< 1 Chroniques 24 >

1 Et quant aux enfants d'Aaron, ce sont ici leurs départements. Les enfants d'Aaron furent, Nadab, Abihu, Eléazar et Ithamar.
Hii ndiyo migawanyo ya wana wa Aroni: Aroni alikuwa na wana wanne: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
2 Mais Nadab et Abihu moururent en la présence de leur père, et n'eurent point d'enfants; et Eléazar et Ithamar exercèrent la sacrificature.
Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, nao hawakuwa na wana; kwa hiyo ndugu zao Eleazari na Ithamari wakahudumu kama makuhani.
3 Or David les distribua, savoir, Tsadoc, qui était des enfants d'Eléazar; et Ahimélec, qui était des enfants d'Ithamar, pour leurs charges, dans le service qu'ils avaient à faire.
Akisaidiwa na Sadoki mwana wa Eleazari na Ahimeleki mwana wa Ithamari, Daudi aliwapanga wazao wa Aroni katika migawanyo kufuatana na wajibu wa huduma zao.
4 Et quand on les distribua, on trouva un beaucoup plus grand nombre des enfants d'Eléazar pour être Chefs de famille, que des enfants d'Ithamar, y ayant eu des enfants d'Eléazar, seize Chefs, selon leurs familles, et [n'y en ayant eu que] huit, des enfants d'Ithamar, selon leurs familles.
Idadi kubwa ya viongozi walipatikana miongoni mwa wazao wa Eleazari, kuliko miongoni mwa wazao wa Ithamari, nao waligawanywa kwa uwiano: Viongozi kumi na sita kutoka jamaa ya wazao wa Eleazari na viongozi wanane kutoka jamaa ya wazao wa Ithamari.
5 Et on fit leurs départements par sort, les entremêlant les uns parmi les autres; car les Gouverneurs du Sanctuaire, et les Gouverneurs [de la maison] de Dieu furent tirés tant des enfants d'Eléazar, que des enfants d'Ithamar.
Waliwagawanya bila upendeleo kwa kupiga kura, kwa kuwa kulikuwa na maafisa wa mahali patakatifu na maafisa wa Mungu miongoni mwa wazao wale wa Eleazari na wale wa Ithamari.
6 Et Sémahja fils de Nathanaël scribe, qui était de la Tribu de Lévi, les mit par écrit en la présence du Roi, des principaux [du peuple], de Tsadoc le Sacrificateur, d'Ahimélec, fils d'Abiathar, et des Chefs des pères [des familles] des Sacrificateurs, et de celles des Lévites. Le [chef] d'une maison de père se tirait pour Eléazar, et celui qui était tiré [après], se tirait pour Ithamar.
Mwandishi Shemaya mwana wa Nethaneli, Mlawi, aliorodhesha majina yao mbele ya Mfalme Daudi na maafisa: Kuhani Sadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa jamaa za makuhani na za Walawi: jamaa moja ikitoka upande wa Eleazari na nyingine upande wa Ithamari.
7 Le premier sort donc échut à Jéhojarib, le second à Jédahia,
Kura ya kwanza ilimwangukia Yehoyaribu, ya pili Yedaya,
8 Le troisième à Harim, le quatrième à Sehorim,
ya tatu Harimu, ya nne Seorimu,
9 Le cinquième à Malkija, le sixième à Mijamin,
ya tano Malkiya, ya sita Miyamini,
10 Le septième à Kots, le huitième à Abija,
ya saba Hakosi, ya nane Abiya,
11 Le neuvième à Jésuah, le dixième à Sécania,
ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania,
12 L'onzième à Eliasib, le douzième à Jakim,
ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu,
13 Le treizième à Huppa, le quatorzième à Jésébab,
ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu,
14 Le quinzième à Bilga, le seizième à Immer,
ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri,
15 Le dix-septième à Hézir, le dix-huitième à Pitsets,
ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi,
16 Le dix-neuvième à Péthahja, le vingtième à Ezéchiel,
ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Yehezkeli,
17 Le vingt et unième à Jakim, et le vingt et deuxième à Gamul,
ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli,
18 Le vingt et troisième à Délaja, le vingt et quatrième à Mahazia.
ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia.
19 Tel fut leur dénombrement pour le service qu'ils avaient à faire, lorsqu'ils entraient dans la maison de l'Eternel, selon qu'il leur avait été ordonné par Aaron leur père, comme l'Eternel le Dieu d'Israël le lui avait commandé.
Huu ulikuwa ndio utaratibu wao uliokubalika wa kuhudumu walipoingia katika Hekalu la Bwana kulingana na masharti waliyoelekezwa na Aroni baba yao, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyokuwa amemwamuru.
20 Et quant aux enfants de Lévi qu'il y avait eu de reste des enfants de Hamram, il y eut Subaël, et des enfants de Subaël Jehdéja.
Kuhusu wazao wa Lawi waliobaki: Kutoka kwa wana wa Amramu: alikuwa Shubaeli; kutoka kwa wana wa Shubaeli: alikuwa Yedeya.
21 De ceux de Réhabia, des enfants, [dis-je], de Réhabia, Jisija était le premier.
Kwa wa Rehabia, kutoka kwa wanawe: Ishia alikuwa wa kwanza.
22 Des Jitsharites, Sélomoth; des enfants de Sélomoth, Jahath.
Kutoka kwa Waishari: alikuwa Shelomithi, kutoka kwa wana wa Shelomithi: alikuwa Yahathi.
23 Et des enfants de Jérija, Amaria le second; Jahaziël le troisième, Jékamham le quatrième.
Wana wa Hebroni: Yeria alikuwa mkuu, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, na Yekameamu wa nne.
24 Des enfants de 'Huziël, Mica; des enfants de Mica, Samir.
Mwana wa Uzieli: alikuwa Mika; kutoka kwa wana wa Mika: alikuwa Shamiri.
25 Le frère de Mica, était Jisija; des enfants de Jisija, Zacharie.
Ndugu yake Mika: alikuwa Ishia; na kutoka kwa wana wa Ishia: alikuwa Zekaria.
26 Des enfants de Mérari, Mahli, et Musi. Des enfants de Jahazija, son fils.
Wana wa Merari: walikuwa Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia: alikuwa Beno.
27 Des enfants [donc] de Mérari, de Jahazija, son fils, et Soham, Zaccur et Hibri.
Wana wa Merari: kutoka kwa Yaazia: ni Beno, Shohamu, Zakuri na Ibri.
28 De Mahli, Eléazar, qui n'eut point de fils.
Kutoka kwa Mahli: alikuwa Eleazari, ambaye hakuwa na wana.
29 De Kis, les enfants de Kis, Jérahméël.
Kutoka kwa Kishi: mwana wa Kishi: alikuwa Yerameeli.
30 Et des enfants de Musi, Mahli, Héder, et Jérimoth. Ce sont là les enfants des Lévites, selon les maisons de leurs pères.
Nao wana wa Mushi: walikuwa Mahli, Ederi na Yeremothi. Hawa walikuwa Walawi kulingana na jamaa zao.
31 Et ils jetèrent pareillement les sorts selon le nombre de leurs frères les enfants d'Aaron, en la présence du Roi David, de Tsadoc, et d'Ahimélec, et des Chefs des pères [des familles] des Sacrificateurs et des Lévites; les Chefs des pères [de famille] correspondant à leurs plus jeunes frères.
Pia walipiga kura kama vile ndugu zao wazao wa Aroni walivyofanya, mbele ya Mfalme Daudi, Sadoki, Ahimeleki na mbele ya viongozi wa jamaa ya makuhani na ya Walawi. Jamaa za ndugu wakubwa zilitendewa sawasawa na zile za ndugu wadogo.

< 1 Chroniques 24 >