< Psaumes 107 >

1 Louez l’Éternel, car il est bon, Car sa miséricorde dure à toujours!
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 Qu’ainsi disent les rachetés de l’Éternel, Ceux qu’il a délivrés de la main de l’ennemi,
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 Et qu’il a rassemblés de tous les pays, De l’orient et de l’occident, du nord et de la mer!
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Ils erraient dans le désert, ils marchaient dans la solitude, Sans trouver une ville où ils pussent habiter.
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 Ils souffraient de la faim et de la soif; Leur âme était languissante.
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 Dans leur détresse, ils crièrent à l’Éternel, Et il les délivra de leurs angoisses;
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7 Il les conduisit par le droit chemin, Pour qu’ils arrivassent dans une ville habitable.
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8 Qu’ils louent l’Éternel pour sa bonté, Et pour ses merveilles en faveur des fils de l’homme!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 Car il a satisfait l’âme altérée, Il a comblé de biens l’âme affamée.
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 Ceux qui avaient pour demeure les ténèbres et l’ombre de la mort Vivaient captifs dans la misère et dans les chaînes,
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 Parce qu’ils s’étaient révoltés contre les paroles de Dieu, Parce qu’ils avaient méprisé le conseil du Très-Haut.
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 Il humilia leur cœur par la souffrance; Ils succombèrent, et personne ne les secourut.
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 Dans leur détresse, ils crièrent à l’Éternel, Et il les délivra de leurs angoisses;
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 Il les fit sortir des ténèbres et de l’ombre de la mort, Et il rompit leurs liens.
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 Qu’ils louent l’Éternel pour sa bonté, Et pour ses merveilles en faveur des fils de l’homme!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16 Car il a brisé les portes d’airain, Il a rompu les verrous de fer.
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Les insensés, par leur conduite coupable Et par leurs iniquités, s’étaient rendus malheureux.
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
18 Leur âme avait en horreur toute nourriture, Et ils touchaient aux portes de la mort.
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 Dans leur détresse, ils crièrent à l’Éternel, Et il les délivra de leurs angoisses;
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 Il envoya sa parole et les guérit, Il les fit échapper de la fosse.
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 Qu’ils louent l’Éternel pour sa bonté, Et pour ses merveilles en faveur des fils de l’homme!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 Qu’ils offrent des sacrifices d’actions de grâces, Et qu’ils publient ses œuvres avec des cris de joie!
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
23 Ceux qui étaient descendus sur la mer dans des navires, Et qui travaillaient sur les grandes eaux,
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 Ceux-là virent les œuvres de l’Éternel Et ses merveilles au milieu de l’abîme.
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
25 Il dit, et il fit souffler la tempête, Qui souleva les flots de la mer.
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 Ils montaient vers les cieux, ils descendaient dans l’abîme; Leur âme était éperdue en face du danger;
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
27 Saisis de vertige, ils chancelaient comme un homme ivre, Et toute leur habileté était anéantie.
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 Dans leur détresse, ils crièrent à l’Éternel, Et il les délivra de leurs angoisses;
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
29 Il arrêta la tempête, ramena le calme, Et les ondes se turent.
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 Ils se réjouirent de ce qu’elles s’étaient apaisées, Et l’Éternel les conduisit au port désiré.
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
31 Qu’ils louent l’Éternel pour sa bonté, Et pour ses merveilles en faveur des fils de l’homme!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
32 Qu’ils l’exaltent dans l’assemblée du peuple, Et qu’ils le célèbrent dans la réunion des anciens!
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
33 Il change les fleuves en désert, Et les sources d’eaux en terre desséchée,
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
34 Le pays fertile en pays salé, A cause de la méchanceté de ses habitants.
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
35 Il change le désert en étang, Et la terre aride en sources d’eaux,
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 Et il y établit ceux qui sont affamés. Ils fondent une ville pour l’habiter;
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 Ils ensemencent des champs, plantent des vignes, Et ils en recueillent les produits.
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 Il les bénit, et ils deviennent très nombreux, Et il ne diminue point leur bétail.
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39 Sont-ils amoindris et humiliés Par l’oppression, le malheur et la souffrance;
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 Verse-t-il le mépris sur les grands, Les fait-il errer dans des déserts sans chemin,
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 Il relève l’indigent et le délivre de la misère, Il multiplie les familles comme des troupeaux.
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 Les hommes droits le voient et se réjouissent, Mais toute iniquité ferme la bouche.
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
43 Que celui qui est sage prenne garde à ces choses, Et qu’il soit attentif aux bontés de l’Éternel.
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.

< Psaumes 107 >