< 2 Chroniques 8 >

1 Or il arriva au bout des vingt ans, pendant lesquels Salomon bâtit la maison de l'Eternel, et sa maison;
Miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Solomoni alilijenga Hekalu la Bwana na jumba lake mwenyewe la kifalme,
2 Qu'il bâtit aussi les villes que Hiram lui avait données, et il y fit habiter les enfants d'Israël.
Solomoni akajenga tena vijiji vile ambavyo Hiramu alikuwa amempa, naye akawapa Waisraeli waishi humo.
3 Puis Salomon s'en alla à Hamath de Tsoba, et la conquit.
Kisha Solomoni akaenda Hamath-Soba na kuuteka.
4 Salomon bâtit aussi Tadmor au désert, et toutes les villes de munitions qu'il bâtit à Hamath.
Pia akajenga mji wa Tadmori katika jangwa na miji yote ya kuhifadhia vitu katika Hamathi.
5 Et il bâtit aussi Beth-horon la haute, et Beth-horon la basse, villes fortes de murailles, de portes, et de barres.
Akajenga tena Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, miji yenye ngome, kuta, malango na makomeo.
6 Et Bahalath, et toutes les villes de munitions qu'eut Salomon, et toutes les villes où il tenait ses chariots, et les villes où il tenait ses gens de cheval, et tout ce que Salomon prit plaisir de bâtir à Jérusalem, et au Liban, et dans tout le pays de sa domination.
Solomoni pia akajenga Baalathi na miji yake yote ya kuhifadhia vitu, na miji kwa ajili ya magari yake na kwa ajili ya farasi wake, chochote alichotaka kujenga katika Yerusalemu, katika Lebanoni na katika nchi yote aliyotawala.
7 Et quant à tout le peuple qui était resté des Héthiens, des Amorrhéens, des Phérésiens, des Héviens et des Jébusiens, qui n'étaient point d'Israël;
Watu wote waliosalia kutoka kwa Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi (haya mataifa hayakuwa Waisraeli),
8 D'entre les gens qui étaient restés après eux au pays, [et] que les enfants d'Israël n'avaient pas entièrement détruits, Salomon les rendit tributaires jusqu'à aujourd'hui.
yaani, wazao wao waliobakia katika nchi, ambao Waisraeli hawakuwa wamewaangamiza: hawa Solomoni akawalazimisha kuwa watumwa katika shokoa, kama ilivyo hadi leo.
9 Mais Salomon ne souffrit point que les enfants d'Israël fussent asservis à faire son ouvrage, mais ils étaient gens de guerre, et principaux Chefs de ses capitaines, et Chefs de ses chariots, et ses hommes d'armes.
Lakini Solomoni hakuwafanya Waisraeli watumwa kwa ajili ya kazi yake, bali walikuwa wapiganaji, majemadari, maafisa wake, majemadari wa magari yake ya vita na waendesha magari ya vita.
10 Il y en avait aussi deux cent cinquante, qui étaient les principaux Chefs de ceux qui étaient établis [sur les ouvrages] du Roi Salomon, lesquels avaient l'intendance sur le peuple.
Pia walikuwa maafisa wakuu wa Mfalme Solomoni, yaani, maafisa wakaguzi 250 waliosimamia watu.
11 Or Salomon fit monter la fille de Pharaon de la Cité de David en la maison qu'il lui avait bâtie; car il dit: Ma femme n'habitera point dans la maison de David Roi d'Israël, parce que les lieux auxquels l'Arche de l'Eternel est entrée sont saints.
Solomoni akampandisha mke wake binti Farao kutoka Mji wa Daudi na kumleta jumba la kifalme alilokuwa amemjengea, kwa kuwa alisema, “Mke wangu hataishi katika jumba la kifalme la Daudi mfalme wa Israeli, kwa sababu mahali ambapo Sanduku la Bwana limefika ni patakatifu.”
12 Et Salomon offrait des holocaustes à l'Eternel, sur l'autel de l'Eternel, qu'il avait bâti vis-à-vis du porche.
Mfalme Solomoni akamtolea Bwana dhabihu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana ambayo alikuwa ameijenga mbele ya ukumbi,
13 Et même selon qu'il échéait chaque jour, offrant selon le commandement de Moïse aux jours de Sabbat, et aux nouvelles lunes, et aux fêtes solennelles, trois fois l'année, [savoir] en la fête solennelle des pains sans levain, en la fête solennelle des semaines, et en la fête solennelle des Tabernacles.
kulingana na mahitaji ya kila siku kwa ajili ya sadaka zilizoamriwa na Mose kwa ajili ya Sabato, Mwezi Mwandamo na sikukuu nyingine tatu za mwaka, yaani, Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma na Sikukuu ya Vibanda.
14 Et il établit, suivant ce qu'avait ordonné David son père, les départements des Sacrificateurs selon leur ministère, et les Lévites selon leurs charges, afin qu'ils louassent [Dieu], et qu'ils fissent le service, aidant les Sacrificateurs selon l'ordinaire de chaque jour. [Il établit aussi] les portiers en leurs départements à chaque porte; car tel avait été le commandement de David homme de Dieu.
Kwa kushika maagizo ya Daudi baba yake, aliweka migawanyo ya makuhani kwa ajili ya kazi zao, nao Walawi kuongoza kusifu na kusaidia makuhani kufuatana na mahitaji ya kila siku. Pia akaweka mabawabu katika migawanyo kwa ajili ya malango mbalimbali, kwa sababu hili ndilo Daudi mtu wa Mungu alilokuwa ameagiza.
15 Et on ne s'écarta point du commandement du Roi touchant les Sacrificateurs et les Lévites, en aucun article, ni en ce qui regardait les trésors.
Nao hawakuziacha amri za mfalme alizoamuru makuhani au Walawi katika jambo lolote, ikiwa ni pamoja na zile za hazina.
16 Tout l'ouvrage donc de Salomon ayant été bien préparé, jusqu'au jour que la maison de l'Eternel fut fondée, et jusqu'à ce qu'elle fut achevée, la maison de l'Eternel fut ainsi finie.
Kazi yote ya Mfalme Solomoni ilifanyika kuanzia siku msingi wa Hekalu la Bwana ulipowekwa mpaka kukamilika kwake. Kwa hiyo Hekalu la Bwana likamalizika kujengwa.
17 Alors Salomon s'en alla à Hetsjon-guéber, et à Eloth, sur le rivage de la mer, qui est au pays d'Edom.
Ndipo Solomoni akaenda Esion-Geberi na Elathi katika pwani ya Edomu.
18 Et Hiram lui envoya, sous la conduite de ses serviteurs, des navires, et des serviteurs expérimentés dans la marine, qui s'en allèrent avec les serviteurs de Salomon à Ophir; et ils prirent de là quatre cent cinquante talents d'or, et les apportèrent au Roi Salomon.
Naye Hiramu alimpelekea meli zilizoongozwa na maafisa wake mwenyewe, watu waliokuwa na ujuzi wa baharini. Hawa watu pamoja na wale wa Solomoni wakasafiri kwa bahari mpaka Ofiri, wakaleta kutoka huko talanta 450 za dhahabu, ambazo walimkabidhi Mfalme Solomoni.

< 2 Chroniques 8 >