< 1 Samuel 17 >

1 Or les Philistins assemblèrent leurs armées pour faire la guerre, et ils s'assemblèrent à Soco, qui est de Juda, et se campèrent entre Soco et Hazéka, sur la frontière de Dammim.
Wakati huu Wafilisti wakakusanya majeshi yao kwa ajili ya vita, nao wakakusanyika huko Soko katika Yuda. Wakapiga kambi huko Efes-Damimu, kati ya Soko na Azeka.
2 Saül aussi et ceux d'Israël s'assemblèrent, et se campèrent en la vallée du chêne, et rangèrent leur bataille pour aller à la rencontre des Philistins.
Sauli na Waisraeli wakakusanyika na kupiga kambi katika Bonde la Ela na kupanga jeshi ili kupigana vita na Wafilisti.
3 Or les Philistins étaient sur une montagne du côté de deçà, et les Israëlites étaient sur une [autre] montagne du côté de delà; de sorte que la vallée était entre deux.
Wafilisti wakawa katika kilima kimoja na Waisraeli katika kilima kingine, hilo bonde likiwa kati yao.
4 Et il sortit du camp des Philistins un homme qui se présentait entre les deux armées, et qui avait nom Goliath, [de la ville] de Gath, haut de six coudées et d'une paume.
Shujaa aliyeitwa Goliathi, aliyetoka Gathi, akajitokeza kutoka kambi ya Wafilisti. Alikuwa na urefu dhiraa sita na shibiri moja.
5 Et il avait un casque d'airain sur sa tête, et était armé d'une cuirasse à écailles; et sa cuirasse pesait cinq mille sicles d'airain.
Alikuwa na chapeo ya shaba kichwani mwake, na alivaa dirii ya shaba kifuani mwake yenye uzito wa shekeli elfu tano.
6 Il avait aussi des jambières d'airain sur ses jambes, et un écu d'airain entre ses épaules.
Miguuni mwake alivaa mabamba ya shaba, na alikuwa na mkuki wa shaba mgongoni mwake.
7 La hampe de sa hallebarde était comme l'ensuble d'un tisserand, et le fer de cette [hallebarde] pesait six cents sicles de fer; et celui qui portait son bouclier marchait devant lui.
Mpini wa huo mkuki ulikuwa kama mti wa mfumaji, na ncha ya chuma yake ilikuwa na uzito wa shekeli mia sita. Mbeba ngao wake alitangulia mbele yake.
8 Il se présentait donc, et criait aux troupes rangées d'Israël, et leur disait: Pourquoi sortiriez-vous pour vous ranger en bataille? Ne suis-je pas Philistin, et vous n'êtes-vous pas serviteurs de Saül? Choisissez l'un d'entre vous, et qu'il descende vers moi.
Goliathi alisimama na kuwapigia kelele majeshi ya Israeli, akisema, “Kwa nini mmetoka kupanga vita? Je, mimi si Mfilisti, na ninyi ni watumishi wa Sauli? Chagueni mtu na anishukie mimi.
9 Que s'il est le plus fort en combattant avec moi, et qu'il me tue, nous serons vos serviteurs; mais si j'ai l'avantage sur lui, et que je le tue, vous serez nos serviteurs, et vous nous serez asservis.
Kama anaweza kupigana nami na kuniua, tutakuwa chini yenu; lakini kama nikimshinda na kumuua, ninyi mtakuwa chini yetu na mtatutumikia.”
10 Et le Philistin disait: J'ai déshonoré aujourd'hui les troupes rangées d'Israël, [en leur disant]: Donnez-moi un homme, et nous combattrons ensemble.
Kisha yule Mfilisti akasema, “Siku hii ya leo nayatukana majeshi ya Israeli! Nipeni mtu tupigane.”
11 [Mais] Saül et tous les Israëlites ayant entendu les paroles du Philistin, furent étonnés, et eurent une grande peur.
Kwa kusikia maneno ya Wafilisti, Sauli na Waisraeli wote wakafadhaika na kuogopa.
12 Or il y avait David, fils d'un homme Ephratien de Bethléhem de Juda, nommé Isaï, qui avait huit fils; il était vieux, et il était mis au rang des personnes de qualité du temps de Saül.
Basi Daudi alikuwa mwana wa Mwefrathi jina lake Yese aliyekuwa ametoka Bethlehemu ya Yuda. Yese alikuwa na wana wanane, naye wakati wa Sauli alikuwa mzee tena wa umri mkubwa.
13 Et les trois plus grands fils d'Isaï s'en étaient allés, et avaient suivi Saül en cette guerre. Les noms de ses trois fils qui s'en étaient allés à la guerre, étaient Eliab, le premier-né; Abinadab, le second; et Samma, le troisième.
Wana wakubwa watatu wa Yese walikuwa wamefuatana na Sauli vitani: Mzaliwa wa kwanza alikuwa Eliabu, wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama.
14 Et David était le plus jeune, et les trois plus grands suivaient Saül.
Daudi ndiye alikuwa mdogo wa wote. Hao wakubwa watatu wakamfuata Sauli,
15 Et David allait et revenait d'auprès de Saül, pour paître les brebis de son père en Bethléhem.
lakini Daudi alikuwa akienda kwa Sauli na kurudi ili kuchunga kondoo wa baba yake huko Bethlehemu.
16 Et le Philistin s'approchant le matin et le soir, se présenta quarante jours durant.
Kwa siku arobaini huyo Mfilisti alikuwa akija mbele kila siku asubuhi na jioni na kujionyesha.
17 Et Isaï dit à David son fils: Prends maintenant pour tes frères un Epha de ce froment rôti, et ces dix pains, et porte les en diligence au camp à tes frères.
Wakati huo Yese akamwambia mwanawe Daudi, “Chukua hii efa ya bisi na hii mikate kumi kwa ajili ya ndugu zako uwapelekee upesi kambini mwao.
18 Tu porteras aussi ces dix fromages de lait au capitaine de leur millier, et tu visiteras tes frères [pour savoir] s'ils se portent bien, et tu m'en apporteras des marques.
Chukua pamoja na hizi jibini kumi kwa jemadari wa kikosi chao. Ujue hali ya ndugu zako na uniletee taarifa za uhakika kutoka kwao.
19 Or Saül, et eux, et tous ceux d'Israël étaient en la vallée du chêne, combattant contre les Philistins.
Wao wako pamoja na Sauli na watu wote wa Israeli huko kwenye Bonde la Ela, wakipigana na Wafilisti.”
20 David donc se leva de bon matin, et laissa les brebis en garde au berger, puis ayant pris sa charge, s'en alla, comme son père Isaï le lui avait commandé, et il arriva au lieu où était le camp; et l'armée était sortie là où elle se rangeait en bataille, et on jetait de grands cris à cause de la bataille.
Asubuhi na mapema Daudi akaondoka, akaliacha kundi la kondoo pamoja na mchungaji, akapakia vitu vile na kuondoka, kama vile Yese alivyokuwa amemwagiza. Akafika kambini wakati jeshi lilikuwa likitoka kwenda kwenye sehemu yake ya kupigania, huku wakipiga kelele za vita.
21 Car les Israëlites et les Philistins avaient rangé armée contre armée.
Israeli na Wafilisti walikuwa wakipanga safu zao wakitazamana.
22 Alors David se déchargea de son bagage, le laissant entre les mains de celui qui gardait le bagage, et courut au lieu où était la bataille rangée, et y étant arrivé, il demanda à ses frères s'ils se portaient bien.
Daudi akaacha vile vitu vyake kwa mtunza vifaa, akakimbilia katika safu za vita na kuwasalimu ndugu zake.
23 Et comme il parlait avec eux, voici monter cet homme qui se présentait entre les deux armées, lequel avait nom Goliath, Philistin de la ville de Gath, [qui s'avançant hors] de l'armée des Philistins proféra les mêmes paroles qu'il avait proférées auparavant, et David les entendit.
Alipokuwa akisema nao, Goliathi, yule Mfilisti shujaa kutoka Gathi, akajitokeza mbele ya safu zake na kupiga ile kelele yake ya kawaida ya matukano, naye Daudi akayasikia.
24 Et tous ceux d'Israël voyant cet homme-là, s'enfuyaient de devant lui, et avaient une grande peur.
Waisraeli walipomwona yule mtu, wote wakamkimbia kwa woga mkuu.
25 Et chacun d'Israël disait: N'avez-vous point vu cet homme-là qui est monté? Il est monté pour déshonorer Israël; et s'il se trouve quelqu'un qui le frappe, le Roi le comblera de richesses, et lui donnera sa fille, et affranchira la maison de son père [de toutes charges] en Israël.
Basi Waisraeli walikuwa wakisema, “Je, mnaona jinsi mtu huyu anavyoendelea kujitokeza. Hujitokeza ili kutukana Israeli. Mfalme atatoa utajiri mwingi kwa yule mtu atakayemuua. Pia atamwoza binti yake na atasamehe jamaa ya baba yake kulipa kodi katika Israeli.”
26 Alors David parla aux gens qui étaient là avec lui, en disant: Quel bien fera-t-on à l'homme qui aura frappé ce Philistin, et qui aura ôté l'opprobre de dessus Israël? Car qui est ce Philistin, cet incirconcis, pour déshonorer ainsi les batailles rangées du Dieu vivant?
Daudi akauliza watu waliokuwa wamesimama karibu naye, “Je, atafanyiwa nini mtu atakayemuua huyu Mfilisti na kuondoa aibu hii katika Israeli? Ni nani huyu Mfilisti asiyetahiriwa hata atukane majeshi ya Mungu aliye hai?”
27 Et le peuple lui répéta ces mêmes paroles-là; et lui dit: C'est là le bien qu'on fera à l'homme qui l'aura frappé.
Wakarudia yale yaliyokuwa yamesemwa na kumwambia kuwa, “Hili ndilo atakalotendewa mtu yule atakayemuua.”
28 Et quand Eliab son frère aîné eut entendu qu'il parlait à ces gens-là, sa colère s'enflamma contre David, et il lui dit: Pourquoi es-tu descendu? et à qui as-tu laissé ce peu de brebis au désert? Je connais ton orgueil, et la malignité de ton cœur, car tu es descendu pour voir la bataille.
Eliabu nduguye mkubwa Daudi alipomsikia akizungumza na watu hasira ikawaka juu yake akamuuliza, “Kwa nini umeteremka kuja hapa? Nao wale kondoo wachache kule nyikani umewaacha na nani? Ninajua jinsi ulivyo na kiburi na jinsi moyo wako ulivyo mwovu; umekuja hapa kutazama vita tu.”
29 Et David répondit: Qu'ai-je fait maintenant? N'y a-t-il pas de quoi?
Daudi akasema, “Sasa nimefanya nini? Je, siwezi hata kuongea.”
30 Puis il se détourna de celui-là vers un autre, et lui dit les mêmes paroles; et le peuple lui répondit de la même manière comme la première fois.
Daudi akamgeukia mtu mwingine na kumuuliza jambo lilo hilo, nao watu wakamjibu vilevile kama mwanzo.
31 Et les paroles que David avait dites ayant été entendues, furent rapportées devant Saül; et il le fit venir.
Lile Daudi alilosema likasikiwa na kuelezwa kwa Sauli, naye Sauli akatuma aitwe.
32 Et David dit à Saül: Que le cœur ne défaille à personne à cause de celui-là; ton serviteur ira, et combattra contre ce Philistin.
Daudi akamwambia Sauli, “Mtu yeyote asife moyo kwa habari ya huyu Mfilisti; mtumishi wako atakwenda kupigana naye.”
33 Mais Saül dit à David: Tu ne saurais aller contre ce Philistin pour combattre contre lui; car tu n'es qu'un jeune garçon, et lui, il est homme de guerre dès sa jeunesse.
Sauli akamjibu Daudi, “Wewe hutaweza kwenda kupigana dhidi ya huyu Mfilisti; wewe ni kijana tu, naye amekuwa mtu wa vita tangu ujana wake.”
34 Et David répondit à Saül: Ton serviteur paissait les brebis de son père; et un lion vint, et un ours, et ils emportaient une brebis du troupeau:
Lakini Daudi akamwambia Sauli, “Mtumishi wako amekuwa akichunga kondoo wa baba yake. Wakati simba au dubu alikuja na kuchukua kondoo kutoka kundi,
35 Mais je sortis après eux, je les frappai, et j'arrachai [la brebis] de leur gueule; et comme ils se levaient contre moi, je les pris par la mâchoire, je les frappai, et je les tuai.
nilifuatia, nikampiga na nikampokonya kondoo kwenye kinywa chake. Aliponigeukia, nilimkamata nywele zake, nikampiga na kumuua.
36 Ton serviteur donc a tué et un lion, et un ours; et ce Philistin, cet incirconcis, sera comme l'un d'eux; car il a déshonoré les troupes rangées du Dieu vivant.
Mtumishi wako ameshaua simba na dubu pia; huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wa hao, kwa sababu ameyatukana majeshi ya Mungu aliye hai.
37 David dit encore: L'Eternel qui m'a délivré de la griffe du lion, et de la patte de l'ours, lui-même me délivrera de la main de ce Philistin. Alors Saül dit à David: Va, et l'Eternel soit avec toi.
Bwana ambaye aliniokoa toka katika makucha ya simba na makucha ya dubu ataniokoa kutoka mikono ya huyu Mfilisti.” Sauli akamwambia Daudi, “Nenda, naye Bwana na awe pamoja nawe.”
38 Et Saül fit armer David de ses armes, et lui mit son casque d'airain sur sa tête, et le fit armer d'une cuirasse.
Ndipo Sauli akamvika Daudi silaha zake mwenyewe za vita. Akamvika dirii na chapeo ya shaba kichwani mwake.
39 Puis David ceignit l'épée [de Saül] sur ses armes, et se mit à marcher; car [jamais] il ne l'avait essayé. Et David dit à Saül: Je ne saurais marcher avec ces armes; car je ne l'ai jamais essayé. Et David les ôta de dessus soi.
Daudi akajifunga upanga juu ya hayo mavazi na kujaribu kutembea kwa sababu alikuwa hana uzoefu navyo. Daudi akamwambia Sauli, “Siwezi kwenda nikiwa nimevaa hivi, kwa sababu sina uzoefu navyo.” Hivyo akavivua.
40 Mais il prit son bâton en sa main, et se choisit du torrent cinq cailloux bien unis, et les mit dans sa mallette de berger qu'il avait, et dans sa poche, et il avait sa fronde en sa main; et il s'approcha du Philistin.
Kisha akachukua fimbo yake mkononi, akachagua mawe laini matano kutoka kwenye kijito, akayaweka kwenye kifuko ndani ya mfuko wake wa kichungaji, akiwa na kombeo yake mkononi mwake, akamkaribia yule Mfilisti.
41 Le Philistin aussi s'en vint, et s'avança, et s'approcha de David, et l'homme qui portait son bouclier [marchait] devant lui.
Wakati ule ule, yule Mfilisti, akiwa na mbeba ngao wake mbele yake, akaendelea kujongea karibu na Daudi.
42 Et le Philistin regarda, et vit David, et le méprisa; car ce n'était qu'un jeune garçon, blond, et beau de visage.
Mfilisti akamwangalia Daudi kote na kumwona kuwa ni kijana tu, mwekundu na mzuri wa kupendeza, naye akamdharau.
43 Et le Philistin dit à David: [Suis-]je un chien, que tu viennes contre moi avec des bâtons? et le Philistin maudit David par ses dieux.
Akamwambia Daudi, “Je, mimi ni mbwa, hata unanijia na fimbo?” Yule Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.
44 Le Philistin dit encore à David: Viens vers moi, et je donnerai ta chair aux oiseaux du ciel, et aux bêtes des champs.
Tena Mfilisti akamwambia, “Njoo hapa, nami nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni nyama yako.”
45 Et David dit au Philistin: Tu viens contre moi avec l'épée, la hallebarde, et l'écu; mais moi, je viens contre toi au nom de l'Eternel des armées, du Dieu des batailles rangées d'Israël, lequel tu as déshonoré.
Daudi akamwambia yule Mfilisti. “Wewe unanijia na upanga, mkuki na fumo, lakini mimi ninakujia kwa jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa majeshi ya Israeli, ambaye wewe umemtukana.
46 Aujourd'hui l'Eternel te livrera entre mes mains, je te frapperai, je t'ôterai la tête de dessus toi, et je donnerai aujourd'hui les charognes du camp des Philistins aux oiseaux des cieux, et aux animaux de la terre; et toute la terre saura qu'Israël a un Dieu.
Siku hii leo Bwana atakutia mkononi mwangu, nami nitakupiga na kukukata kichwa chako. Leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya jeshi la Wafilisti, nayo dunia yote itajua kuwa yuko Mungu katika Israeli.
47 Et toute cette assemblée saura que l'Eternel ne délivre point par l'épée ni par la hallebarde; car cette bataille est à l'Eternel, qui vous livrera entre nos mains.
Wale wote waliokusanyika hapa watajua kuwa Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; kwa kuwa vita ni vya Bwana, naye atawatia wote mikononi mwetu.”
48 Et il arriva que comme le Philistin se fut levé, et qu'il s'approchait pour rencontrer David, David se hâta, et courut au lieu du combat pour rencontrer le Philistin.
Yule Mfilisti aliposogea karibu ili kumshambulia, Daudi akaenda mbio kuelekea safu ya vita kukutana naye.
49 Alors David mit la main à sa mallette, et en prit une pierre, la jeta avec sa fronde, et il en frappa le Philistin au front, tellement que la pierre s'enfonça dans son front; et il tomba le visage contre terre.
Daudi akatia mkono wake mfukoni na kuchukua jiwe, akalirusha kwa kombeo, nalo likampiga yule Mfilisti kwenye paji la uso. Lile jiwe likaingia kipajini mwa uso, akaanguka chini kifudifudi.
50 Ainsi David avec une fronde et une pierre fut plus fort que le Philistin, et frappa le Philistin, et le tua; or David n'avait point d'épée en sa main,
Basi Daudi akamshinda huyo Mfilisti kwa kombeo na jiwe; bila kuwa na upanga mikononi mwake akampiga huyo Mfilisti na kumuua.
51 Mais David courut, se jeta sur le Philistin, prit son épée, la tira de son fourreau, le tua, et lui coupa la tête. Et les Philistins ayant vu que leur homme fort était mort, s'enfuirent.
Daudi akakimbia na kusimama juu yake. Akaushika upanga wa huyo Mfilisti na kuuvuta toka kwenye ala yake. Baada ya kumuua, akakata kichwa chake kwa ule upanga. Wafilisti walipoona kuwa shujaa wao amekufa, wakageuka na kukimbia.
52 Alors ceux d'Israël et de Juda se levèrent, et jetèrent des cris de joie, et poursuivirent les Philistins, jusqu'à la vallée, et jusqu'aux portes de Hékron; et les Philistins blessés à mort tombèrent par le chemin de Saharajim, jusqu'à Gath, et jusqu'à Hékron.
Ndipo watu wa Israeli na Yuda wakainuka kwenda mbele wakipiga kelele na kufuatia Wafilisti mpaka kwenye ingilio la Gathi kwenye malango ya Ekroni. Maiti zao zilitawanyika kando ya barabara ya Shaaraimu hadi Gathi na Ekroni.
53 Et les enfants d'Israël s'en retournèrent de la poursuite des Philistins, et pillèrent leurs camps.
Waisraeli waliporudi kutoka kuwafukuza Wafilisti, waliteka nyara kutoka kambi yao.
54 Et David prit la tête du Philistin, laquelle il porta depuis à Jérusalem; il mit aussi dans sa tente les armes du [Philistin].
Daudi akachukua kichwa cha yule Mfilisti na kukileta Yerusalemu, naye akaweka silaha za huyo Mfilisti katika hema lake mwenyewe.
55 Or comme Saül vit David sortant pour rencontrer le Philistin, il dit à Abner Chef de l'armée: Abner, de qui est fils ce jeune garçon? Et Abner répondit: Comme ton âme vit, ô Roi! je n'en sais rien.
Sauli alipomwona Daudi anakwenda kukabiliana na huyo Mfilisti, alimwambia Abneri, jemadari wa jeshi, “Abneri, yule kijana ni mwana wa nani?” Abneri akajibu, “Hakika kama uishivyo, ee mfalme, mimi sifahamu.”
56 Le Roi lui dit: Enquiers-toi de qui est fils ce jeune garçon.
Mfalme akasema, “Uliza huyu kijana ni mwana wa nani.”
57 Sitôt donc que David fut revenu de tuer le Philistin, Abner le prit, et le mena devant Saül, ayant la tête du Philistin en sa main.
Mara Daudi aliporudi kutoka kumuua huyo Mfilisti, Abneri akamchukua na kumleta mbele ya Sauli. Daudi alikuwa bado anakishikilia kichwa cha yule Mfilisti.
58 Et Saül lui dit: Jeune garçon, de qui es-tu fils? David répondit: Je suis fils d'Isaï Bethléhémite, ton serviteur.
Sauli akamuuliza, “Kijana, wewe ni mwana wa nani?” Daudi akasema, “Mimi ni mwana wa mtumishi wako Yese wa Bethlehemu.”

< 1 Samuel 17 >