< 1 Rois 13 >

1 Et voici, un homme de Dieu vint de Juda à Bethel avec la parole de l'Eternel, lorsque Jéroboam se tenait près de l'autel pour y faire des encensements.
Kwa neno la Bwana, mtu wa Mungu alifika Betheli kutoka Yuda wakati Yeroboamu alipokuwa amesimama kando ya madhabahu ili kutoa sadaka.
2 Et il cria contre l'autel selon la parole de l'Eternel; et dit: Autel! Autel! ainsi a dit l'Eternel, voici, un fils naîtra à la maison de David, qui aura nom Josias; il immolera sur toi les Sacrificateurs des hauts lieux qui font des encensements sur toi, et on brûlera sur toi les os des hommes.
Akapiga kelele dhidi ya madhabahu kwa neno la Bwana: “Ee madhabahu, madhabahu! Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Mwana aitwaye Yosia atazaliwa katika nyumba ya Daudi. Juu yako atawatoa dhabihu makuhani wa mahali pa juu pa kuabudia miungu wale ambao wanatoa sadaka hapa sasa, nayo mifupa ya wanadamu itachomwa juu yako.’”
3 Et il proposa ce jour-là même un miracle, en disant: C'est ici le miracle dont l'Eternel a parlé: Voici, l'autel se fendra tout maintenant, et la cendre qui est dessus sera répandue.
Siku iyo hiyo, mtu wa Mungu akatoa ishara: “Hii ndiyo ishara Bwana aliyotangaza: Madhabahu haya yatapasuka na majivu yaliyo juu yake yatamwagika.”
4 Or il arriva qu'aussitôt que le Roi eut entendu la parole que l'homme de Dieu avait prononcée à haute voix contre l'autel de Bethel, Jéroboam étendit sa main de l'autel, en disant: Saisissez-le. Et la main qu'il étendit contre lui devint sèche, et il ne la put retirer à soi.
Mfalme Yeroboamu aliposikia kile mtu wa Mungu alichosema, alipopiga kelele dhidi ya madhabahu huko Betheli, akanyoosha mkono wake kutoka madhabahuni na kusema, “Mkamate!” Lakini mkono aliokuwa ameunyoosha kumwelekea yule mtu ukasinyaa na kubaki hapo hapo, kiasi kwamba hakuweza kuurudisha.
5 L'autel aussi se fendit, et la cendre qui était sur l'autel fut répandue, selon le miracle que l'homme de Dieu avait proposé suivant la parole de l'Eternel.
Pia, madhabahu yalipasuka na majivu yakamwagika sawasawa na ishara iliyotolewa na mtu wa Mungu kwa neno la Bwana.
6 Et le Roi prit la parole, et dit à l'homme de Dieu: Je te prie qu'il te plaise de supplier l'Eternel ton Dieu, et de faire prière pour moi, afin que ma main retourne à moi. Et l'homme de Dieu supplia l'Eternel, et la main du Roi retourna à lui, et elle fut comme auparavant.
Kisha mfalme akamwambia mtu wa Mungu, “Niombee kwa Bwana Mungu wako ili mkono wangu upate kupona.” Kwa hiyo mtu wa Mungu akamwombea kwa Bwana, nao mkono wa mfalme ukapona na kuwa kama ulivyokuwa hapo kwanza.
7 Alors le Roi dit à l'homme de Dieu: Entre avec moi dans la maison, et y dîne, et je te ferai un présent.
Mfalme akamwambia yule mtu wa Mungu, “Twende nyumbani kwangu upate chakula, nami nitakupa zawadi.”
8 Mais l'homme de Dieu répondit au Roi: Quand tu me donnerais la moitié de ta maison, je n'entrerais point chez toi, et je ne mangerais point de pain, ni ne boirais d'eau en ce lieu-ci.
Lakini yule mtu wa Mungu akamjibu mfalme, “Hata kama ungenipa nusu ya mali zako, nisingekwenda pamoja na wewe, wala nisingekula mkate au kunywa maji hapa.
9 Car il m'a été ainsi commandé par l'Eternel, qui m'a dit: Tu n'y mangeras point de pain, et tu n'y boiras point d'eau, et tu ne t'en retourneras point par le chemin par lequel tu y seras allé.
Kwa kuwa niliagizwa kwa neno la Bwana: ‘Kamwe usile mkate wala usinywe maji au kurudi kwa njia uliyojia.’”
10 Il s'en alla donc par un autre chemin, et ne s'en retourna point par le chemin par lequel il était venu à Bethel.
Kwa hiyo akafuata njia nyingine na hakurudi kupitia njia ile ambayo alikuwa ameijia Betheli.
11 Or il y avait un certain Prophète, vieux homme, qui demeurait à Bethel, à qui son fils vint raconter toutes les choses que l'homme de Dieu avait faites ce jour-là à Bethel, et les paroles qu'il avait dites au Roi; [et les enfants de ce prophète] les rapportèrent à leur père.
Basi kulikuwepo na nabii fulani mzee aliyekuwa anaishi Betheli, ambaye wanawe walikuja kumwambia yote ambayo mtu wa Mungu alikuwa ameyafanya pale siku ile. Pia wakamwambia baba yao yale aliyomwambia mfalme.
12 Et leur père leur dit: Par quel chemin s'en est-il allé? Or ses enfants avaient vu le chemin par lequel l'homme de Dieu qui était venu de Juda s'en était allé.
Baba yao akawauliza, “Ameelekea njia gani?” Nao wanawe wakamwonyesha ile njia yule mtu wa Mungu kutoka Yuda aliyopita.
13 Et il dit à ses fils: Sellez-moi un âne; et ils le sellèrent, puis il monta dessus.
Hivyo akawaambia wanawe, “Nitandikieni punda.” Walipokwisha kumtandikia punda, akampanda
14 Et il s'en alla après l'homme de Dieu, et le trouva assis sous un chêne; et il lui dit: Es-tu l'homme de Dieu qui es venu de Juda? Et il lui répondit: C'est moi.
na kumfuatilia yule mtu wa Mungu. Akamkuta ameketi chini ya mwaloni na akamuuliza, “Je, wewe ndiwe mtu wa Mungu kutoka Yuda?” Akamjibu, “Mimi ndiye.”
15 Alors il lui dit: Viens avec moi dans la maison, et y mange du pain.
Basi nabii akamwambia, “Karibu nyumbani pamoja na mimi ule.”
16 Mais il répondit: Je ne puis retourner avec toi, ni entrer chez toi, et je ne mangerai point de pain, ni je ne boirai point d'eau avec toi en ce lieu-là.
Yule mtu wa Mungu akasema, “Siwezi kurudi na kwenda nawe, wala siwezi kula mkate au kunywa maji pamoja nawe mahali hapa.
17 Car il m'a été dit de la part de l'Eternel: Tu n'y mangeras point de pain, et tu n'y boiras point d'eau, et tu ne t'en retourneras point par le chemin par lequel tu y seras allé.
Nimeambiwa kwa neno la Bwana: ‘Kamwe usile mkate au kunywa maji huko au kurudia njia uliyojia.’”
18 Et il lui dit: Et moi aussi je suis prophète comme toi; et un Ange m'a parlé de la part de l'Eternel, en disant: Ramène-le avec toi dans ta maison, et qu'il mange du pain, et qu'il boive de l'eau; mais il lui mentait.
Yule nabii mzee akajibu, “Mimi pia ni nabii, kama wewe. Naye malaika alisema nami kwa neno la Bwana: ‘Mrudishe aje katika nyumba yako ili apate kula mkate na kunywa maji.’” (Lakini alikuwa akimwambia uongo.)
19 Il s'en retourna donc avec lui, et il mangea du pain, et but de l'eau dans sa maison.
Hivyo mtu wa Mungu akarudi pamoja naye na akala na kunywa katika nyumba yake.
20 Et il arriva que comme ils étaient assis à table, la parole de l'Eternel fut adressée au prophète qui l'avait ramené.
Wakati walipokuwa wameketi mezani, neno la Bwana likamjia yule nabii mzee aliyemrudisha huyo mtu wa Mungu.
21 Et il cria à l'homme de Dieu qui était venu de Juda, en disant: Ainsi a dit l'Eternel; parce que tu as été rebelle au commandement de l'Eternel, et que tu n'as point gardé le commandement que l'Eternel ton Dieu t'avait prescrit;
Akampazia sauti yule mtu wa Mungu aliyekuwa ametoka Yuda, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Umeasi neno la Bwana na hukushika amri uliyopewa na Bwana Mungu wako,
22 Mais tu t'en es retourné, et tu as mangé du pain, et bu de l'eau dans le lieu dont [l'Eternel] t'avait dit; n'y mange point de pain, et n'y bois point d'eau, ton corps n'entrera point au sépulcre de tes pères.
bali ulirudi na ukala mkate na kunywa maji mahali ambapo alikuambia usile wala usinywe. Kwa hiyo maiti yako haitazikwa katika kaburi la baba zako.’”
23 Or après qu'il eut mangé du pain, et qu'il eut bu, [le vieux Prophète] fit seller un âne, pour le Prophète qu'il avait ramené.
Wakati huyo mtu wa Mungu alipomaliza kula na kunywa, nabii aliyekuwa amemrudisha akamtandikia punda wake.
24 Puis [ce Prophète] s'en alla, et un lion le rencontra dans le chemin, et le tua; et son corps était étendu [par terre] dans le chemin, et l'âne se tenait auprès du corps; le lion aussi se tenait auprès du corps.
Alipokuwa akienda akakutana na simba njiani, akamuua na maiti yake ikabwagwa barabarani, yule punda wake na simba wakiwa wamesimama karibu yake.
25 Et voici quelques passants virent le corps étendu dans le chemin, et le lion qui se tenait auprès du corps; et ils vinrent le dire dans la ville où ce vieux prophète demeurait.
Baadhi ya watu waliopita pale waliona maiti imebwagwa pale chini, simba akiwa amesimama kando ya maiti, wakaenda na kutoa habari katika mji ambao nabii mzee aliishi.
26 Et le prophète qui avait ramené du chemin l'homme de Dieu, l'ayant appris, dit: C'est l'homme de Dieu qui a été rebelle au commandement de l'Eternel; c'est pourquoi l'Eternel l'a livré au lion, qui l'aura déchiré après l'avoir tué, selon la parole que l'Eternel avait dite à ce [Prophète].
Yule nabii aliyekuwa amemrudisha kutoka safari yake aliposikia habari hii akasema, “Ni yule mtu wa Mungu ambaye aliasi neno la Bwana. Bwana amemtoa kwa simba, ambaye amemrarua na kumuua, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limemwonya.”
27 Et il parla à ses fils, en disant: Sellez-moi un âne; et ils le lui sellèrent.
Nabii akawaambia wanawe, “Nitandikieni punda,” nao wakafanya hivyo.
28 Et il s'en alla, et trouva le corps de l'homme de Dieu étendu dans le chemin, et l'âne et le lion qui se tenaient auprès du corps; le lion n'avait point mangé le corps, ni déchiré l'âne.
Kisha akatoka akaenda akakuta maiti imebwagwa chini barabarani, punda na simba wakiwa wamesimama kando yake. Simba hakuwa amekula ile maiti wala kumrarua punda.
29 Alors le prophète leva le corps de l'homme de Dieu, et le mit sur l'âne, et le ramena; et ce vieux prophète revint dans la ville pour en mener deuil, et l'ensevelir.
Basi yule nabii mzee akachukua maiti ya mtu wa Mungu, akailaza juu ya punda na akairudisha katika mji wake, ili amwombolezee na kumzika.
30 Et il mit le corps de ce Prophète dans son sépulcre, et ils pleurèrent sur lui, [en disant]: Hélas mon frère!
Kisha akailaza ile maiti katika kaburi lake huyo nabii mzee, nao wakaomboleza juu yake na kusema, “Ee ndugu yangu!”
31 Et il arriva qu'après qu'il l'eut enseveli, il parla à ses fils, en disant: Quand je serai mort, ensevelissez-moi au sépulcre où est enseveli l'homme de Dieu, [et] mettez mes os auprès de lui.
Baada ya kumzika, akawaambia wanawe, “Wakati nitakapokufa, mnizike kwenye kaburi alimozikwa huyu mtu wa Mungu; lazeni mifupa yangu kando ya mifupa yake.
32 Car ce qu'il a prononcé à haute voix selon la parole de l'Eternel contre l'autel qui est à Bethel, et contre toutes les maisons des hauts lieux qui sont dans les villes de Samarie, arrivera infailliblement.
Kwa maana ujumbe alioutangaza kwa neno la Bwana dhidi ya madhabahu huko Betheli na dhidi ya madhabahu yote katika mahali pa juu pa kuabudia miungu katika miji ya Samaria, hakika yatatokea kweli.”
33 Néanmoins Jéroboam ne se détourna point de son mauvais train, mais il revint à faire des Sacrificateurs des hauts lieux d'entre les derniers du peuple; quiconque voulait, se consacrait, et était des Sacrificateurs des hauts lieux.
Hata baada ya haya, Yeroboamu hakubadili njia zake mbaya, lakini mara nyingine tena akaweka makuhani kwa ajili ya mahali pa juu pa kuabudia miungu kutoka watu wa aina zote. Yeyote aliyetaka kuwa kuhani alimweka wakfu kwa ajili ya mahali pa juu pa kuabudia miungu.
34 Et cela tourna en péché à la maison de Jéroboam, qui fut effacée et exterminée de dessus la terre.
Hii ilikuwa ndiyo dhambi ya nyumba ya Yeroboamu ambayo iliisababishia kuanguka na kuangamia kwake hadi kutoweka kwenye uso wa dunia.

< 1 Rois 13 >