< 2 Chroniques 27 >
1 Jotham était âgé de vingt-cinq ans quand il commença à régner, et il régna seize ans à Jérusalem. Sa mère avait nom Jérusa, et elle était fille de Tsadoc.
Yothamu alikuwa na umri wa mika ishirini na mitano alipoanza kutawala; alitawala miaka kumi na sita katika Yerusalemu. Jina la mama yake lilikuwa Yerusha; alikuwa binti Sadoki.
2 Il fit ce qui est droit devant l'Eternel, comme Hozias son père avait fait, mais il n'entra pas [comme lui] au Temple de l'Eternel; néanmoins le peuple se corrompait encore.
Akafanya yaliyomema katika macho ya Yawe, akiufuta mfano wa baba yake, Uzia, katika mabo yote. Pia alijiepusha kuingia katika hekalu la Yahwe. Lakini watu bado walikuwa wanaenda katika njia za uovu.
3 Il bâtit la plus haute porte de la maison de l'Eternel; il bâtit beaucoup en la muraille d'Hophel.
Akalijenga tena lango la juu la nyumba ya Yahwe, na juu ya kilima cha Ofeli akajenga sana.
4 Il bâtit aussi des villes sur les montagnes de Juda, et des châteaux, et des tours dans les forêts.
Vilevile alijenga miji katika kilima cha Yuda, na katika mistu alijenga ngome na minara.
5 Et il combattit contre le Roi des enfants de Hammon, et fut le plus fort; et cette année-là les enfants de Hammon lui donnèrent cent talents d'argent, et dix mille Cores de blé, et dix mille d'orge. les enfants de Hammon lui donnèrent ces choses-là, même la seconde et la troisième année.
Pia alipigana na mfalme wa watu wa Amoni na akawashinda. Katika mwaka huo huo, watu wa Amoni walimpa talanta mia moja za fedha, kori elfu kumi za ngano, kori elfu kumi za shayiri. Watu wa Amoni wakampa hivyo hivyo katika mwaka wa pili na wa tatu.
6 Jotham devint donc fort puissant, parce qu'il avait dirigé ses voies devant l'Eternel son Dieu.
Kwa hiyo Yothamu akawa na nguvu sana kwa sababu alitembea imara mbele za Yahwe Mungu wake.
7 Le reste des faits de Jotham, et tous ses combats et sa conduite, voilà, toutes ces choses sont écrites au Livre des Rois d'Israël et de Juda.
Kwa mambo mengine kuhusu Yothamu, vita vyake vyote, na njia zake zote, ona, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
8 Il était âgé de vingt-cinq ans quand il commença à régner, et il régna seize ans à Jérusalem.
Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; alitawala kwa miaka kumi na sita kataika Yerusalemu.
9 Puis Jotham s'endormit avec ses pères, et on l'ensevelit en la Cité de David; et Achaz son fils régna en sa place.
Yothamu akalala pamoja na babu zake, na wakamzika katika mji wa Daudi. Ahazi, mwanaye, akawa mfalme katika nafasi yake.