< 1 Thessaloniciens 5 >

1 Pour ce qui est des temps et des moments, vous n’avez pas besoin, frères, qu’on vous en écrive.
Basi, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira hatuna haja ya kuwaandikia,
2 Car vous savez bien vous-mêmes que le jour du Seigneur viendra comme un voleur dans la nuit.
kwa kuwa mnajua vyema kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajapo usiku.
3 Quand les hommes diront: Paix et sûreté! Alors une ruine soudaine les surprendra, comme les douleurs de l’enfantement surprennent la femme enceinte, et ils n’échapperont point.
Wakati watu wanaposema, “Kuna amani na salama,” maangamizi huwajia ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwanamke mwenye mimba; nao hakika hawatatoroka.
4 Mais vous, frères, vous n’êtes pas dans les ténèbres, pour que ce jour vous surprenne comme un voleur;
Bali ninyi, ndugu, hampo gizani hata siku ile iwakute ghafula kama mwizi.
5 vous êtes tous des enfants de la lumière et des enfants du jour. Nous ne sommes point de la nuit ni des ténèbres.
Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku.
6 Ne dormons donc point comme les autres, mais veillons et soyons sobres.
Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi.
7 Car ceux qui dorment dorment la nuit, et ceux qui s’enivrent s’enivrent la nuit.
Kwa kuwa wote walalao hulala usiku na wale walewao hulewa usiku.
8 Mais nous qui sommes du jour, soyons sobres, ayant revêtu la cuirasse de la foi et de la charité, et ayant pour casque l’espérance du salut.
Lakini kwa kuwa sisi ni wana wa mchana, basi tuwe na kiasi, tukijivika imani na upendo kama dirii kifuani na tumaini letu la wokovu kama chapeo.
9 Car Dieu ne nous a pas destinés à la colère, mais à l’acquisition du salut par notre Seigneur Jésus-Christ,
Kwa maana Mungu hakutuita ili tupate ghadhabu bali tupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
10 qui est mort pour nous, afin que, soit que nous veillions, soit que nous dormions, nous vivions ensemble avec lui.
Yeye alikufa kwa ajili yetu ili hata kama tuko macho au tumelala, tupate kuishi pamoja naye.
11 C’est pourquoi exhortez-vous réciproquement, et édifiez-vous les uns les autres, comme en réalité vous le faites.
Kwa hiyo farijianeni na kujengana, kama vile mnavyofanya sasa.
12 Nous vous prions, frères, d’avoir de la considération pour ceux qui travaillent parmi vous, qui vous dirigent dans le Seigneur, et qui vous exhortent.
Sasa tunawaomba, ndugu, waheshimuni wale wanaofanya kazi kwa bidii miongoni mwenu, wale ambao wana mamlaka juu yenu katika Bwana na ambao wanawaonya.
13 Ayez pour eux beaucoup d’affection, à cause de leur œuvre. Soyez en paix entre vous.
Waheshimuni sana katika upendo kwa ajili ya kazi zao. Ishini kwa amani ninyi kwa ninyi.
14 Nous vous en prions aussi, frères, avertissez ceux qui vivent dans le désordre, consolez ceux qui sont abattus, supportez les faibles, usez de patience envers tous.
Nasi twawasihi, ndugu, waonyeni walio wavivu, watieni moyo waoga, wasaidieni wanyonge na kuwavumilia watu wote.
15 Prenez garde que personne ne rende à autrui le mal pour le mal; mais poursuivez toujours le bien, soit entre vous, soit envers tous.
Angalieni kuwa mtu asimlipe mwenzake maovu kwa maovu, bali siku zote tafuteni kutendeana mema ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.
16 Soyez toujours joyeux.
Furahini siku zote;
17 Priez sans cesse.
ombeni bila kukoma;
18 Rendez grâces en toutes choses, car c’est à votre égard la volonté de Dieu en Jésus-Christ.
shukuruni kwa kila jambo, kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu kwa ajili yenu katika Kristo Yesu.
19 N’éteignez pas l’Esprit.
Msiuzime moto wa Roho Mtakatifu;
20 Ne méprisez pas les prophéties.
msiyadharau maneno ya unabii.
21 Mais examinez toutes choses; retenez ce qui est bon;
Jaribuni kila kitu. Yashikeni yaliyo mema.
22 abstenez-vous de toute espèce de mal.
Jiepusheni na uovu wa kila namna.
23 Que le Dieu de paix vous sanctifie lui-même tout entiers, et que tout votre être, l’esprit, l’âme et le corps, soit conservé irrépréhensible, lors de l’avènement de notre Seigneur Jésus-Christ!
Mungu mwenyewe, Mungu wa amani, awatakase ninyi kabisa. Nanyi mhifadhiwe roho zenu, nafsi zenu na miili yenu, bila kuwa na lawama katika Bwana wetu Yesu Kristo.
24 Celui qui vous a appelés est fidèle, et c’est lui qui le fera.
Yeye aliyewaita ni mwaminifu naye atafanya hayo.
25 Frères, priez pour nous.
Ndugu, tuombeeni.
26 Saluez tous les frères par un saint baiser.
Wasalimuni ndugu wote kwa busu takatifu.
27 Je vous en conjure par le Seigneur, que cette lettre soit lue à tous les frères.
Nawaagizeni mbele za Bwana mhakikishe kuwa ndugu wote wanasomewa barua hii.
28 Que la grâce de notre Seigneur Jésus-Christ soit avec vous!
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Amen.

< 1 Thessaloniciens 5 >