< 2 Chroniques 27 >
1 Jotham était âgé de vingt-cinq ans quand il commença à régner, et il régna seize ans à Jérusalem. Sa mère avait nom Jérusa, et elle était fille de Tsadoc.
Yothamu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita. Mama yake aliitwa Yerusha binti Sadoki.
2 Il fit ce qui est droit devant l'Eternel, comme Hozias son père avait fait, mais il n'entra pas [comme lui] au Temple de l'Eternel; néanmoins le peuple se corrompait encore.
Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana kama Uzia baba yake alivyokuwa amefanya, lakini tofauti na yeye, hakuingilia huduma za hekaluni mwa Bwana. Lakini hata hivyo, watu wakaendelea na desturi zao mbaya.
3 Il bâtit la plus haute porte de la maison de l'Eternel; il bâtit beaucoup en la muraille d'Hophel.
Yothamu akajenga upya Lango la Juu la Hekalu la Bwana na kufanya kazi kubwa kwenye ukuta katika kilima cha Ofeli.
4 Il bâtit aussi des villes sur les montagnes de Juda, et des châteaux, et des tours dans les forêts.
Akajenga miji katika vilima vya Yuda pamoja na ngome na minara mwituni.
5 Et il combattit contre le Roi des enfants de Hammon, et fut le plus fort; et cette année-là les enfants de Hammon lui donnèrent cent talents d'argent, et dix mille Cores de blé, et dix mille d'orge. les enfants de Hammon lui donnèrent ces choses-là, même la seconde et la troisième année.
Yothamu akafanya vita na mfalme wa Waamoni na kumshinda. Mwaka ule Waamoni wakamlipa talanta 100 za fedha, kori 10,000 za ngano na kori 10,000 za shayiri. Waamoni wakamletea kiasi hicho hicho mwaka wa pili na wa tatu.
6 Jotham devint donc fort puissant, parce qu'il avait dirigé ses voies devant l'Eternel son Dieu.
Yothamu akaendelea kuwa na nguvu kwa sababu alienenda kwa ukamilifu mbele za Bwana Mungu wake.
7 Le reste des faits de Jotham, et tous ses combats et sa conduite, voilà, toutes ces choses sont écrites au Livre des Rois d'Israël et de Juda.
Matukio mengine ya utawala wa Yothamu, pamoja na vita vyake vyote na vitu vingine alivyofanya, vimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
8 Il était âgé de vingt-cinq ans quand il commença à régner, et il régna seize ans à Jérusalem.
Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na sita.
9 Puis Jotham s'endormit avec ses pères, et on l'ensevelit en la Cité de David; et Achaz son fils régna en sa place.
Yothamu akalala na baba zake na akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Ahazi mwanawe akawa mfalme baada yake.