< 2 Chroniques 12 >

1 Or il arriva qu'aussitôt que le Royaume de Roboam fut établi et fortifié, [Roboam] abandonna la Loi de l'Eternel, et tout Israël [l'abandonna aussi] avec lui.
Baada ya nafasi ya Rehoboamu kuimarika na kuwa na nguvu, yeye na Israeli yote waliiacha sheria ya Bwana Mungu.
2 C'est pourquoi il arriva que la cinquième année du Roi Roboam, Sisak Roi d'Egypte monta contre Jérusalem, parce qu'ils avaient péché contre l'Eternel.
Kwa sababu hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu.
3 Il avait avec lui mille deux cents chariots, et soixante mille hommes de cheval, et le peuple qui était venu avec lui d'Egypte, [savoir], les Libyens, les Sukiens, et les Ethiopiens, était sans nombre.
Akiwa na magari ya vita 1,200 na wapanda farasi 60,000 na idadi isiyohesabika ya majeshi ya Walibia, Wasukii na Wakushi yaliyokuja pamoja naye kutoka Misri.
4 Et il prit les villes fortes qui appartenaient à Juda, et vint jusqu'à Jérusalem.
Akateka miji ya Yuda yenye ngome akaendelea mpaka Yerusalemu.
5 Alors Sémahia le Prophète vint vers Roboam, et vers les principaux de Juda qui s'étaient assemblés à Jérusalem à cause de Sisak, et leur dit: Ainsi a dit l'Eternel: Vous m'avez abandonné, c'est pourquoi je vous ai aussi abandonnés entre les mains de Sisak.
Ndipo nabii Shemaya akaja kwa Rehoboamu na kwa viongozi wa Yuda waliokuwa wamekusanyika huko Yerusalemu kwa ajili ya hofu ya Shishaki naye akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Ninyi mmeniacha mimi, kwa hiyo, mimi nami sasa ninawaacha ninyi mkononi mwa Shishaki.’”
6 Alors les principaux d'Israël et le Roi s'humilièrent, et dirent: L'Eternel est juste.
Viongozi wa Israeli na mfalme wakajinyenyekeza na kusema, “Bwana Mungu ni mwenye haki.”
7 Et quand l'Eternel eut vu qu'ils s'étaient humiliés, la parole de l'Eternel fut adressée à Sémahia, en disant: Ils se sont humiliés, je ne les détruirai point, mais je leur donnerai dans peu de temps quelque moyen d'échapper, et ma fureur ne se répandra point sur Jérusalem par le moyen de Sisak.
Bwana Mungu alipoona kwamba wamejinyenyekeza, neno hili la Bwana likamjia Shemaya: “Maadamu wamejinyenyekeza, sitawaangamiza bali hivi karibuni nitawapatia wokovu. Ghadhabu yangu haitamwagwa juu ya Yerusalemu kwa kupitia Shishaki.
8 Toutefois ils lui seront asservis, afin qu'ils sachent ce que c'est que de ma servitude, et de la servitude des Royaumes de la terre.
Hata hivyo, watamtumikia Shishaki ili wapate kujifunza tofauti kati ya kunitumikia mimi na kuwatumikia wafalme wa nchi nyingine.”
9 Sisak donc Roi d'Egypte monta contre Jérusalem, et prit les trésors de la maison de l'Eternel, et les trésors de la Maison Royale, il prit tout; il prit aussi les boucliers d'or que Salomon avait faits.
Shishaki mfalme wa Misri alipoishambulia Yerusalemu, alichukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
10 Et le Roi Roboam fit des boucliers d'airain au lieu de ceux-là, et les mit entre les mains des capitaines des archers qui gardaient la porte de la maison du Roi.
Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
11 Et quand le Roi entrait dans la maison de l'Eternel, les archers venaient, et les portaient, puis ils les rapportaient dans la chambre des archers.
Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana walinzi walikwenda pamoja naye wakiwa wamebeba hizo ngao na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
12 Parce donc qu'il s'humilia, la colère de l'Eternel se détourna de lui, en sorte qu'il ne les détruisit point entièrement; car aussi il y avait de bonnes choses en Juda.
Kwa sababu Rehoboamu alijinyenyekeza, hasira ya Bwana ikageukia mbali naye, hakuangamizwa kabisa. Kukawa na hali nzuri katika Yuda.
13 Ainsi le Roi Roboam se fortifia dans Jérusalem, et régna. Or Roboam était âgé de quarante et un ans, quand il commença à régner, et il régna dix-sept ans à Jérusalem, la ville que l'Eternel avait choisie d'entre toutes les Tribus d'Israël pour y mettre son Nom; et sa mère avait nom Nahama, et était Hammonite.
Mfalme Rehoboamu akajiweka imara katika Yerusalemu na akaendelea kuwa mfalme. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na saba, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli ili aliweke Jina lake humo. Mama yake aliitwa Naama, alikuwa Mwamoni.
14 Mais il fit ce qui est déplaisant à [l'Eternel]; car il ne disposa point son cœur pour chercher l'Eternel.
Rehoboamu akatenda maovu kwa sababu hakuuelekeza moyo wake katika kumtafuta Bwana Mungu.
15 Or les faits de Roboam, tant les premiers que les derniers, ne sont-ils pas écrits dans les Livres de Sémahia le Prophète, et de Hiddo le Voyant, dans le récit des généalogies; avec les guerres que Roboam et Jéroboam ont eues tout le temps qu'ils ont vécu?
Kwa habari ya matukio katika utawala wa Rehoboamu, tangu mwanzo mpaka mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Shemaya na mwonaji Ido zinazohusiana na vizazi? Kulikuwako na vita mara kwa mara kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
16 Et Roboam s'endormit avec ses pères, et fut enseveli en la Cité de David; et Abija son fils régna en sa place.
Rehoboamu akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Chroniques 12 >