< 2 Chroniques 14 >

1 Puis Abija s'endormit avec ses pères, et on l'ensevelit dans la Cité de David, et Asa son fils régna en sa place. De son temps le pays fut en repos durant dix ans.
Naye Abiya akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akawa mfalme baada yake. Katika siku zake, nchi ikawa na amani kwa miaka kumi.
2 Or Asa fit ce qui est bon et droit devant l'Eternel son Dieu.
Asa akatenda yaliyo mema na haki machoni pa Bwana Mungu wake.
3 Car il ôta les autels [des dieux] des étrangers, et les hauts lieux, et brisa les statues, et coupa les bocages.
Akaziondoa madhabahu za kigeni na mahali pa juu pa kuabudia miungu, akayavunja yale mawe ya kuabudiwa na kuzikatakata nguzo za Maashera.
4 Et il commanda à Juda de rechercher l'Eternel le Dieu de leurs pères, et d'observer la Loi et les Commandements.
Akawaamuru Yuda kumtafuta Bwana, Mungu wa baba zao na kutii sheria zake na amri zake.
5 Et il ôta aussi de toutes les villes de Juda les hauts lieux et les tabernacles; et le Royaume fut en repos sous sa conduite.
Akaondoa mahali pa juu pa kuabudia miungu na madhabahu za kufukizia uvumba kwenye kila mji katika Yuda, nao ufalme ulikuwa na amani katika utawala wake.
6 Il bâtit aussi des villes fortes en Juda, parce que le pays était en repos; et pendant ces années-là il n'y eut point de guerre contre lui, parce que l'Eternel lui donnait du repos.
Akajenga miji yenye ngome katika Yuda, wakati nchi ikiwa na amani. Hakuna mtu yeyote aliyepigana vita naye katika miaka hiyo, kwa kuwa Bwana alimstarehesha.
7 Car il dit à Juda: Bâtissons ces villes, et entourons-les de murailles, de tours, de portes, et de barres, pendant que nous sommes maîtres du pays; parce que nous avons invoqué l'Eternel notre Dieu; nous l'avons invoqué, et il nous a donné du repos tout alentour; c'est pourquoi ils bâtirent, et prospérèrent.
Mfalme akawaambia Yuda, “Tuijenge hii miji na tuizungushie kuta, pamoja na minara, malango na makomeo. Nchi bado ni yetu, kwa sababu tumemtafuta Bwana Mungu wetu, tulimtafuta naye ametupa raha kila upande.” Hivyo wakajenga na wakafanikiwa.
8 Or Asa avait en son armée trois cent mille hommes de ceux de Juda, portant le bouclier et la javeline; et deux cent quatre-vingt mille de ceux de Benjamin, portant le bouclier, et tirant de l'arc, tous forts et vaillants.
Asa alikuwa na jeshi la watu 300,000 kutoka Yuda, wenye ngao kubwa na mikuki na jeshi la watu 280,000 kutoka Benyamini, wenye ngao ndogo na pinde. Watu hawa wote walikuwa wapiganaji mashujaa.
9 Et Zeraph Ethiopien sortait contr'eux avec une armée d'un million [d'hommes], et de trois cents chariots, et il vint jusqu'à Marésa.
Zera Mkushi akatoka kupigana dhidi yao akiwa na jeshi la watu maelfu ya maelfu na magari ya vita 300, nao wakaja mpaka Maresha.
10 Et Asa alla au devant de lui, et on rangea la bataille en la vallée de Tséphath, près de Marésa.
Asa akatoka kumkabili, nao wakapanga vita katika Bonde la Sefatha karibu na Maresha.
11 Alors Asa cria à l'Eternel son Dieu, et dit: Eternel! Il ne t'est pas plus difficile d'aider celui qui n'a point de force, que celui qui a des gens en grand nombre. Aide-nous, ô Eternel notre Dieu! car nous nous sommes appuyés sur toi; et nous sommes venus en ton Nom contre cette multitude. Tu es l'Eternel notre Dieu; que l'homme n'ait point de force contre toi!
Kisha Asa akamlilia Bwana Mungu wake na kusema, “Ee Bwana, hakuna yeyote aliye kama wewe wa kuwasaidia wasio na nguvu dhidi ya wenye nguvu. Utusaidie, Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, kwa kuwa tunakutumainia wewe, nasi kwa jina lako tumekuja dhidi ya jeshi hili kubwa. Ee Bwana, wewe ndiwe Mungu wetu, usiwaache wanadamu wakushinde wewe.”
12 Et l'Eternel frappa les Ethiopiens devant Asa et devant Juda; en sorte que les Ethiopiens s'enfuirent.
Bwana akawapiga Wakushi mbele ya Asa na Yuda. Wakushi wakakimbia,
13 Et Asa et le peuple qui était avec lui les poursuivirent jusqu'à Guérar; et il tomba tant d'Ethiopiens, qu'ils n'eurent plus aucune force; car ils furent défaits devant l'Eternel, et devant son armée; et on en rapporta un fort grand butin.
naye Asa na jeshi lake wakawafuatia mpaka Gerari. Idadi kubwa ya Wakushi ilianguka hata wasiweze kuinuka tena, wakapondapondwa mbele za Bwana na majeshi yake.
14 Ils frappèrent aussi toutes les villes qui étaient autour de Guérar, parce que la terreur de l'Eternel était sur eux; et ils pillèrent toutes ces villes; car il y avait dans ces villes [de quoi faire] un grand butin.
Watu wa Yuda wakachukua nyara nyingi sana, wakaangamiza vijiji vyote vinavyoizunguka Gerari, kwa kuwa hofu ya Bwana ilikuwa imewaangukia. Wakateka nyara vijiji hivi vyote, kwani kulikuwepo nyara nyingi huko.
15 Ils abattirent aussi les tentes des troupeaux, et emmenèrent quantité de brebis et de chameaux; après quoi ils s'en retournèrent à Jérusalem.
Pia wakashambulia kambi za wachunga makundi ya wanyama wakachukua na kuyaswaga makundi ya kondoo, mbuzi na ngamia. Kisha wakarudi Yerusalemu.

< 2 Chroniques 14 >