< Proverbes 23 >
1 Si tu es à table avec un grand, Fais attention à ce qui est devant toi;
Unapoketi kula pamoja na mtawala, angalia kwa uangalifu kilichopo mbele yako,
2 Mets un couteau à ta gorge, Si tu as trop d’avidité.
na kama ni mtu unayependa kula chakula sana weka kisu kooni.
3 Ne convoite pas ses friandises: C’est un aliment trompeur.
Usitamani vinono vyake maana ni chakula cha uongo.
4 Ne te tourmente pas pour t’enrichir, N’y applique pas ton intelligence.
Usifanye kazi sana ili kupata mali; uwe na busara ya kutosha ili ujue wakati wa kuacha.
5 Veux-tu poursuivre du regard ce qui va disparaître? Car la richesse se fait des ailes, Et comme l’aigle, elle prend son vol vers les cieux.
Je utaruhusu macho yako yaangaze juu yake? Itaondoka, maana itawaa mabawa kama tai na kuruka angani.
6 Ne mange pas le pain de celui dont le regard est malveillant, Et ne convoite pas ses friandises;
Usile chakula cha yule mwenye jicho baya- na usiwe na shauku ya vinono vyake,
7 Car il est comme les pensées de son âme. Mange et bois, te dira-t-il; Mais son cœur n’est point avec toi.
maana ni mtu mwenye kuhesabu gharama ya chakula. “Kula na kunywa!” anakuambia, lakini moyo wake haupo pamoja nawe.
8 Tu vomiras le morceau que tu as mangé, Et tu auras perdu tes propos agréables.
Utatapika kiasi kidogo ulichokula na utakuwa umepoteza sifa zako njema.
9 Ne parle pas aux oreilles de l’insensé, Car il méprise la sagesse de tes discours.
Usiongee katika usikivu wa mpumbavu, maana atadharau hekima ya maneno yako.
10 Ne déplace pas la borne ancienne, Et n’entre pas dans le champ des orphelins;
Usihamishe jiwe la mpaka wa kale au kunyang'anya mashamba ya yatima,
11 Car leur vengeur est puissant: Il défendra leur cause contre toi.
maana Mkombozi wao ni imara na atatetea kesi yao dhidi yako.
12 Ouvre ton cœur à l’instruction, Et tes oreilles aux paroles de la science.
Elekeza moyo wako katika mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
13 N’épargne pas la correction à l’enfant; Si tu le frappes de la verge, il ne mourra point.
Usizuie kuadilisha mtoto, maana ukimchapa kwa fimbo, hatakufa.
14 En le frappant de la verge, Tu délivres son âme du séjour des morts. (Sheol )
Ni wewe unayepaswa kumchapa kwa fimbo na kuikoa nafsi yake kuzimu. (Sheol )
15 Mon fils, si ton cœur est sage, Mon cœur à moi sera dans la joie;
Mwanangu, kama moyo wako una busara, basi moyo wangu utafurahi pia;
16 Mes entrailles seront émues d’allégresse, Quand tes lèvres diront ce qui est droit.
sehemu zangu ndani kabisa zitafurahi sana midomo yako inaponena haki.
17 Que ton cœur n’envie point les pécheurs, Mais qu’il ait toujours la crainte de l’Éternel;
Usiruhusu moyo wako kuwahusudu wenye dhambi, lakini endelea kumcha Yehova siku zote.
18 Car il est un avenir, Et ton espérance ne sera pas anéantie.
Hakika tumaini lako halitaondolewa na siku zako za hapo baadaye.
19 Écoute, mon fils, et sois sage; Dirige ton cœur dans la voie droite.
Sikia- wewe! - mwanangu, na uwe mwenye busara na uelekeze moyo wako katika njia.
20 Ne sois pas parmi les buveurs de vin, Parmi ceux qui font excès des viandes:
Usishirikiane pamoja na walevi, au pamoja na walaji wa nyama walafi,
21 Car l’ivrogne et celui qui se livre à des excès s’appauvrissent, Et l’assoupissement fait porter des haillons.
maana mlevi na mlafi wanakuwa masikini na usingizi utawavika kwa matambara.
22 Écoute ton père, lui qui t’a engendré, Et ne méprise pas ta mère, quand elle est devenue vieille.
Msikilize baba yako ambaye alikuzaa na usimdharau mama yako wakati akiwa mzee.
23 Acquiers la vérité, et ne la vends pas, La sagesse, l’instruction et l’intelligence.
Inunue kweli, lakini usiiuze; nunua hekima, nidhamu, na ufahamu.
24 Le père du juste est dans l’allégresse, Celui qui donne naissance à un sage aura de la joie.
Baba yake mwenye haki atafurahia sana, na yule amzaaye mtoto mwenye busara atamfurahia.
25 Que ton père et ta mère se réjouissent, Que celle qui t’a enfanté soit dans l’allégresse!
Mfurahishe baba yako na mama yako na yule aliyekuzaa afurahie.
26 Mon fils, donne-moi ton cœur, Et que tes yeux se plaisent dans mes voies.
Mwanangu, nipe moyo wako na macho yako yachunguze njia zangu.
27 Car la prostituée est une fosse profonde, Et l’étrangère un puits étroit.
Maana malaya ni shimo refu, na mke wa mume mwingine ni kisima chembamba.
28 Elle dresse des embûches comme un brigand, Et elle augmente parmi les hommes le nombre des perfides.
Anavizia kama mnyang'anyi na huongeza idadi ya wadanganyifu miongoni mwa wanadamu.
29 Pour qui les ah? Pour qui les hélas? Pour qui les disputes? Pour qui les plaintes? Pour qui les blessures sans raison? Pour qui les yeux rouges?
Nani mwenye taabu? Nani mwenye huzuni? Nani mwenye mapigano? Nani mwenye malalamiko? Nani mwenye majeraha bila sababu? Nani mwenye macho mekundu?
30 Pour ceux qui s’attardent auprès du vin, Pour ceux qui vont déguster du vin mêlé.
Ni wale ambao huzengea kwenye mvinyo, wale wanaojaribu kuchanganya mvinyo.
31 Ne regarde pas le vin qui paraît d’un beau rouge, Qui fait des perles dans la coupe, Et qui coule aisément.
Usiutazame mvinyo ukiwa mwekundu, wakati unametameta kwenye kikombe na kutelemka kwa uraini.
32 Il finit par mordre comme un serpent, Et par piquer comme un basilic.
Mwisho wake unauma kama nyoka na sumu yake kama kifutu.
33 Tes yeux se porteront sur des étrangères, Et ton cœur parlera d’une manière perverse.
Macho yako yataona vitu vigeni na moyo wako utatamka vitu vya ukaidi.
34 Tu seras comme un homme couché au milieu de la mer, Comme un homme couché sur le sommet d’un mât:
Utakuwa kama anayelala kwenye bahari au anayelala juu ya mlingoti. “
35 On m’a frappé, … je n’ai point de mal!… On m’a battu, … je ne sens rien!… Quand me réveillerai-je?… J’en veux encore!
Wamenipiga,” utasema, “lakini sikuumia. Wamenichapa, lakini sikuwa na hisia. Nitaamka lini? Nitatafuta kinywaji kingine.”