aire d'Arauna Jébusien.
Siku hiyo Gadi akamwendea Daudi na kumwambia, “Panda ukamjengee Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.”
19 Et David monta selon la parole de Gad, ainsi que l'Eternel l'avait commandé.
Kwa hiyo Daudi akakwea kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kwa kinywa cha Gadi.
20 Et Arauna regarda, et vit le Roi, et ses serviteurs qui venaient vers lui; et ainsi Arauna sortit, et se prosterna devant le Roi, le visage contre terre.
Arauna alipotazama na kumwona mfalme na watu wake wakija kumwelekea, alitoka nje na kusujudu mbele ya mfalme kifudifudi, akiuinamisha uso wake ardhini.
21 Et Arauna dit: Pour quel sujet le Roi mon Seigneur vient-il vers son serviteur? Et David répondit: Pour acheter ton aire, et y bâtir un autel à l'Eternel, afin que cette plaie soit arrêtée de dessus le peuple.
Arauna akasema, “Mbona bwana wangu mfalme amekuja kwa mtumishi wake?” Daudi akajibu, “Kununua sakafu yako ya kupuria, ili niweze kumjengea Bwana madhabahu, ili tauni iliyo katika watu iondolewe.”
22 Et Arauna dit à David: Que le Roi mon Seigneur prenne et offre ce qu'il lui plaira. Voilà des bœufs pour l'holocauste, et des chariots, et un attelage de bœufs au lieu de bois.
Arauna akamwambia Daudi, “Bwana wangu mfalme na achukue chochote kinachompendeza na akitoe sadaka. Hapa kuna maksai kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia kuna miti ya kupuria na nira za ngʼombe kwa ajili ya kuni.
23 Arauna donna tout cela au Roi [comme] un Roi. Et Arauna dit au Roi: L'Eternel ton Dieu veuille t'avoir pour agréable!
Ee mfalme, Arauna anatoa vyote hivi kwa mfalme.” Pia Arauna akamwambia mfalme, “Bwana Mungu wako na akukubali.”
24 Et le Roi répondit à Arauna: Non, mais je l'achèterai de toi pour un certain prix, et je n'offrirai point à l'Eternel mon Dieu des holocaustes qui ne me coûtent rien. Ainsi David acheta l'aire, et il [acheta aussi] les bœufs cinquante sicles d'argent.
Lakini mfalme akamjibu Arauna, “La hasha, nasisitiza kuvilipia. Sitatoa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana Mungu wangu isiyonigharimu chochote.” Kwa hiyo Daudi akanunua ile sakafu ya kupuria nafaka na maksai, akazilipia shekeli hamsini za fedha.
25 Puis David bâtit là un autel à l'Eternel, et offrit des holocaustes et des sacrifices de prospérités; et l'Eternel fut apaisé envers le pays, et la plaie fut arrêtée en Israël.
Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha Bwana akajibu kwa ajili ya nchi, nayo tauni ikakoma katika Israeli.

< 2 Samuel 24 >