< Éphésiens 5 >
1 Devenez donc les imitateurs de Dieu, comme des enfants bien-aimés;
Kwa hiyo, mfuateni Mungu kama watoto wapendwao,
2 et marchez dans la charité, à l’exemple de Christ, qui nous a aimés, et qui s’est livré lui-même à Dieu pour nous comme une offrande et un sacrifice de bonne odeur.
mkiishi maisha ya upendo, kama vile Kristo alivyotupenda sisi akajitoa kwa ajili yetu kuwa sadaka yenye harufu nzuri na dhabihu kwa Mungu.
3 Que l’impudicité, qu’aucune espèce d’impureté, et que la cupidité, ne soient pas même nommées parmi vous, ainsi qu’il convient à des saints.
Lakini uasherati, usitajwe miongoni mwenu, wala uchafu wa aina yoyote, wala tamaa, kwa sababu mambo haya hayastahili miongoni mwa watakatifu.
4 Qu’on n’entende ni paroles déshonnêtes, ni propos insensés, ni plaisanteries, choses qui sont contraires à la bienséance; qu’on entende plutôt des actions de grâces.
Wala pasiwepo mazungumzo machafu ya aibu, au maneno ya upuzi au mzaha, ambayo hayafai, badala yake mshukuruni Mungu.
5 Car, sachez-le bien, aucun impudique, ou impur, ou cupide, c’est-à-dire, idolâtre, n’a d’héritage dans le royaume de Christ et de Dieu.
Kwa habari ya mambo haya mjue hakika kwamba: Msherati, wala mtu mwovu, wala mwenye tamaa mbaya, mtu kama huyo ni mwabudu sanamu, kamwe hataurithi Ufalme wa Kristo na wa Mungu.
6 Que personne ne vous séduise par de vains discours; car c’est à cause de ces choses que la colère de Dieu vient sur les fils de la rébellion.
Mtu yeyote na asiwadanganye kwa maneno matupu, kwa kuwa hasira ya Mungu huwaka kwa sababu ya mambo kama haya juu ya wale wasiomtii.
7 N’ayez donc aucune part avec eux.
Kwa hiyo, msishirikiane nao.
8 Autrefois vous étiez ténèbres, et maintenant vous êtes lumière dans le Seigneur. Marchez comme des enfants de lumière!
Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, lakini sasa ninyi ni nuru katika Bwana. Enendeni kama watoto wa nuru
9 Car le fruit de la lumière consiste en toute sorte de bonté, de justice et de vérité.
(kwa kuwa tunda la nuru hupatikana katika wema wote, haki na kweli),
10 Examinez ce qui est agréable au Seigneur;
nanyi tafuteni yale yanayompendeza Bwana.
11 et ne prenez point part aux œuvres infructueuses des ténèbres, mais plutôt condamnez-les.
Msishiriki matendo ya giza yasiyofaa, bali yafichueni.
12 Car il est honteux de dire ce qu’ils font en secret;
Kwa maana ni aibu hata kutaja mambo yale ambayo wasiotii wanayafanya sirini.
13 mais tout ce qui est condamné est manifesté par la lumière, car tout ce qui est manifesté est lumière.
Lakini kila kitu kilichowekwa nuruni, huonekana,
14 C’est pour cela qu’il est dit: Réveille-toi, toi qui dors, Relève-toi d’entre les morts, Et Christ t’éclairera.
kwa kuwa nuru ndiyo hufanya kila kitu kionekane. Hii ndiyo sababu imesemekana: “Amka, wewe uliyelala, ufufuke kutoka kwa wafu, naye Kristo atakuangazia.”
15 Prenez donc garde de vous conduire avec circonspection, non comme des insensés, mais comme des sages;
Kwa hiyo angalieni sana jinsi mnavyoenenda, si kama watu wasio na hekima, bali kama wenye hekima,
16 rachetez le temps, car les jours sont mauvais.
mkiukomboa wakati, kwa sababu nyakati hizi ni za uovu.
17 C’est pourquoi ne soyez pas inconsidérés, mais comprenez quelle est la volonté du Seigneur.
Kwa hiyo msiwe wajinga, bali mpate kujua nini mapenzi ya Bwana.
18 Ne vous enivrez pas de vin: c’est de la débauche. Soyez, au contraire, remplis de l’Esprit;
Pia msilewe kwa mvinyo, ambamo ndani yake mna upotovu, bali mjazwe Roho.
19 entretenez-vous par des psaumes, par des hymnes, et par des cantiques spirituels, chantant et célébrant de tout votre cœur les louanges du Seigneur;
Msemezane ninyi kwa ninyi kwa zaburi, nyimbo na tenzi za rohoni, mkimwimbia na kumsifu Bwana mioyoni mwenu,
20 rendez continuellement grâces pour toutes choses à Dieu le Père, au nom de notre Seigneur Jésus-Christ,
siku zote mkimshukuru Mungu Baba kwa kila jambo katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
21 vous soumettant les uns aux autres dans la crainte de Christ.
Nyenyekeaneni ninyi kwa ninyi kwa heshima kwa ajili ya Kristo.
22 Femmes, soyez soumises à vos maris, comme au Seigneur;
Ninyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana.
23 car le mari est le chef de la femme, comme Christ est le chef de l’Église, qui est son corps, et dont il est le Sauveur.
Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe kama vile Kristo alivyo kichwa cha Kanisa, ambalo ni mwili wake, naye Kristo ni Mwokozi wake.
24 Or, de même que l’Église est soumise à Christ, les femmes aussi doivent l’être à leurs maris en toutes choses.
Basi, kama vile Kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo na wake nao imewapasa kuwatii waume zao kwa kila jambo.
25 Maris, aimez vos femmes, comme Christ a aimé l’Église, et s’est livré lui-même pour elle,
Ninyi waume, wapendeni wake zenu, kama vile Kristo alivyolipenda Kanisa akajitoa kwa ajili yake
26 afin de la sanctifier par la parole, après l’avoir purifiée par le baptême d’eau,
kusudi alifanye takatifu, akilitakasa kwa kuliosha kwa maji katika Neno lake,
27 afin de faire paraître devant lui cette Église glorieuse, sans tache, ni ride, ni rien de semblable, mais sainte et irrépréhensible.
apate kujiletea Kanisa tukufu lisilo na doa wala kunyanzi au waa lolote, bali takatifu na lisilo na hatia.
28 C’est ainsi que les maris doivent aimer leurs femmes comme leurs propres corps. Celui qui aime sa femme s’aime lui-même.
Vivyo hivyo imewapasa waume kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.
29 Car jamais personne n’a haï sa propre chair; mais il la nourrit et en prend soin, comme Christ le fait pour l’Église,
Hakuna mtu anayeuchukia mwili wake mwenyewe, bali huulisha na kuutunza vizuri, kama Kristo anavyolitunza Kanisa lake.
30 parce que nous sommes membres de son corps.
Sisi tu viungo vya mwili wake.
31 C’est pourquoi l’homme quittera son père et sa mère, et s’attachera à sa femme, et les deux deviendront une seule chair.
“Kwa sababu hii, mwanaume atamwacha baba yake na mama yake, naye ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.”
32 Ce mystère est grand; je dis cela par rapport à Christ et à l’Église.
Siri hii ni kubwa, bali mimi nanena kuhusu Kristo na Kanisa.
33 Du reste, que chacun de vous aime sa femme comme lui-même, et que la femme respecte son mari.
Hata hivyo, kila mmoja wenu ampende mkewe kama anavyoipenda nafsi yake mwenyewe, naye mke lazima amheshimu mumewe.