< Job 13 >
1 Voici, mon œil a vu tout cela, Mon oreille l’a entendu et y a pris garde.
Tazama, jicho langu limeyaona haya yote; sikio langu limeyasikia na kuyaelewa hayo.
2 Ce que vous savez, je le sais aussi, Je ne vous suis point inférieur.
Kile mnachokifahamu, ndicho hicho mimi pia ninachokifahamu; Mimi siyo duni kwenu ninyi.
3 Mais je veux parler au Tout-Puissant, Je veux plaider ma cause devant Dieu;
Hata hivyo, Mimi ningeweza kuzungumza na mwenye nguvu; Mimi natamani kusemezana na Mungu.
4 Car vous, vous n’imaginez que des faussetés, Vous êtes tous des médecins de néant.
Lakini ninyi mnauficha ukweli kwa uongo; ninyi nyote ni tabibu msiokuwa na thamani.
5 Que n’avez-vous gardé le silence? Vous auriez passé pour avoir de la sagesse.
Laiti, kwamba kwa pamoja mngeshikilia amani yenu! Hilo lingekuwa hekima yenu ninyi.
6 Écoutez, je vous prie, ma défense, Et soyez attentifs à la réplique de mes lèvres.
Sikia sasa kuhoji kwangu; Sikiliza kusihi kwa midomo yangu mwenyewe.
7 Direz-vous en faveur de Dieu ce qui est injuste, Et pour le soutenir alléguerez-vous des faussetés?
Ninyi mtazungumza visivyo haki kwa ajili ya Mungu, na ninyi mtazungumza udanganyifu kwa yeye? Ni kweli ninyi mngeonyesha ukarimu kwa yeye?
8 Voulez-vous avoir égard à sa personne? Voulez-vous plaider pour Dieu?
Ni kweli ninyi mngetetea katika mahakama kama mawakili wa Mungu?
9 S’il vous sonde, vous approuvera-t-il? Ou le tromperez-vous comme on trompe un homme?
Je, kweli ingekuwa vizuri kwenu wakati yeye akiwatafuta ninyi? Mngeweza ninyi kumdanganya yeye kama mlivyoweza kuwadanganya watu?
10 Certainement il vous condamnera, Si vous n’agissez en secret que par égard pour sa personne.
Yeye kwa hakika angewathibitisha upya ninyi ikiwa katika siri ninyi mmeonyesha kutokukamilika.
11 Sa majesté ne vous épouvantera-t-elle pas? Sa terreur ne tombera-t-elle pas sur vous?
Je, ukuu wake usingewafanya ninyi muogope? Je, utisho wake usingeshuka juu yenu?
12 Vos sentences sont des sentences de cendre, Vos retranchements sont des retranchements de boue.
Hadithi zenu za misemo ya kukariri, ni mithali zimetengenezwa kwa majivu; utetezi wenu ni utetezi uliotengenezwa kwa udongo wa mfinyanzi.
13 Taisez-vous, laissez-moi, je veux parler! Il m’en arrivera ce qu’il pourra.
Shikilieni amani yenu, mniache peke yangu, ili ya kwamba nipate kusema, acheni yaje yale yanayoweza kuja kwangu.
14 Pourquoi saisirais-je ma chair entre les dents? J’exposerai plutôt ma vie.
Nitaichukua nyama yangu mwenywewe katika meno yangu; Nitayachukua maisha yangu katika mikono yangu.
15 Voici, il me tuera; je n’ai rien à espérer; Mais devant lui je défendrai ma conduite.
Tazama, ikiwa ataniua mimi, sitakuwa na tumaini lililobakia; hata hivyo, nitazitetea njia zangu mbele zake yeye.
16 Cela même peut servir à mon salut, Car un impie n’ose paraître en sa présence.
Hiki kitakuwa sababu ya kutohesabiwa hatia, kwamba mimi sikuja mbele zake kama mtu asiyemcha Mungu.
17 Écoutez, écoutez mes paroles, Prêtez l’oreille à ce que je vais dire.
Mungu, sikiliza kwa makini kuzungumza kwangu; ruhusu kutangaza kwangu kuje kwenye masikio yako.
18 Me voici prêt à plaider ma cause; Je sais que j’ai raison.
Tazama sasa, Nimeuweka utetezi wangu katika mpangilio, Mimi ninafahamu kwamba mimi sina hatia.
19 Quelqu’un disputera-t-il contre moi? Alors je me tais, et je veux mourir.
Ni nani anayeweza kushindana na mimi katika mahakama? Ikiwa mlikuja kufanya hivyo, na kama mimi nilithibitishwa kukosea, ndipo ningekuwa kimya na kuyatoa maisha yangu.
20 Seulement, accorde-moi deux choses Et je ne me cacherai pas loin de ta face:
Mungu, fanya mambo mawili kwa ajili yangu, na tena Mimi sitajificha kutoka katika uso wako.
21 Retire ta main de dessus moi, Et que tes terreurs ne me troublent plus.
Ondoa kutoka kwangu mkono wako unaotesa, na usiache utisho wako unifanye mimi kuogopa.
22 Puis appelle, et je répondrai, Ou si je parle, réponds-moi!
Ndipo niite mimi, na mimi nitakujibu; au uniache mimi niseme na wewe na wewe unijibu mimi.
23 Quel est le nombre de mes iniquités et de mes péchés? Fais-moi connaître mes transgressions et mes péchés.
Je, maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi? Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
24 Pourquoi caches-tu ton visage, Et me prends-tu pour ton ennemi?
Kwa nini unaficha uso wako kutoka kwangu mimi na kunitendea mimi kama adui yako?
25 Veux-tu frapper une feuille agitée? Veux-tu poursuivre une paille desséchée?
Je, wewe utalitesa jani linalopeperushwa? Je, utaendelea kulifuatilia bua kavu?
26 Pourquoi m’infliger d’amères souffrances, Me punir pour des fautes de jeunesse?
Kwa maana wew unaandika chini vitu vichungu dhidi yangu mimi; wewe unanifanya mimi kurithi uovu wa ujana wangu.
27 Pourquoi mettre mes pieds dans les ceps, Surveiller tous mes mouvements, Tracer une limite à mes pas,
Wewe pia unaiweka miguu yangu katika nguo nyembamba; wewe waangalia njia zangu zote; wewe wachunguza chini mahali ambapo nyayo za miguu yangu zimekanyaga.
28 Quand mon corps tombe en pourriture, Comme un vêtement que dévore la teigne?
japokuwa mimi ni kama kitu kilichooza ambacho hutupwa mbali, kama vazi lile ambalo nondo wamelila.