< 1 Chroniques 16 >

1 Ils amenèrent donc l'Arche de Dieu, et la posèrent dans le tabernacle que David lui avait tendu; et on offrit devant Dieu des holocaustes et des sacrifices de prospérités.
Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
2 Et quand David eut achevé d'offrir les holocaustes et les sacrifices de prospérités, il bénit le peuple au Nom de l'Eternel.
Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana.
3 Et il distribua à chacun, tant aux hommes qu'aux femmes, un pain, et une pièce de chair, et une bouteille de vin.
Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.
4 Et il établit quelques-uns des Lévites devant l'Arche de l'Eternel, pour y faire le service, pour célébrer, remercier, et louer le Dieu d'Israël.
Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli:
5 Asaph était le premier, et Zacharie le second, Jéhiël, Sémiramoth, Jéhiël, Mattitia, Eliab, Bénéja, Hobed-Edom, et Jéchiël, qui avaient des instruments de musique, [savoir] des musettes et des violons; et Asaph faisait retentir [sa voix] avec des cymbales.
Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi,
6 Et Bénéja et Jahaziël Sacrificateurs étaient continuellement avec des trompettes devant l'Arche de l'alliance de Dieu.
nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.
7 Et en ce même jour David remit entre les mains d'Asaph et de ses frères, les [Psaumes suivants], pour commencer à célébrer l'Eternel.
Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:
8 CELEBREZ l'Eternel, invoquez son Nom, faites connaître parmi les peuples ses exploits.
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
9 Chantez lui, psalmodiez lui, parlez de toutes ses merveilles.
Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
10 Glorifiez-vous du Nom de sa sainteté; que le cœur de ceux qui cherchent l'Eternel se réjouisse.
Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
11 Recherchez l'Eternel et sa force, cherchez continuellement sa face.
Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
12 Souvenez-vous des merveilles qu'il a faites; de ses miracles, et des jugements de sa bouche.
Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
13 La postérité d'Israël sont ses serviteurs; les enfants de Jacob sont ses
enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
14 Il est l'Eternel notre Dieu; ses jugements sont par toute la terre.
Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
15 Souvenez-vous toujours de son alliance, de la parole qu'il a prescrite en mille générations;
Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
16 Du traité qu'il a fait avec Abraham; et de son serment fait à Isaac;
agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
17 Lequel il a confirmé à Jacob [et] à Israël, pour être une ordonnance et une alliance éternelle.
Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
18 En disant: Je te donnerai le pays de Canaan, pour le lot de ton héritage;
“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
19 Encore que vous soyez un petit nombre de gens, et même que vous y séjourniez depuis peu de temps, comme étrangers.
Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
20 Car ils étaient errants de nation en nation, et d'un Royaume vers un autre peuple.
walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
21 Il n'a pas souffert qu'aucun les outrageât; même il a châtié les Rois pour l'amour d'eux.
Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
22 [Et il a dit]: Ne touchez point à mes Oints, et ne faites point de mal à mes Prophètes.
“Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
23 TOUTE la terre, chantez à l'Eternel, prêchez chaque jour sa délivrance;
Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
24 Racontez sa gloire parmi les nations, [et] ses merveilles parmi tous les peuples.
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
25 Car l'Eternel est grand, et très-digne de louange, il est plus redoutable que tous les dieux.
Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
26 Et en effet tous les dieux des peuples sont des idoles; mais l'Eternel a fait les cieux.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
27 La Majesté et la magnificence [marchent] devant lui; la force et la joie sont dans le lieu où il habite.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
28 Familles des peuples, attribuez à l'Eternel, attribuez à l'Eternel gloire et force.
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
29 Attribuez à l'Eternel la gloire due à son Nom; apportez l'oblation, et présentez-vous devant lui; prosternez-vous devant l'Eternel avec une sainte magnificence.
mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
30 Vous tous les habitants de la terre tremblez, tout étonnés pour la présence de sa face; car la terre habitable est affermie [par lui], sans qu'elle soit ébranlée.
Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
31 Que les cieux se réjouissent, que la terre s'égaye, et qu'on dise parmi les nations: L'Eternel règne.
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
32 Que la mer et tout ce qu'elle contient bruie; que les champs et tout ce qui est en eux se réjouissent.
Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
33 Alors les arbres de la forêt crieront de joie au devant de l'Eternel, parce qu'il vient juger la terre.
Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
34 Célébrez l'Eternel, car il est bon; parce que sa gratuité demeure à jamais.
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
35 Et dites: Ô Dieu! de notre salut, sauve-nous, et nous rassemble, et nous retire d'entre les nations, pour célébrer ton saint Nom, [et] pour nous glorifier en ta louange.
Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
36 Béni soit l'Eternel le Dieu d'Israël, depuis un siècle jusqu'à l'autre! Et tout le peuple dit: Amen; et on loua l'Eternel.
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
37 On laissa donc là devant l'Arche de l'alliance de l'Eternel, Asaph et ses frères, pour faire le service continuellement, selon ce qu'il y avait à faire chaque jour devant l'Arche.
Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
38 Et Hobed-Edom, et ses frères, au nombre de soixante-huit, Hobed-Edom, dis-je, fils de Jéduthun, et Hosa pour portiers.
Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
39 Et [on laissa] Tsadoc le Sacrificateur, et ses frères Sacrificateurs, devant le pavillon de l'Eternel, dans le haut lieu qui était à Gabaon,
Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
40 Pour offrir des holocaustes à l'Eternel continuellement sur l'autel de l'holocauste, le matin, et le soir, et pour faire toutes les choses qui sont écrites dans la Loi de l'Eternel, lesquelles il avait commandées à Israël;
ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
41 Et avec eux Héman et Jéduthun, et les autres qui furent choisis et marqués par leur nom, pour célébrer l'Eternel, parce que sa gratuité demeure éternellement.
Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
42 Et Héman et Jéduthun étaient avec ceux-là; il y avait aussi des trompettes, et des cymbales pour ceux qui faisaient retentir [leur voix], et des instruments pour chanter les cantiques de Dieu; et les fils de Jéduthun étaient portiers.
Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
43 Puis tout le peuple s'en alla chacun en sa maison, et David aussi s'en retourna pour bénir sa maison.
Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.

< 1 Chroniques 16 >