< Job 12 >

1 Job prit la parole et dit:
Ndipo Ayubu akajibu:
2 On dirait, en vérité, que le genre humain c’est vous, Et qu’avec vous doit mourir la sagesse.
“Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
3 J’ai tout aussi bien que vous de l’intelligence, moi, Je ne vous suis point inférieur; Et qui ne sait les choses que vous dites?
Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
4 Je suis pour mes amis un objet de raillerie, Quand j’implore le secours de Dieu; Le juste, l’innocent, un objet de raillerie!
“Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
5 Au malheur le mépris! C’est la devise des heureux; A celui dont le pied chancelle est réservé le mépris.
Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
6 Il y a paix sous la tente des pillards, Sécurité pour ceux qui offensent Dieu, Pour quiconque se fait un dieu de sa force.
Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
7 Interroge les bêtes, elles t’instruiront, Les oiseaux du ciel, ils te l’apprendront;
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
8 Parle à la terre, elle t’instruira; Et les poissons de la mer te le raconteront.
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
9 Qui ne reconnaît chez eux la preuve Que la main de l’Éternel a fait toutes choses?
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
10 Il tient dans sa main l’âme de tout ce qui vit, Le souffle de toute chair d’homme.
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
11 L’oreille ne discerne-t-elle pas les paroles, Comme le palais savoure les aliments?
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
12 Dans les vieillards se trouve la sagesse, Et dans une longue vie l’intelligence.
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
13 En Dieu résident la sagesse et la puissance. Le conseil et l’intelligence lui appartiennent.
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
14 Ce qu’il renverse ne sera point rebâti, Celui qu’il enferme ne sera point délivré.
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
15 Il retient les eaux et tout se dessèche; Il les lâche, et la terre en est dévastée.
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
16 Il possède la force et la prudence; Il maîtrise celui qui s’égare ou fait égarer les autres.
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
17 Il emmène captifs les conseillers; Il trouble la raison des juges.
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
18 Il délie la ceinture des rois, Il met une corde autour de leurs reins.
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
19 Il emmène captifs les sacrificateurs; Il fait tomber les puissants.
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
20 Il ôte la parole à ceux qui ont de l’assurance; Il prive de jugement les vieillards.
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
21 Il verse le mépris sur les grands; Il relâche la ceinture des forts.
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
22 Il met à découvert ce qui est caché dans les ténèbres, Il produit à la lumière l’ombre de la mort.
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
23 Il donne de l’accroissement aux nations, et il les anéantit; Il les étend au loin, et il les ramène dans leurs limites.
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
24 Il enlève l’intelligence aux chefs des peuples, Il les fait errer dans les déserts sans chemin;
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
25 Ils tâtonnent dans les ténèbres, et ne voient pas clair; Il les fait errer comme des gens ivres.
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.

< Job 12 >