< 1 Chroniques 19 >

1 Or il arriva après cela que Nahas Roi des enfants de Hammon mourut, et son fils régna en sa place.
Baada ya muda, Nahashi mfalme wa Waamoni akafa, mwanawe akaingia mahali pake.
2 Et David dit: J'userai de gratuité envers Hanun, fils de Nahas; car son père a usé de gratuité envers moi. Ainsi David envoya des messagers pour le consoler sur la mort de son père; et les serviteurs de David vinrent au pays des enfants de Hammon vers Hanun pour le consoler.
Daudi akawaza, “Nitamtendea wema Hanuni mwana wa Nahashi, kwa sababu baba yake alinitendea wema.” Hivyo Daudi akatuma wajumbe ili kumfariji Hanuni kwa ajili ya kifo cha baba yake. Watu wa Daudi walipofika kwa Hanuni katika nchi ya Waamoni ili kumfariji,
3 Mais les principaux d'entre les enfants de Hammon dirent à Hanun: Penses-tu que ce soit pour honorer ton père que David t'a envoyé des consolateurs? n'est-ce pas pour examiner exactement et épier le pays, afin de le détruire, que ses serviteurs sont venus vers toi?
wakuu wa Waamoni wakamwambia Hanuni, “Hivi unadhani Daudi anamheshimu baba yako kwa kuwatuma wajumbe kukufariji? Je, hawa watu hawakuja kuipeleleza na kuidadisi nchi ili waishinde?”
4 Hanun donc prit les serviteurs de David, et les fit raser, et fit couper leurs habits par le milieu jusqu'aux hanches, puis il les renvoya.
Kwa hiyo Hanuni akawakamata watu wa Daudi, akawanyoa ndevu akakata nguo zao katikati kwenye matako, akawaacha waende zao.
5 Et ils s'en allèrent, et le firent savoir par [le moyen] de quelques personnes à David, qui envoya au devant d'eux; car ces hommes-là étaient fort confus. Et le Roi leur manda: Demeurez à Jérico jusqu'à ce que votre barbe soit recrue; et alors vous retournerez.
Mtu mmoja alipofika na kumpasha Daudi habari za watu hawa, akawatuma wajumbe wengine kuwalaki, kwa maana walikuwa wamevunjiwa heshima sana. Mfalme akasema, “Kaeni huko Yeriko mpaka ndevu zenu ziote, ndipo mje.”
6 Or les enfants de Hammon voyant qu'ils s'étaient mis en mauvaise odeur auprès de David, Hanun et eux envoyèrent mille talents d'argent, pour prendre à leurs dépens des chariots et des gens de cheval de Mésopotamie, et de Syrie, de Mahaca, et de Tsoba.
Waamoni walipotambua kuwa wamekuwa machukizo kwa Daudi, Hanuni na Waamoni wakatuma talanta 1,000 za fedha ili kukodisha magari ya vita pamoja na waendeshaji wa hayo magari ya kukokotwa na farasi, kutoka Aramu-Naharaimu, Aramu-Maaka na Soba.
7 Et ils levèrent à leurs frais pour eux trente-deux mille hommes, [et] des chariots, et le Roi de Mahaca avec son peuple qui vinrent, et se campèrent devant Médeba. Les Hammonites aussi s'assemblèrent de leurs villes, et vinrent pour combattre.
Wakakodisha magari ya vita 32,000 yakiwa na waendeshaji wake, pamoja na mfalme wa Maaka na vikosi vyake, wakaja na kupiga kambi karibu na Medeba. Waamoni nao wakakusanyika toka miji yao, wakatoka ili kupigana vita.
8 Ce que David ayant appris, il envoya Joab, et ceux de toute l'armée qui étaient les plus vaillants.
Daudi aliposikia jambo hili, akamtuma Yoabu na jeshi lote la wapiganaji.
9 Et les enfants de Hammon sortirent, et rangèrent leur armée en bataille à l'entrée de la ville, et les Rois qui étaient venus, étaient à part dans la campagne.
Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati wale wafalme wengine waliokuja nao walijipanga kwa vita uwanjani.
10 Et Joab voyant que l'armée était tournée contre lui, devant et derrière, prit de tous les gens d'élite d'Israël, et les rangea contre les Syriens.
Yoabu akaona kuwa mbele yake na nyuma yake kumepangwa vita; kwa hiyo akachagua baadhi ya vikosi vilivyo bora sana katika Israeli akavipanga dhidi ya Waaramu.
11 Et il donna la conduite du reste du peuple à Abisaï son frère; et on les rangea contre les enfants de Hammon.
Akawaweka wale wanajeshi wengine waliobaki chini ya amri ya Abishai ndugu yake, nao wakapangwa ili wakabiliane na Waamoni.
12 Et [Joab lui] dit: Si les Syriens sont plus forts que moi, tu viendras me délivrer; et si les enfants de Hammon sont plus forts que toi, je te délivrerai.
Yoabu akasema, “Kama Waaramu watanizidi nguvu, basi itakupasa wewe unisaidie; lakini kama Waamoni watakuzidi nguvu, basi mimi nitakusaidia.
13 Sois vaillant, et portons-nous vaillamment pour notre peuple, et pour les villes de notre Dieu; et que l'Eternel fasse ce qui lui semblera bon.
Uwe hodari na tupigane kwa ujasiri kwa ajili ya watu wetu na miji ya Mungu wetu. Bwana atafanya lile lililo jema machoni pake.”
14 Alors Joab et le peuple qui était avec lui s'approchèrent pour donner bataille aux Syriens, qui s'enfuirent de devant lui.
Basi Yoabu na vikosi vyake wakasonga mbele kupigana na Waaramu, nao Waaramu wakakimbia mbele yake.
15 Et les enfants de Hammon voyant que les Syriens s'en étaient fuis, eux aussi s'enfuirent de devant Abisaï frère de Joab, et rentrèrent dans la ville; et Joab revint à Jérusalem.
Waamoni walipoona Waaramu wanakimbia, nao pia wakakimbia mbele ya nduguye Abishai na kuingia ndani ya mji. Basi Yoabu akarudi Yerusalemu.
16 Mais les Syriens, qui avaient été battus par ceux d'Israël, envoyèrent des messagers, et firent venir les Syriens qui étaient au delà du fleuve; et Sophach capitaine de l'armée de Hadarhézer les conduisait.
Baada ya Waaramu kuona kwamba wameshindwa na Israeli, wakapeleka wajumbe na kuwataka Waaramu wengine kutoka ngʼambo ya Mto Frati, wakiongozwa na Shofaki, jemadari wa jeshi la Hadadezeri.
17 Ce qui ayant été rapporté à David, il assembla tout Israël, et passa le Jourdain, et alla au devant d'eux, et se rangea en bataille contr'eux. David donc rangea la bataille contre les Syriens, et ils combattirent contre lui.
Daudi alipoambiwa haya, akawakusanya Israeli wote na kuvuka Yordani. Akasonga mbele dhidi yao na akajipanga kuwakabili. Daudi akapanga vita ili kupigana na Waaramu, nao wakapigana dhidi yake.
18 Mais les Syriens s'enfuirent de devant Israël; et David défit sept mille chariots des Syriens, et quarante mille hommes de pied, et il tua Sophach le Chef de l'armée.
Lakini Waaramu wakakimbia mbele ya Israeli, naye Daudi akawaua waendesha magari 7,000 na askari wao wa miguu 40,000. Pia akamuua Shofaki, jemadari wa jeshi lao.
19 Alors les serviteurs de Hadarhézer voyant qu'ils avaient été battus par ceux d'Israël, firent la paix avec David, et lui furent asservis; et les Syriens ne voulurent plus secourir les enfants de Hammon.
Raiya wa Hadadezeri walipoona kuwa wameshindwa na Israeli, wakafanya mapatano ya amani na Daudi, wakawa watumishi wake. Hivyo Waaramu hawakukubali kuwasaidia Waamoni tena.

< 1 Chroniques 19 >