< 2 Rois 15 >

1 La vingt-septième année de Jéroboam Roi d'Israël, Hazaria fils d'Amatsia Roi de Juda régnait.
Katika mwaka wa ishirini na saba wa Yeroboamu mfalme wa Israeli, Azaria mwana wa Amazia mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
2 Il était âgé de seize ans quand il commença à régner, et il régna cinquante-deux ans à Jérusalem; sa mère avait nom Jécolia, [et] était de Jérusalem.
Azaria alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala, na alitawala kwa mda wa miaka hamsini na mbili katika Yerusalemu. Mama yake alikuwa anaitwa Yekolia, na alikuwa anatokea Yerusalemu.
3 Il fit ce qui est droit devant l'Eternel, comme avait fait Amatsia son père.
Alifanya yaliyo mema machoni pa Yahwe, kama baba yake Amazia alivyofanya.
4 Tellement qu'il n'y eut que les hauts lieux qui ne furent point ôtés; le peuple sacrifiait encore et faisait des encensements sur les hauts lieux.
Lakini, mahali pa juu hapakuwa pameondolewa. Watu wakaendelea kutoa sadaka na kufukiza ubani katika mahala pa juu.
5 r l'Eternel frappa le Roi, qui fut lépreux jusqu'au jour qu'il mourut, et il demeura dans une maison séquestrée; et Jotham fils du Roi avait la charge de la maison, jugeant le peuple du pays.
Yhawe akampiga mfalme hivyo basi akawa na ukoma mpaka siku ya kifo chake na alikaa kwenye nyumba ya pekee. Yothamu, mtoto wa mfalme, alikuwa juu ya watu na kuwaongoza watu wa nchi.
6 Le reste des faits de Hazaria, tout ce, dis-je, qu'il a fait, n'est-il pas écrit au Livre des Chroniques des Rois de Juda?
Kama kwa mambo mengine yanayomhusu Azaria, yote aliyoyafanya, je hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
7 Et Hazaria s'endormit avec ses pères, et fut enseveli avec ses pères en la Cité de David, et Jotham son fils régna en sa place.
Hivyo Azaria alilala pamoja na babu zake katika mji wa Daudi. Yothamu, mtoto wake, akawa mfalme katika mahala pake.
8 La trente-huitième année de Hazaria Roi de Juda, Zacharie fils de Jéroboam commença à régner sur Israël à Samarie, [et il régna] six mois.
Katika mwaka wa thelathini na nane mwaka wa Azaria mfalme wa Yuda, Zekaria mwana wa Yeroboamu akatawala juu ya Israeli katika Samaria kwa miezi sita.
9 Et il fit ce gui déplaît à l'Eternel, comme avaient fait ses pères; il ne se détourna point des péchés de Jéroboam fils de Nébat, par lesquels il avait fait pécher Israël.
Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe, kama baba zake waliyoyafanya. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nabeti, ambaye alisababisha Israeli kuasi
10 Or Sallum fils de Jabés, fit une conspiration contre lui, et le frappa en la présence du peuple, et le tua, et il régna en sa place.
Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya njama dhidi ya Zekaria, akamshambulia katika Ibleamu, na kumuua. Kisha akawa mfalme katika mahala pake.
11 Quant au reste des faits de Zacharie, voilà, ils sont écrits au Livre des Chroniques des Rois d'Israël.
Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Zekaria, yameandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli.
12 C'est là la parole de l'Eternel laquelle il avait prononcée à Jéhu, en disant: Tes fils seront assis sur le trône d'Israël jusqu'à la quatrième génération; et il arriva ainsi.
Hili ndilo lililokuwa neno la Yahwe ambalo aliongea na Yehu, kusema, “Kizazi chako kitakaa katika kiti cha Israeli mpaka kizazi cha nne.” Hiyo ikatokea.
13 Sallum fils de Jabés commença à régner la trente-neuvième année d'Hozias Roi de Juda, et il ne régna que l'espace d'un mois entier à Samarie.
Shalumu mwana wa Yabeshi akaanza kutawala katika mwaka wa thelathini na tisa wa Azaria mfalme wa Yuda, na kutawala kwa mwezi mmoja tu katika Samaria.
14 Car Ménahem fils de Gadi, qui était de Tirtsa, monta, et entra dans Samarie, et frappa Sallum fils de Jabés à Samarie, et le tua, et il régna en sa place.
Menahemu mwana wa Gadi akapanda kutoka Tirza kwenda Samaria. Akamshambulia Shalumu mwana wa Yabeshi hapo, katika Samria. Akamuua na kuwa mfalme katika mahali pake.
15 Quant au reste des faits de Sallum, et quant à la conspiration qu'il fit, voilà, ces choses sont écrites au Livre des Chroniques des Rois d'Israël.
Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Shalumu na njama aliyoifanya, yameandikwa kwenye kitabu cha matukio cha wafle wa Israeli.
16 Et Ménahem battit Tiphsah, et tous ceux qui étaient dedans, et dans sa contrée, depuis Tirtsa, parce qu'elle ne lui avait point ouvert [les portes], et les tua; et il fendit toutes les femmes grosses qui s'y trouvèrent.
Ndipo Menahemu akamshambulia Tifsa na wote waliokuwa pale, na mipaka yote kuzunguka Tizra, kwasababu hawakufungua kwenye mji. Hivyo akaushambulia, na akawapasua wanawake wajawazito wote katika hicho kijiji.
17 La trente-neuvième année de Hazaria Roi de Juda, Ménahem fils de Gadi, commença à régner sur Israël, [il régna] dix ans en Samarie.
Katika mwaka wa thelathini na tisa wa Ahazia mfalme wa Yuda, Menahemu mwana wa Gadi akaanza kutawala; alitawala kwa miaka kumi katika Samaria.
18 Et il fit ce qui déplaît à l'Eternel; il ne se détourna point des péchés de Jéroboam fils de Nébat, par lesquels il avait fait pécher Israël, durant tout son temps.
Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe. Katika maisha yake yote, hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nabeti, ambaye alifanya Israeli kufanya dhambi.
19 Alors Pul, Roi des Assyriens, vint contre le pays; et Ménahem donna mille talents d'argent à Pul, afin qu'il lui aidât à affermir son Royaume entre ses mains.
Kisha Pulu mfalme wa Ashuru akaja kinyume cha nchi, na Menahemu akampatia Pulu talanta elfu moja za fedha, hivyo msaada wa Pulu ungeweza kuwa na yeye kuimarisha utawala wa Israeli katika nchi yake.
20 Et Ménahem tira cet argent d'Israël, de tous ceux qui étaient puissants en biens, pour le donner au Roi des Assyriens, de chacun cinquante sicles d'argent; ainsi le Roi des Assyriens s'en retourna, et ne s'arrêta point au pays.
Menahemu akatoza hii pesa kutoka Israeli kwa kumtaka kila mtu tajiri alipe shekeli hamsini za fedha kwake kumpatia mfalme wa Ashura. Hivyo mfalme wa Ashuru akarudi na hakukaa pale katika ile nchi.
21 Le reste des faits de Ménahem, tout ce, dis-je, qu'il a fait, n'est-il pas écrit au Livre des Chroniques des Rois d'Israël?
Kama kwa mabo mengine yanayomuhusu Menahemu, na yote aliyoyafanya, je hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya waflme wa Israeli?
22 Et Ménahem s'endormit avec ses pères, et Pékachia son fils régna en sa place.
Hivyo Menahemu akalala pamoja na babu zake, na Pekahia mtoto wake akawa mfalme katika mahala pake.
23 La cinquantième année d'Hazaria Roi de Juda, Pékachia fils de Ménahem commença à régner sur Israël à Samarie, [et il régna] deux ans.
Katika mwaka wa hamsini wa Azaria mfalme wa Yuda, Pekahia mwana wa Menahemu akaanza kutawala juu ya Israeli katika Samaria; alitawala kwa muda wa miaka miwili.
24 Et il fit ce qui déplaît à l'Eternel, et ne se détourna point des péchés de Jéroboam fils de Nébat, par lesquels il avait fait pécher Israël.
Alifanya yaliyo maovu usoni pa Yahwe. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nabeti, ambazo kwa hizo alisababisha Israeli kufanya dhambi.
25 Et Pékach fils de Rémalia son capitaine fit une conspiration contre lui, et le frappa à Samarie, au palais de la maison Royale, avec Argob et Arié, ayant avec soi cinquante hommes des enfants des Galaadites; ainsi il le tua, et il régna en sa place.
Pekahia alikuwa na afisa aliyekuwa anaitwa Peka mwana wa Remalia, ambaye alifanya njama dhidi yake. Pamoja na watu hamsini wa Gileadi, Peka akamuua Pekahia pamoja na Argobu na Arie katika Samaria, katika ngome ya nyumba ya mfalme. Peka akamuua alipomua Pekahia akawa mfalme katika mahala pake.
26 Le reste des actions de Pékachia, tout ce, dis-je, qu'il a fait, voilà, il est écrit au Livre des Chroniques des Rois d'Israël.
Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Pekahia, yote aliyoyafanya, yameandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli.
27 La cinquante et deuxième année d'Hazaria Roi de Juda, Pékach fils de Rémalia commença à régner sur Israël à Samarie, [et il régna] vingt ans.
Katika mwaka wa hamsini na mbili wa Azia mfalme wa Yuda, Peka mwana wa Remalia akaanza kutawala juu ya Israeli katika Samaria; alitawala miaka Ishirini.
28 Et il fit ce qui déplaît à l'Eternel, il ne se détourna point des péchés de Jéroboam fils de Nébat, par lesquels il avait fait pécher Israël.
Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe. Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nabati, ambaye alisababisha Israeli kufanya dhambi.
29 Aux jours de Pékach Roi d'Israël, Tiglath-piléser Roi des. Assyriens, vint, et prit Hijon, et Abel-bethmahaca, et Janoah, et Kédés, et Hatsor, et Galaad, et la Galilée, même tout le pays de Nephthali, et en transporta le peuple en Assyrie.
Katika siku za Peka mfalme wa Israeli, Tiglath Pileseri mfalme wa Ashuru akaja na kuichukua Iyoni, Abel Beth Maaka, Yanoa, Kadeshi, Hazori, Gileadi, na nchi yote ya Naftali. Akawachukua hao watu hadi Ashuru.
30 Or Hosée, fils d'Ela, fit une conspiration contre Pékach fils de Rémalia, et le frappa, et le tua, et il régna en sa place la vingtième année de Jotham fils de Hozias.
Hivyo Hoshea mwana wa Ela akafanya njama dhidi ya Peka mwana wa Remalia. Akaishambulia na kisha kumuua. Kisha akawa mfalme katika mahali pake, katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.
31 Le reste des faits de Pékach, tout ce, dis-je, qu'il a fait, voilà, il est écrit au Livre des Chroniques des Rois d'Israël.
Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Peka, yote aliyoyafanya, yameandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli.
32 La seconde année de Pékach fils de Rémalia Roi d'Israël, Jotham fils de Hozias, Roi de Juda commença à régner.
Katika mwaka wa pili wa Peka mwana wa Remalia, mfalme wa Israeli, Yothamu mwana wa Azaria, mfalme wa Yuda akaanza kutawala.
33 Il était âgé de vingt et cinq ans quand il commença à régner; et il régna seize ans à Jérusalem; sa mère avait nom Jérusa, [et] était fille de Tsadok.
Alikuwa na umri wa miaka ishirini alipoanza kutawala; alitawala kwa muda wa miaka kumi na sita katika Yerusalimu. Mama yake alikuwa anaitwa Yerusha; alikuwa binti ya Sadoki.
34 Il fit ce qui est droit devant l'Eternel; il fit comme Hozias son père avait fait.
Yotahmu alifanya yaliyo sahihi usoni pa Yahwe. Alifuata mfano wa yote baba yake Azaria aliyofanya.
35 De sorte qu'il n'y eut que les hauts lieux qui ne furent point ôtés, le peuple sacrifiait encore et faisait des encensements dans les hauts lieux; ce fut lui qui bâtit la plus haute porte de la maison de l'Eternel.
Ila, mahali pa juu hapakuchukuliwa. Watu walikuwa wakitio sadaka na kufukiza ubani katika mahali pa juu. Yothamu akajenga lango la juu la nyumba ya Yahwe.
36 Le reste des faits de Jotham, tout ce, dis-je, qu'il a fait, n'est-il pas écrit au Livre des Chroniques des Rois de Juda?
Kama kwa mambo mengine yanayomuhusu Yothamu, na yote aliyoyafanya, je yameandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?
37 En ces jours-là l'Eternel commença d'envoyer contre Juda Retsin Roi de Syrie et Pékach fils de Rémalia.
Katika zamani hizo Yahwe akaanza kumtuma dhidi ya Yuda Rezini mfalme wa Sahmu, na Peka mwana wa Remalia.
38 Et Jotham s'endormit avec ses pères, et fut enseveli en la Cité de David son père, et Achaz son fils régna en sa place.
Yothamu akalala pamoja na babu zake na akazikwa pamoja na babu zake katika mji wa Daudi, babu yake. Kisha Ahazi, mtoto wake, akwa mfalme katika mhali pake.

< 2 Rois 15 >