< 1 Corinthiens 12 >
1 Or pour ce qui regarde les dons spirituels, je ne veux point, mes frères, que vous [en] soyez ignorants.
Basi ndugu zangu, kuhusu karama za rohoni, sitaki mkose kufahamu.
2 Vous savez que vous étiez Gentils, entraînés après les idoles muettes, selon que vous étiez menés.
Mnajua kwamba mlipokuwa watu wasiomjua Mungu, kwa njia moja au ingine mlishawishika na kupotoshwa mkielekezwa kwa sanamu zisizonena.
3 C'est pourquoi je vous fais savoir que nul homme parlant par l'Esprit de Dieu, ne dit que Jésus doit être rejeté; et que nul ne peut dire que par le Saint-Esprit, que Jésus est le Seigneur.
Kwa hiyo nawaambieni ya kuwa hakuna mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu anayeweza kusema, “Yesu na alaaniwe.” Pia hakuna mtu awezaye kusema, “Yesu ni Bwana,” isipokuwa ameongozwa na Roho Mtakatifu.
4 Or il y a diversité de dons, mais il n'y a qu'un même Esprit.
Kuna aina mbalimbali za karama, lakini Roho ni yule yule.
5 Il y a aussi diversité de ministères, mais il n'y a qu'un même Seigneur.
Kuna huduma za aina mbalimbali, lakini Bwana ni yule yule.
6 Il y a aussi diversité d'opérations; mais il n'y a qu'un même Dieu, qui opère toutes choses en tous.
Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.
7 Or à chacun est donnée la lumière de l'Esprit pour procurer l'utilité [commune].
Basi kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa faida ya wote.
8 Car à l'un est donnée par l'Esprit, la parole de sagesse; et à l'autre par le même Esprit, la parole de connaissance;
Maana mtu mmoja kwa Roho hupewa neno la hekima na mwingine neno la maarifa kwa Roho huyo huyo.
9 Et à un autre, la foi par ce même Esprit; à un autre, les dons de guérison par ce même Esprit;
Mtu mwingine imani kwa huyo Roho na mwingine karama za kuponya kwa huyo Roho mmoja.
10 Et à un autre, les opérations des miracles; à un autre, la prophétie; à un autre, le don de discerner les esprits; à un autre, la diversité de Langues; et à un autre, le don d'interpréter les Langues.
Kwa mwingine matendo ya miujiza, kwa mwingine unabii kwa mwingine kupambanua roho, kwa mwingine aina mbalimbali za lugha, na kwa mwingine bado, tafsiri za lugha.
11 Mais un seul et même Esprit fait toutes ces choses, distribuant à chacun ses dons comme il le trouve à propos.
Haya yote hufanywa na huyo huyo Roho mmoja, Roho naye humgawia kila mtu, kama apendavyo.
12 Car comme le corps n'est qu'un, et cependant il a plusieurs membres, mais tous les membres de ce corps, qui n'est qu'un, quoiqu'ils soient plusieurs, ne sont qu'un corps, il en est de même de Christ.
Kama vile mwili ulivyo mmoja nao una viungo vingi, navyo viungo vyote vya mwili ingawa ni vingi, ni mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo.
13 Car nous avons tous été baptisés d'un même Esprit, pour être un même corps, soit Juifs, soit Grecs, soit esclaves, soit libres, nous avons tous, dis-je, été abreuvés d'un même Esprit.
Kwa maana katika Roho mmoja wote tulibatizwa katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au Wayunani, kama ni watumwa au watu huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja.
14 Car aussi le corps n'est pas un seul membre, mais plusieurs.
Basi mwili si kiungo kimoja, bali ni viungo vingi.
15 Si le pied dit: parce que je ne suis pas la main, je ne suis point du corps; n'est-il pas pourtant du corps?
Kama mguu ungesema, “Kwa kuwa mimi si mkono basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya huo mguu usiwe sehemu ya mwili.
16 Et si l'oreille dit: parce que je ne suis pas l'œil, je ne suis point du corps; n'est-elle pas pourtant du corps?
Na kama sikio lingesema, “Kwa kuwa mimi si jicho, basi mimi si wa mwili,” hiyo isingefanya hilo sikio lisiwe sehemu ya mwili.
17 Si tout le corps est l'œil, où sera l'ouïe? si tout est l'ouïe, où sera l'odorat?
Kama mwili wote ungelikuwa jicho, kusikia kungekuwa wapi? Au kama mwili wote ungelikuwa sikio, kunusa kungekuwa wapi?
18 Mais maintenant Dieu a placé chaque membre dans le corps, comme il a voulu.
Lakini kama ilivyo, Mungu ameweka viungo katika mwili, kila kimoja kama alivyopenda.
19 Et si tous étaient un seul membre, où serait le corps?
Kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi?
20 Mais maintenant il y a plusieurs membres, toutefois il n'y a qu'un seul corps.
Kama ulivyo, una viungo vingi, lakini mwili ni mmoja.
21 Et l'œil ne peut pas dire à la main: je n'ai que faire de toi; ni aussi la tête aux pieds: je n'ai que faire de vous.
Jicho haliwezi kuuambia mkono, “Sina haja nawe!” Wala kichwa hakiwezi kuiambia miguu, “Sina haja na ninyi!”
22 Et qui plus est, les membres du corps qui semblent être les plus faibles, sont beaucoup plus nécessaires.
Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana.
23 Et ceux que nous estimons être les moins honorables au corps, nous les ornons avec plus de soin, et les parties qui sont en nous les moins belles à voir, sont les plus parées.
Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee;
24 Car les parties qui sont belles en nous, n'en ont pas besoin; mais Dieu a apporté ce tempérament dans notre corps, qu'il a donné plus d'honneur à ce qui en manquait;
wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa,
25 Afin qu'il n'y ait point de division dans le corps, mais que les membres aient un soin mutuel les uns des autres.
ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake.
26 Et soit que l'un des membres souffre quelque chose, tous les membres souffrent avec lui; ou soit que l'un des membres soit honoré, tous les membres ensemble s'en réjouissent.
Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.
27 Or vous êtes le corps de Christ, et vous êtes chacun un de ses membres.
Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili.
28 Et Dieu a mis dans l'Eglise, d'abord des Apôtres, ensuite des Prophètes, en troisième lieu des Docteurs, ensuite les miracles, puis les dons de guérisons, les secours, les gouvernements, les diversités de Langues.
Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, aina mbalimbali za lugha.
29 Tous sont-ils Apôtres? tous sont-ils Prophètes? tous sont-ils Docteurs? tous ont-ils le don des miracles?
Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza?
30 Tous ont-ils les dons de guérisons? tous parlent-ils [diverses] Langues? tous interprètent-ils?
Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri?
31 Or désirez avec ardeur des dons plus excellents, et je vais vous en montrer un chemin qui surpasse encore de beaucoup.
Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.