< 2 Chroniques 31 >

1 Or sitôt qu'on eut achevé toutes ces choses, tous ceux d'Israël qui s'étaient trouvés là, allèrent par les villes de Juda, et brisèrent les statues, et coupèrent les bocages, et démolirent les hauts lieux, et les autels de tout Juda et Benjamin, et ils en firent de même en Ephraïm et en Manassé, jusqu'à détruire tout; puis tous les enfants d'Israël retournèrent chacun en sa possession dans leurs villes.
Baada ya mambo haya yote kumalizika, Waisraeli ambao walikuwako huko wakaenda kwenye miji ya Yuda, wakayavunja yale mawe ya kuabudia na kuzikatakata zile nguzo za Ashera. Wakabomoa mahali pa juu pa kuabudia miungu pamoja na madhabahu zake kila mahali katika Yuda na Benyamini na katika Efraimu na Manase. Baada ya kuviharibu hivi vyote, Waisraeli wakarudi katika miji yao wenyewe na kwenye milki zao.
2 Ezéchias aussi rétablit les départements des Sacrificateurs et des Lévites, selon les départements qui en avaient été faits, chacun selon son ministère, tant les Sacrificateurs, que les Lévites, pour les holocaustes, et pour les sacrifices de prospérités, afin de faire le service, de célébrer, et de chanter les louanges [de Dieu] aux portes du camp de l'Eternel.
Hezekia akawapanga makuhani na Walawi katika migawanyo, kila mgawanyo kulingana na wajibu wao, kama ni makuhani au Walawi, ili kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, kuhudumu, kushukuru na kuimba sifa katika malango ya makao ya Bwana.
3 Il fit aussi une ordonnance par laquelle le Roi serait chargé d'une contribution prise de ses finances pour les holocaustes, [savoir] pour les holocaustes du matin et du soir, et pour les holocaustes des Sabbats, et des nouvelles lunes, et des fêtes solennelles, selon qu'il est écrit dans la Loi de l'Eternel.
Mfalme akatoa matoleo kutoka mali zake mwenyewe kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa za asubuhi na za jioni na sadaka za kuteketezwa kwa siku za Sabato, kwa Sikukuu za Mwezi Mwandamo na kwa ajili ya sikukuu zilizoamriwa kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana.
4 Et il dit au peuple, [savoir] aux habitants de Jérusalem, qu'ils donnassent la portion des Sacrificateurs et des Lévites, afin qu'ils prissent courage [pour observer] la Loi de l'Eternel.
Akawaagiza watu wanaoishi Yerusalemu watoe sehemu iliyo haki ya makuhani na Walawi ili waweze kujitoa kikamilifu kutimiza wajibu wao katika Sheria ya Bwana.
5 Et sitôt que la chose fut publiée, les enfants d'Israël apportèrent en abondance les prémices du froment, du vin, de l'huile, du miel, et de tout le provenu des champs, ils apportèrent, [dis-je], les dîmes de toutes ces choses en abondance.
Mara tu baada ya kutolewa tangazo hilo, Waisraeli wakatoa kwa ukarimu malimbuko ya nafaka zao, divai mpya, mafuta na asali pamoja na vyote vilivyotoka mashambani. Wakaleta kiasi kikubwa cha fungu la kumi la kila kitu.
6 Et les enfants d'Israël et de Juda, qui habitaient dans les villes de Juda, apportèrent aussi les dîmes du gros et du menu bétail, et les dîmes des choses saintes, qui étaient consacrées à l'Eternel leur Dieu; et les mirent par monceaux.
Watu wa Israeli na Yuda walioishi katika miji ya Yuda wakaleta pia fungu la kumi la makundi yao ya ngʼombe na makundi ya kondoo na mbuzi pia na fungu la kumi la vitu vitakatifu vilivyowekwa wakfu kwa ajili ya Bwana Mungu wao na kuvikusanya katika malundo.
7 Ils commencèrent au troisième mois de faire les premiers monceaux, et au septième mois ils les achevèrent.
Wakaanza kufanya haya katika mwezi wa tatu na kumaliza katika mwezi wa saba.
8 Alors Ezéchias et les principaux vinrent, virent les monceaux, et bénirent l'Eternel et son peuple d'Israël.
Wakati Hezekia na maafisa wake walipokuja na kuona yale malundo, wakamsifu Bwana na kuwabariki watu wake Israeli.
9 Puis Ezéchias s'informa des Sacrificateurs et des Lévites touchant ces monceaux.
Hezekia akawauliza makuhani na Walawi kuhusu yale malundo,
10 Et Hazaria le principal Sacrificateur, qui était de la famille de Tsadoc, lui répondit, et [lui] dit: Depuis qu'on a commencé d'apporter des offrandes dans la maison de l'Eternel, nous avons mangé, et nous avons été rassasiés, et il en est resté en grande abondance; car l'Eternel a béni son peuple, et cette grande quantité est ce qu'il y a eu de reste.
naye Azaria aliyekuwa kuhani mkuu, kutoka jamaa ya Sadoki, akajibu, “Tangu watu walipoanza kuleta sadaka zao katika Hekalu la Bwana tumekuwa na chakula cha kutosha na vingi vya kuweka akiba kwa sababu Bwana amewabariki watu wake, hivyo tumekuwa na kiasi kingi kilichobaki.”
11 Alors Ezéchias commanda qu'on préparât des chambres dans la maison de l'Eternel; et ils les préparèrent.
Hezekia akatoa agizo la kutengeneza vyumba vya ghala katika Hekalu la Bwana nalo hili likafanyika.
12 Puis ils portèrent dedans fidèlement les offrandes, et les dîmes, et les choses consacrées, et Conania Lévite en eut l'intendance, et Simhi son frère était commis sous lui.
Kisha kwa uaminifu wakaleta sadaka zao, mafungu yao ya kumi na vitu vilivyowekwa wakfu. Konania Mlawi, ndiye alikuwa msimamizi wa vitu hivi na Shimei ndugu yake ndiye alikuwa msaidizi wake.
13 Et Jéhiël, Hazazia, Nahath, Hasaël, Jérimoth, Jozabad, Eliël, Jismacia, Mahath, et Bénaia étaient commis sous la conduite de Conania, et de Simhi son frère, par le commandement du Roi Ezéchias, et de Hazaria Gouverneur de la maison de Dieu.
Yehieli, Azazia, Nahathi, Asaheli, Yeremothi, Yozabadi, Elieli, Ismakia, Mahathi na Benaya walikuwa waangalizi chini ya Konania na Shimei ndugu yake, waliokuwa wamewekwa na Mfalme Hezekia na Azaria, afisa msimamizi wa Hekalu la Mungu.
14 Et Coré fils de Jimna Lévite, qui était portier vers l'Orient, avait la charge des choses qui étaient volontairement offertes à Dieu pour fournir l'offrande élevée de l'Eternel, et les choses très-saintes.
Kore mwana wa Imna, Mlawi, bawabu wa Lango la Mashariki, alikuwa msimamizi wa sadaka za hiari zilizotolewa kwa Mungu, akiyagawanya hayo matoleo yaliyotolewa kwa Bwana na pia zile sadaka zilizowekwa wakfu.
15 Et il avait sous sa conduite Héden, Minjamin, Jésuah, Sémahia, Amaria, et Sécania, dans les villes des Sacrificateurs, ayant cette charge d'ordinaire, pour distribuer les portions à leurs frères, tant aux plus petits qu'aux plus grands.
Edeni, Miniamini, Yeshua, Shemaya, Amaria na Shekania walimsaidia kwa uaminifu katika miji ya makuhani, wakiwagawia makuhani wenzao kufuatana na migawanyo yao, wazee kwa vijana sawasawa.
16 Outre cela on fit un dénombrement selon les généalogies des mâles d'entre eux, depuis ceux de trois ans, et au dessus, [savoir] de tous ceux qui entraient dans la maison de l'Eternel, pour y faire ce qu'il y fallait faire chaque jour, selon leur ministère et leurs charges, suivant leurs départements.
Zaidi ya hao wakawagawia wanaume wenye umri wa miaka mitatu au zaidi ambao majina yao yalikuwa kwenye orodha ya vizazi, wale wote ambao wangeingia katika Hekalu la Bwana ili kufanya kazi zao mbalimbali za kila siku kulingana na wajibu katika mgawanyo wao.
17 Et outre le dénombrement que l'on fit des Sacrificateurs selon leur généalogie et selon la maison de leurs pères, et des Lévites, depuis ceux de vingt ans et au dessus, selon leurs départements;
Kuandikishwa kwa makuhani kulikuwa kwa kufuata chimbuko la nyumba za baba zao na Walawi kuanzia umri wa miaka ishirini au zaidi ilikuwa kufuatana na huduma zao, kwa migawanyo yao.
18 On fit aussi un dénombrement selon leurs généalogies de toutes leurs familles, de leurs femmes, de leurs fils, et de leurs filles, pour toute l'assemblée, et en toute sincérité ils se sanctifiaient avec soin.
Makuhani waliandikishwa pamoja na watoto wao wadogo, wake zao, watoto wao wa kiume na wa kike, jamii yote iliandikishwa kwa kufuata orodha ya vizazi vyao. Kwa kuwa walikuwa waaminifu katika kujitakasa.
19 Et quant aux enfants d'Aaron Sacrificateurs, qui étaient à la campagne et dans les faubourgs de leurs villes, dans chaque ville, il y avait des gens nommés par leur nom, pour distribuer la portion à tous les mâles des Sacrificateurs, et à tous ceux des Lévites dont on avait fait le dénombrement selon leur généalogie.
Kuhusu makuhani, wazao wa Aroni walioishi kwenye mashamba yaliyozunguka miji yao au katika miji mingine yoyote, watu walitajwa majina ili kumgawia kila mwanaume miongoni mwao na kwa wote waliokuwa katika orodha ya vizazi vya Walawi.
20 Ezéchias en fit ainsi par tout Juda, et il fit ce qui est bon, et droit, et véritable, en la présence de l'Eternel son Dieu.
Hivi ndivyo Hezekia alivyofanya katika Yuda yote, akifanya lile lililo jema, sawa na la uaminifu mbele za Bwana Mungu wake.
21 Et il travailla de tout son cœur dans tout l'ouvrage qu'il entreprit pour le service de la maison de Dieu, et dans la Loi, et dans les commandements, recherchant son Dieu; et il prospéra.
Naye katika kila kitu alichofanya katika huduma kwenye Hekalu la Mungu na katika utii kwa sheria na amri, alimtafuta Mungu wake na kufanya kazi kwa moyo wake wote. Naye hivyo akafanikiwa.

< 2 Chroniques 31 >