< 1 Samuel 24 >
1 Et quand Saül fut revenu de la poursuite des Philistins, on lui fit ce rapport, disant: Voilà David au désert de Hen-guédi.
Sauli aliporudi kuwafukuza Wafilisti, akaambiwa kwamba, “Daudi yuko katika jangwa la Engedi.”
2 Alors Saül prit trois mille hommes d'élite de tout Israël, et il s'en alla chercher David et ses gens, jusques sur le haut des rochers des chamois.
Ndipo Sauli akachukua watu elfu tatu waliochaguliwa kutoka Iraeli yote, wakaenda kumtafuta Daudi na watu wake katika miamba ya Mbuzi Mwitu.
3 Et Saül vint aux parcs des brebis auprès du chemin, où il y avait une caverne en laquelle il entra pour ses nécessités; et David et ses gens se tenaient au fond de la caverne.
Akafika penye mazizi ya kondoo kando ya njia, mahali palipokuwa na pango. Sauli akaingia ndani yake kujisaidia. Wakati huo Daudi na watu wake walikuwa wamekaa mbali zaidi ndani ya pango lilelile.
4 Et les gens de David lui dirent: Voici le jour dont l'Eternel t'a dit: Voici, je te livre ton ennemi entre tes mains, afin que tu lui fasses selon qu'il te semblera bon. Et David se leva, et coupa tout doucement le pan du manteau de Saül.
Watu wake Daudi wakamwambia, “Hii ndiyo siku ambayo BWANA aliisema akikuambia, 'Nitamweka adui wako mkononi mwako, ili umtendee kama unavyotaka.”' Kisha Daudi akainuka na kumnyemelea kwa mbele kimya kimya na kulikata pindo la kanzu ya Sauli.
5 Après cela David fut touché en son cœur de ce qu'il avait coupé le pan [du manteau] de Saül.
Baadaye moyo wa Daudi ukamchoma kwa sababu alilikata pindo la kanzu ya Sauli.
6 Et il dit à ses gens: Que l'Eternel me garde de commettre une telle action contre mon Seigneur, l'Oint de l'Eternel, en mettant ma main sur lui; car il est l'Oint de l'Eternel.
Akawaambia watu wake, “BWANA anisamehe, sikupaswa kumtendea jambo hili bwana wangu, Mtiwa mafuta wa BWANA, kwa kunyoosha mkono wangu juu yake, maana yeye ni masihi wa BWANA.”
7 Ainsi David détourna ses gens par ses paroles, et il ne leur permit point de s'élever contre Saül. Puis Saül se leva de la caverne, et s'en alla son chemin.
Hivyo Daudi akawakemea watu wake kwa maneno haya, na kuwazuia wasimpige Sauli. Sauli akasimama, akatoka pangoni, na kwenda zake.
8 Après cela David se leva, et sortit de la caverne, et cria après Saül, en disant: Mon Seigneur le Roi! et Saül regarda derrière lui, et David s'inclina le visage contre terre, et se prosterna.
Baadaye tena, Daudi akasimama juu, akatoka pangoni, na kumwita Sauli: “Bwana wangu mfalme.” Sauli alipotazama nyuma, Daudi akasujudu hadi chini na kuonyesha heshima.
9 Et David dit à Saül: Pourquoi écouterais-tu les paroles des gens qui disent: Voilà, David cherche ton mal?
Daudi akamwambia Sauli, “Kwa nini unawasikiliza watu ambao wanasema, “Angalia, Daudi anatafuta kukudhuru?'
10 Voici, aujourd'hui tes yeux ont vu que l'Eternel t'avait livré aujourd'hui en ma main dans la caverne, et on m'a dit que je te tuasse; mais je t'ai épargné, et j'ai dit: Je ne porterai point ma main sur mon Seigneur; car il est l'Oint de l'Eternel.
Leo macho yako yameona jinsi BWANA alivyokuweka mkononi mwangu tulipokuwa ndani ya pango. Wengine waliniambia nikuuwe, lakini nilikuacha hai. Nikasema, 'Sitanyoosha mkono wangu juu ya bwana wangu; kwa kuwa ni masihi wa BWANA.'
11 Regarde donc, mon père, regarde, dis-je, le pan de ton manteau qui est en ma main; car quand je coupais le pan de ton manteau, je ne t'ai point tué. Sache et connais qu'il n'y a point de mal ni d'injustice en ma main; et que je n'ai point péché contre toi; et cependant tu épies ma vie pour me l'ôter.
Tazama, baba yangu, angalia pindo la kanzu yako mkononi mwangu. Kwa maana kama nilikata pindo la kanzu yako na sikukuua, basi ujuwe na uone kwamba sina uovu au kosa katika mkono wangu, na sijafanya dhambi juu yako, ingawa unawinda kuutoa uhai wangu.
12 L'Eternel sera juge entre moi et toi, et l'Eternel me vengera de toi, mais ma main ne sera point sur toi.
BWANA aamue kati yangu na wewe, na BWANA anilipizie kisasi juu yako, lakini mkono wangu kamwe hautakuwa juu yako.
13 C'est des méchants que vient la méchanceté, comme dit le proverbe des anciens; c'est pourquoi ma main ne sera point sur toi.
Kama mithali ya wazee isemavyo, 'Katika waovu hutoka uovu.' Lakini mkono wangu hautakuwa juu yako.
14 Après qui est sorti un Roi d'Israël? qui poursuis-tu? un chien mort, une puce?
Mfalme wa Israeli ametoka kumuandama nani? Unamsaka nani? Unasaka mzoga wa mbwa! Unasaka kiroboto!
15 L'Eternel donc sera juge, et jugera entre moi et toi; et il regardera et plaidera ma cause, et me garantira de ta main.
BWANA na awe mwamuzi na atoe hukumu kati yangu na wewe, na akaione, na akatetee sababu yangu na aniruhusu kuepuka mkono wako.”
16 Or il arriva qu'aussitôt que David eut achevé de dire ces paroles à Saül, Saül dit: N'est-ce pas là ta voix, mon fils David? et Saül éleva sa voix, et pleura.
Daudi alipomaliza kuongea maneno haya kwa Sauli, Sauli akasema, “Hii ni sauti yako, mwanangu Daudi?” Sauli alinyanyua sauti yake akalia.
17 Et il dit à David: Tu es plus juste que moi; car tu m'as rendu le bien pour le mal que je t'ai fait,
Akamwambia Daudi, “Wewe ni mwenye haki kuliko mimi. Kwa sababu umenilipa mazuri, wakati mimi nimekulipa maovu.
18 Et tu m'as fait connaître aujourd'hui comment tu as usé de gratuité envers moi, car l'Eternel m'avait livré entre tes mains, et cependant tu ne m'as point tué.
Leo umetangaza jinsi ulivyonitendea mazuri, kwa sababu hukuniua wakati BWANA aliponiweka katika rehema yako.
19 Or qui est-ce qui ayant trouvé son ennemi, le laisserait aller sans lui faire du mal? que l'Eternel donc te rende du bien, pour ce que tu m'as fait aujourd'hui.
Kwa kuwa mtu akimpata adui yake, atamwacha aende zake salama? Na BWANA akuzawadie mema kwa kile ulichonifanyia leo.
20 Et maintenant voici, je connais que certainement tu régneras et que le Royaume d'Israël sera ferme entre tes mains.
Basi, najua kwa hakika kwamba utakuwa mfalme na kwamba ufalme wa Israeli utaimarika katika mkono wako.
21 C'est pourquoi maintenant jure-moi, par l'Eternel, que tu ne détruiras point ma race après moi, et que tu n'extermineras point mon nom de la maison de mon père.
Niapie kwa BWANA kwamba baada yangu hautawakatilia mbali uzao wangu, na kwamba hautaliharibu jina langu katika nyumba ya baba yangu.”
22 Et David le jura à Saül, et Saül s'en alla en sa maison; et David et ses gens montèrent dans le lieu fort.
Hivyo Daudi akamwapia Sauli kiapo. Kisha Sauli akaenda nyumbani, lakini Daudi na watu wake wakapanda kwenda ngomeni.