< Sophonie 1 >

1 Parole du Seigneur, qui vint à Sophonie, fils de Chusi, fils de Godolias, fils d'Amorias, fils d'Ézécias, durant les jours de Josias, fils d'Amon, roi de Juda.
Hili ni neno la Yahwe ambalo lilikuja kwa Sefania mwana wa Kushi mwana wa Gedalia mwana wa Amaria mwana Hezekia, katika siku za Yosia mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda. “
2 Que toute chose tombe de défaillance sur la face de la terre, dit le Seigneur.
Nitaangamiza kabisa kila kitu kutoka usoni mwa dunia - hili ni tamko la Bwana mwenyewe.
3 Que l'homme et les bêtes disparaissent; que disparaissent les oiseaux du ciel et les poissons de la mer; et les impies seront sans force, et Je chasserai les pécheurs de la face de la terre, dit le Seigneur.
Nitamwangamiza mtu na mnyama; Nitawaangamiza ndege wa mbinguni na samaki wa baharini, uharibifu pamoja na waovu. Hivyo nitamfutilia mbali mtu kutoka uso wa dunia - hili ni tamko la Bwana mwenyewe.
4 Et J'étendrai Ma main sur Juda et sur les habitants de Jérusalem; et J'effacerai de ce lieu les noms de Baal et de ses prêtres,
Nitafika kwa mkono wangu juu ya Yuda na wote wenyeji wa Yerusalemu. Nitafutilia mbali kila mabaki ya Baali kutoka sehemu hii na majina ya watu waabuduo sanamu miongoni mwa makuhani,
5 et ceux qui adorent sur leurs terrasses l'armée du ciel, et se prosternent en jurant par le Seigneur, et ceux qui jurent par leur roi,
watu ambao juu ya nyumba huabudu miili ya mbinguni, na watu ambao huabudu na kuapa kwa Yahwe bali ambao pia huapa kwa mfalme wao.
6 et ceux qui s'éloignent du Seigneur, et ceux qui ne cherchent pas le Seigneur, et ceux qui ne s'attachent pas au Seigneur.
Nitawafutilia mbali pia wale ambao wamegeuka nyuma kutoka kumfuata Yahwe, wale ambao pia humtafuta Yahwe pasipo kuuliza ulinzi wake.
7 Craignez la face du Seigneur Dieu; car le jour du Seigneur est proche, et le Seigneur a préparé Sa victoire, et Il a sanctifié Ses convives.
Uwe kimya mbele ya Bwana Yahwe! Kwa kuwa siku ya Yahwe ni karibu, Yahwe ameandaa dhabihu na amewatenga wageni wake.
8 Et il arrivera que, le jour du sacrifice du Seigneur, Je tirerai vengeance des princes et de la maison du roi, et de tous ceux qui ont porté des vêtements étrangers.
“Itakuja katika siku ya dhabihu ya Bwana, hivyo nitawapiga wakuu na wana wa mfalme, na kila mmoja aliyevikwa mavazi ya kigeni.
9 Et ce jour-là Je tirerai dans les parvis une vengeance éclatante de ceux qui remplissent d'impiété et de fraude le temple du Seigneur leur Dieu.
Katika siku hiyo nitawapiga wote wale ambao huruka juu ya kizingiti, wale ambao hujaza nyumba ya bwana wao kwa vurugu na udanganyifu.
10 Et ce jour-là, dit le Seigneur, il y aura des cris à la porte des Assaillants, des hurlements à la seconde porte, et de grands brisements de cœur sur les collines.
Itakuwa katika siku ile - hili ni tangazo la Yahwe - kwamba kilio cha huzuni kitakuja kutoka kwenye mlango wa samaki, ikipiga yowe kutoka Wilaya ya Pili, na sauti ya kishindo kikuu kutoka vilimani.
11 Pleurez, vous qui habitez cette ville abattue; car tout le peuple est devenu comme Chanaan, et tous ceux qui se glorifiaient de leur argent ont été exterminés.
Pigeni yowe, wenyeji wa Soko la Wilaya, kwa wote wafanyabiashara watakuwa wameharibiwa, wote wale ambao hupima fedha watakuwa wamefutiliwa mbali.
12 Et en ce jour-là, Je chercherai Jérusalem la lampe à la main, et Je tirerai vengeance des hommes qui méprisent Mes commandements, et qui disent en leur cœur: Le Seigneur ne fera pas de bien, Il ne fera pas de mal.
Itakuwa katika siku ile nitaitafuta Yerusalemu kwa taa na kuwapiga wanaume ambao watakuwa wamekaa kwenye mvinyo wao na kusema mioyoni mwao, 'Yahwe hatafanya chochote, ama kizuri au kiovu.'.
13 Leur richesse sera mise au pillage, et leurs maisons en ruines. Ils se bâtiront des demeures, et ils ne les habiteront pas; ils planteront des vignes, et ils n'en boiront pas le vin.
Mali zao zitakuja kuporwa, na nyumba zao zitakuwa zimetelekezwa kwa maangamizi! Watajenga nyumba lakini hawataishi humo, na kupanda mizabibu lakini hawatakunywa mvinyo wake.
14 Car le grand jour du Seigneur est proche; il est proche, il accourt. Le bruit du jour du Seigneur est lamentable et terrible.
Siku kubwa ya Yahwe ni karibu, karibu na inaharakisha upesi! Sauti ya siku ya Yahwe itakuwa ya kilio cha uchungu wa kishujaa!
15 Le jour de Sa colère est un grand jour; ce jour-là est un jour d'affliction et de calamité; c'est un jour d'angoisse et d'extermination, un jour d'ombre et de ténèbres, un jour de nuages et de vapeurs.
Siku hiyo itakuwa siku ya ghadabu, siku ya huzuni na uchungu, siku ya dhoruba na maangamizi, siku ya giza na utusitusi, siku ya mawingu na giza nene.
16 En ce jour-là, sur les villes fortes et sur les cimes élevées, les cris et les trompettes retentissent.
Itakuwa siku ya parapanda na kengele dhidi ya ngome mijini na buruji ndefu.
17 Et J'écraserai tous les hommes, et ils marcheront comme des aveugles; car ils ont péché contre le Seigneur; et Il répandra leur sang comme la poussière, et leurs chairs comme le fumier.
Hivyo nitaleta dhiki juu ya wanadamu, kwa hiyo watatembea karibu kama wanaume vipofu tangu walipofanya dhambi dhidi ya Yahwe. Damu yao itamwagwa kama vumbi, na sehemu zao za ndani kama kinyesi.
18 Et au jour de la colère du Seigneur, ni leur argent ni leur or ne pourront les sauver; et, dans le feu de Son zèle, toute la terre périra, car Il aura hâte d'exterminer jusqu'au dernier de tous ceux qui l'habitent.
Wala fedha zao wala dhahabu zao hazitaweza kuwaokoa juu ya ghadhabu ya Yahwe. Ndani ya moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa, hivyo ataleta ukamilifu, miwisho wa kutisha kwa wote wakaao duniani.”

< Sophonie 1 >