< 1 Rois 8 >

1 Alors Salomon assembla devant lui à Jérusalem les Anciens d'Israël, et tous les chefs des Tribus, les principaux des pères des enfants d'Israël, pour transporter l'Arche de l'alliance de l'Eternel de la Cité de David, qui est Sion.
Kisha Mfalme Solomoni akawaita mbele zake huko Yerusalemu wazee wa Israeli, viongozi wote wa makabila na wakuu wa jamaa za Waisraeli, ili walilete Sanduku la Agano la Bwana kutoka Sayuni, Mji wa Daudi.
2 Et tous ceux d'Israël furent assemblés vers le Roi Salomon, au mois d'Ethanim, qui est le septième mois, le jour même de la fête.
Wanaume wote wa Israeli wakakusanyika kwa Mfalme Solomoni wakati wa sikukuu ya mwezi wa Ethanimu, ndio mwezi wa saba.
3 Tous les Anciens d'Israël donc vinrent; et les Sacrificateurs portèrent l'Arche.
Wazee wote wa Israeli walipofika, makuhani wakajitwika Sanduku la Agano,
4 Ainsi on transporta l'Arche de l'Eternel, et le Tabernacle d'assignation, et tous les saints vaisseaux qui étaient au Tabernacle; les Sacrificateurs, dis-je, et les Lévites les emportèrent.
nao wakalipandisha Sanduku la Bwana, na Hema la Kukutania pamoja na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa ndani yake. Makuhani na Walawi wakavibeba,
5 Or le Roi Salomon, et toute l'assemblée d'Israël qui s'était rendue auprès de lui, étaient ensemble devant l'Arche [et] ils sacrifiaient du gros et du menu bétail en si grand nombre, qu'on ne le pouvait ni nombrer ni compter.
naye Mfalme Solomoni na kusanyiko lote la Israeli waliokusanyika kumzunguka walikuwa mbele ya hilo Sanduku, nao wakatoa dhabihu nyingi za kondoo na ngʼombe ambao idadi yao haikuwezekana kuandikwa au kuhesabiwa.
6 Et les Sacrificateurs portèrent l'Arche de l'Alliance de l'Eternel en son lieu, dans l'Oracle de la maison, au lieu Très-saint, sous les ailes des Chérubins.
Makuhani wakalileta Sanduku la Agano la Bwana hadi mahali pake ndani ya sehemu takatifu ndani ya Hekalu, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na kuliweka chini ya mabawa ya makerubi.
7 Car les Chérubins étendaient les ailes sur l'endroit où devait être l'Arche, et les Chérubins couvraient l'Arche et ses barres, par dessus.
Makerubi yalitandaza mabawa yao juu ya mahali pa Sanduku la Agano na kutia kivuli Sanduku pamoja na mipiko yake ya kubebea.
8 Et ils retirèrent les barres en dedans, de sorte que les bouts des barres se voyaient du lieu Saint sur le devant de l'Oracle, mais ils ne se voyaient point au dehors; et elles sont demeurées là jusqu'à ce jour.
Mipiko hiyo ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba ncha zake zilionekana kutoka Mahali Patakatifu mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, lakini sio nje ya Mahali Patakatifu. Hiyo mipiko ipo hata leo.
9 Il n'y avait rien dans l'Arche que les deux tables de pierre que Moïse y avait mises en Horeb, quand l'Eternel traita [alliance] avec les enfants d'Israël, lorsqu'ils furent sortis du pays d'Egypte.
Ndani ya Sanduku hapakuwepo kitu kingine chochote isipokuwa zile mbao mbili za mawe ambazo Mose alikuwa ameziweka ndani yake huko Horebu, mahali ambapo Bwana alifanya Agano na Waisraeli baada ya kutoka Misri.
10 Or il arriva que comme les Sacrificateurs furent sortis du lieu Saint, une nuée remplit la maison de l'Eternel.
Makuhani walipoondoka katika Mahali Patakatifu, wingu likajaza Hekalu la Bwana.
11 De sorte que les Sacrificateurs ne se pouvaient tenir debout pour faire le service, à cause de la nuée; car la gloire de l'Eternel avait rempli la maison de l'Eternel.
Nao makuhani hawakuweza kufanya huduma yao kwa sababu ya lile wingu, kwa kuwa utukufu wa Bwana ulijaza Hekalu lake.
12 Alors Salomon dit: L'Eternel a dit qu'il habiterait dans l'obscurité.
Ndipo Solomoni akasema, “Bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene;
13 J'ai achevé, [ô Eternel!] de bâtir une maison pour ta demeure, un domicile fixe, afin que tu y habites éternellement.
naam, hakika nimekujengea Hekalu zuri sana, mahali pako pa kuishi milele.”
14 Et le Roi tournant son visage, bénit toute l'assemblée d'Israël; car toute l'assemblée d'Israël se tenait [là] debout.
Kusanyiko lote la Israeli lilipokuwa limesimama hapo, mfalme akageuka na kuwabariki.
15 Et il dit: Béni soit l'Eternel, le Dieu d'Israël, qui a parlé de sa propre bouche à David mon père, et qui l'a accompli par sa puissance, et a dit:
Kisha akasema: “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye kwa mkono wake mwenyewe ametimiza lile alilomwahidi Daudi baba yangu kwa kinywa chake mwenyewe. Kwa kuwa alisema,
16 Depuis le jour que je retirai mon peuple d'Israël hors d'Egypte, je n'ai choisi aucune ville d'entre toutes les Tribus d'Israël pour y bâtir une maison, afin que mon Nom y fût; mais j'ai choisi David, afin qu'il eût la charge de mon peuple d'Israël.
‘Tangu siku niliyowatoa watu wangu Israeli kutoka Misri, sikuchagua mji katika kabila lolote la Israeli ili Hekalu lijengwe humo ili Jina langu lipate kuwamo humo, bali nimemchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.’
17 Et David mon père avait au cœur de bâtir une maison au Nom de l'Eternel, le Dieu d'Israël.
“Ilikuwa moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
18 Mais l'Eternel dit à David mon père: Quant à ce que tu as eu au cœur de bâtir une maison à mon Nom, tu as bien fait d'avoir eu cela au cœur.
Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu ilikuwa moyoni mwako kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu, ulifanya vyema kuwa na jambo hili moyoni mwako.
19 Néanmoins tu ne bâtiras point cette maison, mais ton fils qui sortira de tes reins, sera celui qui bâtira cette maison à mon Nom.
Hata hivyo, sio wewe utakayenijengea hekalu, bali mwanao, ambaye ni nyama yako na damu yako mwenyewe, yeye ndiye atakayejenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
20 L'Eternel a donc accompli sa parole, qu'il avait prononcée, et j'ai succédé à David mon père, et je suis assis sur le trône d'Israël, comme l'Eternel en avait parlé; et j'ai bâti cette maison au Nom de l'Eternel le Dieu d'Israël.
“Bwana ametimiza ahadi aliyoiweka: Nimeingia mahali pa Daudi baba yangu na sasa ninakikalia kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Bwana alivyoahidi, nami nimejenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
21 Et j'ai assigné ici un lieu à l'Arche, dans laquelle est l'alliance de l'Eternel, qu'il traita avec nos pères, quand il les eut tirés hors du pays d'Egypte.
Nimetenga nafasi humo kwa ajili ya Sanduku la Agano, ambamo ndani yake kuna lile Agano la Bwana alilofanya na baba zetu wakati alipowatoa Misri.”
22 Ensuite Salomon se tint devant l'autel de l'Eternel en la présence de toute l'assemblée d'Israël, et ayant ses mains étendues vers les cieux,
Kisha Solomoni akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana machoni pa kusanyiko lote la Israeli, akakunjua mikono yake kuelekea mbinguni
23 Il dit: Ô Eternel Dieu d'Israël! il n'y a point de Dieu semblable à toi dans les cieux en haut, ni sur la terre en bas; tu gardes l'alliance et la gratuité envers tes serviteurs, qui marchent de tout leur cœur devant ta face.
na kusema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni wala chini duniani, wewe unayetunza Agano lako la upendo na watumishi wanaodumu katika njia yako kwa moyo wote.
24 [Et] tu as tenu à ton serviteur David mon père ce dont tu lui avais parlé; car ce dont tu lui avais parlé de ta bouche, tu l'as accompli de ta main, comme [il paraît] aujourd'hui.
Umetimiza ahadi yako kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, kwa kinywa chako uliahidi na kwa mkono wako umetimiza, kama ilivyo leo.
25 Maintenant donc, ô Eternel Dieu d'Israël! tiens à ton serviteur David mon père, ce dont tu lui as parlé, en disant: Jamais il ne te sera retranché de devant ma face un [successeur] pour être assis sur le trône d'Israël, pourvu seulement que tes fils prennent garde à leur voie, afin de marcher devant ma face, comme tu y as marché.
“Sasa Bwana, Mungu wa Israeli, mtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu ahadi zako ulizomwahidi uliposema, ‘Kamwe hutakosa kuwa na mtu atakayeketi mbele zangu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama wanao wakiangalia yote wayafanyayo kuenenda mbele zangu kama vile ulivyofanya.’
26 Et maintenant, ô Dieu d'Israël! je te prie, que ta parole, laquelle tu as prononcée à ton serviteur David mon père, soit ratifiée.
Sasa, Ee Mungu wa Israeli, acha neno lako lile ulilomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu litimie.
27 Mais Dieu habiterait-il effectivement sur la terre? Voilà, les cieux, même les cieux des cieux ne te peuvent contenir; combien moins cette maison que j'ai bâtie.
“Lakini kweli, je, Mungu atafanya makao duniani? Mbingu, hata mbingu zilizo juu sana, haziwezi kukutosha wewe. Sembuse Hekalu hili nililojenga!
28 Toutefois, ô Eternel mon Dieu! aie égard à la prière de ton serviteur, et à sa supplication, pour entendre le cri et la prière que ton serviteur te fait aujourd'hui;
Hata hivyo sikiliza dua ya mtumishi wako na maombi yake kwa huruma, Ee Bwana Mungu wangu. Sikia kilio na dua ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako siku hii ya leo.
29 [Qui est], que tes yeux soient ouverts jour et nuit sur cette maison, le lieu dont tu as dit: Mon nom sera là, pour exaucer la prière que ton serviteur fait en ce lieu-ci.
Macho yako na yafumbuke kuelekea Hekalu hili usiku na mchana, mahali hapa ambapo ulisema, ‘Jina langu litakuwako humo,’ ili kwamba upate kusikia maombi ambayo mtumishi wako ataomba kuelekea mahali hapa.
30 Exauce donc la supplication de ton serviteur, et de ton peuple d'Israël quand ils te prieront en ce lieu-ci; exauce[-les], [dis-je], du lieu de ta demeure, des cieux; exauce, et pardonne.
Usikie maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli wakati wanapoomba kuelekea mahali hapa. Sikia kutoka mbinguni, mahali pa makao yako na usikiapo, samehe.
31 Quand quelqu'un aura péché contre son prochain, et qu'on lui aura déféré le serment pour le faire jurer, et que le serment aura été fait devant ton autel dans cette maison;
“Mtu anapomkosea jirani yake na akatakiwa kuapa, akija na kuapa mbele ya madhabahu yako ndani ya Hekalu hili,
32 Exauce[-les] toi des cieux, et exécute [ce que portera l'exécration du serment], et juge tes serviteurs en condamnant le méchant, [et] lui rendant selon ce qu'il aura fait; et en justifiant le juste, et lui rendant selon sa justice.
basi, sikia kutoka mbinguni na ukatende. Hukumu kati ya watumishi wako, ukimhukumu yule mwenye hatia na kuleta juu ya kichwa chake yale aliyoyatenda. Umtangazie mwenye haki kwamba hana hatia, hivyo ukathibitishe kuwa haki kwake.
33 Quand ton peuple d'Israël aura été battu par l'ennemi, à cause qu'ils auront péché contre toi, si ensuite ils se retournent vers toi, en réclamant ton nom, et en te faisant des prières et des supplications dans cette maison;
“Wakati watu wako Israeli watakapokuwa wameshindwa na adui kwa sababu ya dhambi walizofanya dhidi yako, watakapokugeukia na kulikiri jina lako, wakiomba na kufanya dua kwako katika Hekalu hili,
34 Exauce[-les], toi, des cieux, et pardonne le péché de ton peuple d'Israël, et ramène-les dans la terre que tu as donnée à leurs pères.
basi usikie kutoka mbinguni, ukasamehe dhambi ya watu wako Israeli na kuwarudisha katika nchi uliyowapa baba zao.
35 Quand les cieux seront resserrés, et qu'il n'y aura point de pluie, à cause que [ceux d'Israël] auront péché contre toi, s'ils te font prière en ce lieu-ci, et s'ils réclament ton Nom, et s'ils se détournent de leurs péchés, parce que tu les auras affligés;
“Wakati mbingu zitakapokuwa zimefungwa kusiwe na mvua kwa sababu watu wako wametenda dhambi dhidi yako, watakapoomba kuelekea mahali hapa na kulikiri jina lako nao wakageuka kutoka dhambi zao kwa sababu umewaadhibu,
36 Exauce[-les], toi, des cieux, et pardonne le péché de tes serviteurs, et de ton peuple d'Israël, lorsque tu leur auras enseigné le bon chemin, par lequel ils doivent marcher, et envoie-leur la pluie sur la terre que tu as donnée à ton peuple pour héritage.
basi usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi ya watumishi wako, watu wako Israeli. Wafundishe njia sahihi ya kuishi na ukanyeshe mvua juu ya nchi uliyowapa watu wako kuwa urithi.
37 Quand il y aura famine au pays, ou la mortalité; quand il y aura brûlure, nielle, sauterelles, et vermisseaux, même quand les ennemis les assiégeront jusques dans leur propre pays, [ou qu'il y aura plaie, ou] maladie;
“Wakati njaa au tauni vikija juu ya nchi, au koga au kawa, nzige au panzi, au wakati adui atakapowazingira katika mji wao wowote, maafa ya namna yoyote au ugonjwa wowote unaoweza kuwajia,
38 Quelque prière, et quelque supplication que te fasse quelque homme que ce soit de tout ton peuple d'Israël, selon qu'ils auront connu chacun la plaie de son cœur; et que chacun aura étendu ses mains vers cette maison;
wakati dua au maombi yatakapofanywa na mmojawapo wa watu wako Israeli, kila mmoja akitambua taabu za moyo wake mwenyewe, naye akainyoosha mikono yake kuelekea Hekalu hili:
39 Alors exauce[-les], toi, des cieux, du domicile arrêté de ta demeure, et pardonne, et fais, et rends à chacun selon toutes ses voies, parce que tu auras connu son cœur; car tu connais toi-seul le cœur de tous les hommes;
basi usikie kutoka mbinguni, katika makao yako. Usamehe na utende, umpe kila mtu kulingana na matendo yake, kwa kuwa unaujua moyo wake (kwa kuwa ni wewe peke yako ujuaye mioyo ya watu wote),
40 Afin qu'ils te craignent tout le temps qu'ils vivront sur la terre que tu as donnée à nos pères.
ili wakuogope kwa wakati wote watakaoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
41 Et même lorsque l'étranger qui ne sera pas de ton peuple d'Israël, mais qui sera venu d'un pays éloigné pour l'amour de ton Nom;
“Kwa habari ya mgeni ambaye si miongoni mwa watu wako Israeli, lakini amekuja kutoka nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako,
42 (Car on entendra parler de ton Nom, qui est grand, et de ta main forte, et de ton bras étendu; ) lors donc qu'il sera venu, et qu'il te priera dans cette maison;
kwa maana watu watasikia juu ya Jina lako kuu na juu ya mkono wako wenye nguvu na mkono wako ulionyooshwa, atakapokuja na kuomba kuelekea Hekalu hili,
43 Exauce[-le], toi, des cieux, du domicile arrêté de ta demeure, et fais selon tout ce pour quoi cet étranger aura crié vers toi; afin que tous les peuples de la terre connaissent ton Nom pour te craindre, comme ton peuple d'Israël; et pour connaître que ton Nom est réclamé sur cette maison que j'ai bâtie.
basi na usikie kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, ukafanye lolote ambalo mgeni huyo anakuomba, ili mataifa yote ya dunia wapate kujua jina lako na wakuogope kama wafanyavyo watu wako Israeli nao wapate pia kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa Jina lako.
44 Quand ton peuple sera sorti en guerre contre son ennemi, dans le chemin par lequel tu l'auras envoyé, s'ils font prière à l'Eternel en regardant vers cette ville que tu as choisie, et vers cette maison que j'ai bâtie à ton Nom;
“Wakati watu wako watakapokwenda vitani dhidi ya adui zao, popote utakapowapeleka, wakati watakapoomba kwa Bwana kuelekea mji ambao umeuchagua, na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
45 Alors exauce des cieux leur prière et leur supplication, et maintiens leur droit.
basi usikie dua na maombi yao kutoka mbinguni, ukawatetee haki yao.
46 Quand ils auront péché contre toi, car il n'y a point d'homme qui ne pèche, et que tu seras irrité contr'eux, tellement que tu les auras livrés entre les [mains] de leurs ennemis, et que ceux qui les auront pris les auront menés captifs en pays ennemi, soit loin, soit près;
“Watakapotenda dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna mtu yeyote ambaye hatendi dhambi, nawe ukachukizwa nao na kuwakabidhi kwa adui, ambaye atawachukua utumwani katika nchi yake mwenyewe, mbali au karibu;
47 Si au pays où ils auront été menés captifs, ils reviennent à eux-mêmes, et se repentant ils te prient au pays de ceux qui les auront emmenés captifs, en disant: Nous avons péché, nous avons fait iniquité, et nous avons fait méchamment;
na kama watabadilika mioyo yao katika nchi wanakoshikiliwa mateka, nao wakatubu na kukulilia katika nchi ya wale waliowashinda na kusema, ‘Tumetenda dhambi, tumefanya makosa, tumetenda uovu’;
48 S'ils retournent donc à toi de tout leur cœur et de toute leur âme, dans le pays de leurs ennemis, qui les auront emmenés captifs, et s'ils t'adressent leurs prières, en regardant vers leur pays que tu as donné à leurs pères, vers cette ville que tu as choisie, et vers cette maison que j'ai bâtie à ton Nom;
kama wakikugeukia kwa moyo wao wote na nafsi zao katika nchi ya adui zao ambao waliwachukua mateka, wakakuomba kuelekea nchi uliyowapa baba zao, kuelekea mji uliouchagua na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako;
49 Alors exauce des cieux, du domicile arrêté de ta demeure, leur prière, et leur supplication, et maintiens leur droit.
basi kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, usikie dua yao na maombi yao na kuitetea haki yao.
50 Et pardonne à ton peuple qui aura péché contre toi, et même [pardonne-leur] tous les crimes qu'ils auront commis contre toi, et fais que ceux qui les auront emmenés captifs aient pitié d'eux, et leur fassent grâce.
Uwasamehe watu wako, waliotenda dhambi dhidi yako; uwasamehe makosa yote waliyoyatenda dhidi yako, ukawafanye wale waliowashinda kuwaonea huruma;
51 Car ils sont ton peuple et ton héritage, que tu as tiré hors d'Egypte, du milieu d'un fourneau de fer.
kwa maana ni watu wako na urithi wako, uliowatoa Misri, kutoka kwenye lile tanuru la kuyeyushia chuma.
52 Que tes yeux donc soient ouverts sur la prière de ton serviteur, et sur la supplication de ton peuple d'Israël, pour les exaucer dans tout ce pourquoi ils crieront à toi.
“Macho yako na yafumbuke juu ya ombi la mtumishi wako na ombi la watu wako Israeli, nawe uwasikilize wakati wowote wanapokulilia.
53 Car tu les as mis à part pour toi d'entre tous les peuples de la terre, afin qu'ils fussent ton héritage, comme tu en as parlé par le moyen de Moïse ton serviteur, quand tu retiras nos pères hors d'Egypte, ô Seigneur Eternel!
Kwa maana uliwachagua wao kutoka mataifa yote ya ulimwengu kuwa urithi wako mwenyewe, kama ulivyotangaza kupitia mtumishi wako Mose wakati wewe, Ee Bwana Mwenyezi, ulipowatoa baba zetu kutoka Misri.”
54 Or aussitôt que Salomon eut achevé de faire toute cette prière, et cette supplication à l'Eternel, il se leva de devant l'autel de l'Eternel, et n'étant plus à genoux, mais ayant [encore] les mains étendues vers les cieux;
Wakati Solomoni alipomaliza dua hizi zote na maombi kwa Bwana, akainuka kutoka mbele ya madhabahu ya Bwana, mahali alipokuwa amepiga magoti, mikono yake ikawa imekunjuliwa kuelekea juu mbinguni.
55 Il se tint debout, et bénit toute l'assemblée d'Israël à haute voix, en disant:
Akasimama na kubariki kusanyiko lote la Israeli kwa sauti kubwa akisema:
56 Béni soit l'Eternel, qui a donné du repos à son peuple d'Israël, comme il en avait parlé; il n'est pas tombé [à terre] un seul mot de toutes les bonnes paroles qu'il avait prononcées par le moyen de Moïse son serviteur.
“Ahimidiwe Bwana, aliyewapa pumziko watu wake Israeli kama vile alivyokuwa ameahidi. Hakuna hata neno moja lililopunguka kati ya ahadi zote nzuri alizozitoa kupitia mtumishi wake Mose.
57 Que l'Eternel notre Dieu soit avec nous, comme il a été avec nos pères; qu'il ne nous abandonne point, et qu'il ne nous délaisse point.
Bwana Mungu wetu na awe pamoja nasi kama alivyokuwa na baba zetu, kamwe asituache wala kutukataa.
58 [Mais] qu'il incline notre cœur vers lui, afin que nous marchions en toutes ses voies, et que nous gardions ses commandements, ses statuts, et ses ordonnances qu'il a prescrites à nos pères;
Yeye na aielekeze mioyo yetu kwake, ili tutembee katika njia zake zote na kuzishika amri na maagizo na masharti aliyowapa baba zetu.
59 Et que mes paroles, par lesquelles j'ai fait supplication à l'Eternel, soient présentes devant l'Eternel notre Dieu jour et nuit; afin qu'il maintienne le droit de son serviteur, et le droit de son peuple d'Israël, selon qu'il en aura besoin chaque jour.
Nami maneno yangu haya, ambayo nimeyaomba mbele za Bwana, yawe karibu na Bwana Mungu wetu usiku na mchana, ili kwamba atetee shauri la mtumishi wake na la watu wake Israeli kulingana na hitaji lao la kila siku,
60 Afin que tous les peuples de la terre connaissent que c'est l'Eternel qui est Dieu, [et] qu'il n'y en a point d'autre;
ili kwamba mataifa yote ya dunia wajue kwamba Bwana ndiye Mungu na kwamba hakuna mwingine.
61 Et afin que votre cœur soit pur envers l'Eternel votre Dieu, pour marcher dans ses statuts, et pour garder ses commandements, comme aujourd'hui.
Lakini ni lazima mwiweke mioyo yenu kikamilifu kwa Bwana Mungu wetu, kuishi kwa maagizo yake na kutii amri zake, kama ilivyo wakati huu.”
62 Et le Roi, et tout Israël avec lui, sacrifièrent des sacrifices devant l'Eternel.
Kisha mfalme na Israeli wote pamoja naye wakatoa dhabihu mbele za Bwana.
63 Et Salomon offrit un sacrifice de prospérités, qu'il sacrifia à l'Eternel, [savoir], vingt et deux mille bœufs, et six vingt mille brebis. Ainsi le Roi et tous les enfants d'Israël dédièrent la maison de l'Eternel.
Solomoni akatoa dhabihu sadaka za amani kwa Bwana: ngʼombe 22,000, pamoja na kondoo na mbuzi 120,000. Hivyo ndivyo mfalme na Waisraeli wote walivyoweka wakfu Hekalu la Bwana.
64 En ce jour-là le Roi consacra le milieu du parvis, qui était devant la maison de l'Eternel; car il offrit là les holocaustes, et les gâteaux, et les graisses des sacrifices de prospérités, parce que l'autel d'airain qui était devant l'Eternel, était trop petit pour contenir les holocaustes, et les gâteaux, et les graisses des sacrifices de prospérités.
Siku iyo hiyo mfalme akaweka wakfu sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya Hekalu la Bwana na hapo akatoa sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele za Bwana ilikuwa ndogo sana kuweza kubeba sadaka hizo za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta ya sadaka ya amani.
65 Et en ce temps-là Salomon célébra une fête solennelle; et avec lui tout Israël qui était une grande assemblée, [venue] depuis où l'on entre en Hamath jusqu'au torrent d'Egypte, devant l'Eternel notre Dieu, et cela dura sept jours, et sept autres jours, ce qui fut quatorze jours.
Hivyo Solomoni akaiadhimisha sikukuu kwa wakati ule, na Israeli wote pamoja naye. Walikuwa kusanyiko kubwa sana, watu kutoka Lebo-Hamathi hadi Kijito cha Misri. Wakaiadhimisha mbele za Bwana Mungu wetu kwa siku saba na siku saba zaidi, yaani, jumla siku kumi na nne.
66 [Et] au huitième jour il renvoya le peuple, qui bénit le Roi; puis ils s'en allèrent dans leurs tentes, en se réjouissant, et ayant le cœur plein de joie à cause de tout le bien que l'Eternel avait fait à David son serviteur, et à Israël son peuple.
Siku iliyofuata, aliwaruhusu watu waondoke. Wakambariki mfalme, kisha wakaenda nyumbani, wakiwa na mashangilio na furaha rohoni kwa ajili ya mambo yote mema ambayo Bwana ametenda kwa ajili ya Daudi mtumishi wake na watu wake Israeli.

< 1 Rois 8 >