< Zacharie 14 >
1 Voici que les jours du Seigneur arrivent; et tes dépouilles au milieu de toi vont être partagées.
Siku ya Bwana inakuja ambayo nyara zilizotekwa kwenu zitagawanywa miongoni mwenu.
2 Et Je rassemblerai toutes les nations pour qu'elles combattent contre Jérusalem; et la ville sera prise, et les maisons seront livrées au pillage, et les femmes seront profanées; et la moitié des habitants sera emmenée captive, et le reste de Mon peuple ne sera point massacré dans la ville.
Nitayakusanya mataifa yote huko Yerusalemu kupigana dhidi yake, mji utatekwa, nyumba zitavamiwa na kuporwa na wanawake watanajisiwa. Nusu ya mji watakwenda uhamishoni, lakini watakaobaki hawataondolewa kutoka mjini.
3 Et le Seigneur sortira et Il combattra les gentils, comme Il combat au jour de la bataille.
Kisha Bwana atatoka na kupigana dhidi ya watu wa yale mataifa, kama apiganavyo siku ya vita.
4 Et ce jour-là Ses pieds poseront sur la montagne des Oliviers, vis-à-vis de Jérusalem, du côté de l'Orient. Et la montagne des Oliviers se fendra, moitié vers l'Orient, moitié du côté de la mer; il y aura entre les deux moitiés un immense ravin. Et l'une des deux moitiés s'inclinera au nord, et l'autre au midi.
Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, mashariki mwa Yerusalemu, nao Mlima wa Mizeituni utagawanyika mara mbili kuanzia mashariki hadi magharibi, ukifanya bonde kubwa, nusu ya mlima ukisogea kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini.
5 Et la gorge de Mes montagnes se fermera; et la gorge des montagnes sera resserrée jusqu'à Jasod, et elle sera close comme elle l'a été du temps du tremblement de terre, durant les jours d'Ozias, roi de Juda. Et le Seigneur mon Dieu viendra, et tous Ses saints avec Lui.
Nanyi mtakimbia kupitia katika bonde hilo la mlima wangu kwa kuwa litaenea hadi Aseli. Mtakimbia kama mlivyokimbia tetemeko la ardhi katika siku za Uzia mfalme wa Yuda. Kisha Bwana Mungu wangu atakuja na watakatifu wote pamoja naye.
6 Et voici ce qui arrivera: en ce jour-là il n'y aura point de lumière, mais du froid et de la gelée qui
Siku hiyo hakutakuwepo nuru, baridi wala theluji.
7 dureront tout le jour; et ce jour-là sera connu du Seigneur, et ce ne sera pas le jour, et ce ne sera pas la nuit; et, sur le soir, il y aura une lumière.
Itakuwa siku ya kipekee, isiyo na mchana wala usiku, siku ijulikanayo na Bwana. Jioni inapofika nuru itakuwepo.
8 Et ce jour-là une eau vive sortira de Jérusalem, et la moitié coulera à la première mer, et l'autre moitié à la dernière; et il en sera ainsi pendant le printemps et l'été.
Siku hiyo, maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu, nusu kwenda kwenye bahari ya mashariki, na nusu kwenda kwenye bahari ya magharibi wakati wa kiangazi na wakati wa masika.
9 Et le Seigneur sera roi de toute la terre; et ce jour-là le Seigneur sera le seul Dieu, et Son Nom sera un,
Bwana atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo atakuwepo Bwana mmoja na jina lake litakuwa jina pekee.
10 tout autour de la terre et du désert de Gaza à Remmon, au midi de Jérusalem. Rama subsistera où il est, de la porte de Benjamin à la place de l'ancienne porte, et à la porte des Angles, et de la tour d'Anaméel aussi loin que les pressoirs du roi.
Nchi yote kuanzia Geba, kaskazini mwa Yuda, hadi Rimoni, kusini mwa Yerusalemu, itakuwa kama Araba. Lakini Yerusalemu utainuliwa juu na kubaki mahali pake, toka Lango la Benyamini hadi mahali pa Lango la Kwanza, mpaka kwenye Lango la Pembeni na kutoka Mnara wa Hananeli hadi kwenye mashinikizo ya divai ya mfalme.
11 Jérusalem sera repeuplée; elle ne sera plus frappée d'anathème, et elle sera assise en assurance.
Utakaliwa na watu, kamwe hautaharibiwa tena, Yerusalemu utakaa salama.
12 Et voici le fléau dont le Seigneur frappera tous les peuples qui auront marché contre elle. Leurs chairs se liquéfieront, eux debout sur leurs pieds; leurs yeux s'écouleront hors de leurs orbites, et leur langue se liquéfiera dans leur bouche.
Hii ndiyo tauni ambayo Bwana atapiga nayo mataifa yote ambayo yalipigana dhidi ya Yerusalemu: Nyama ya miili yao itaoza wangali wamesimama kwa miguu yao, macho yao yataoza kwenye matundu yake na ndimi zao zitaoza vinywani mwao.
13 Et ce jour-là voici ce qui arrivera: il y aura contre eux un grand transport du Seigneur; et ils se prendront par la main les uns les autres, et les mains entrelaceront les mains.
Katika siku hiyo Bwana atawatia wanaume hofu kuu. Kila mwanaume atakamata mkono wa mwenzake nao watashambuliana.
14 Et Juda se rangera en bataille contre Jérusalem; et on recueillera les richesses de tous les peuples d'alentour, l'or, l'argent et des vêtements innombrables.
Yuda pia atapigana katika Yerusalemu. Utajiri wa mataifa yote yanayoizunguka Yerusalemu utakusanywa, wingi wa dhahabu, fedha na nguo.
15 Et les chevaux, les mulets, les chameaux, les ânes et toutes les bêtes qui seront dans les camps seront pareillement détruits.
Tauni ya aina iyo hiyo itapiga farasi na nyumbu, ngamia na punda, nao wanyama wote walioko kwenye kambi za adui.
16 Voici ce qui arrivera: les survivants parmi les gentils qui auront marché contre Jérusalem y monteront chaque année pour y adorer le Roi, Seigneur tout-puissant, et pour célébrer la fête des Tabernacles.
Kisha walionusurika katika mataifa yote ambayo yaliushambulia Yerusalemu watakuwa wakipanda Yerusalemu kila mwaka kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote na kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
17 Et voici ce qui arrivera: si de toutes les tribus de la terre on ne monte pas à Jérusalem pour adorer le Roi, Seigneur tout-puissant, ceux qui s'en abstiendront seront pareillement punis.
Ikiwa taifa lolote la dunia hawatakwenda Yerusalemu kumwabudu Mfalme, Bwana Mwenye Nguvu Zote, mvua haitanyesha kwao.
18 Et s'il est une des tribus de l'Égypte qui ne monte pas au temple, les mêmes fléaux l'atteindront; elle sera frappée comme toutes les nations qui ne viendront pas célébrer la fête des Tabernacles.
Ikiwa watu wa Misri nao hawatakwenda kushiriki, hawatapata mvua. Bwana ataleta juu yao tauni ile ambayo itawapiga mataifa yale ambayo hayatakwenda kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
19 Ce sera le péché de l'Égypte, et le péché de toutes mes nations qui ne viendront pas célébrer la fête des tabernacles.
Hii itakuwa adhabu ya Misri na adhabu ya mataifa yote yale ambayo hayatakwenda Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda.
20 Et ce jour-là tout ce qui orne le frein des chevaux sera consacré au Seigneur tout-puissant; les chaudières seront dans le temple du Seigneur comme les coupes devant l'autel.
Katika siku hiyo, kengele zilizofungwa kwenye farasi zitaandikwa maneno haya: Takatifu kwa Bwana, navyo vyungu vya kupikia katika nyumba ya Bwana vitakuwa kama bakuli takatifu mbele ya madhabahu.
21 Et toutes les chaudières de Jérusalem et de Juda seront consacrées au Seigneur tout-puissant. Et tous ceux qui offriront des sacrifices viendront, et ils prendront de ces chaudières, et ils s'en serviront pour faire cuire les victimes; et ce jour-là il n'y aura plus de Chananéens dans la maison du Seigneur tout-puissant.
Kila chungu kilichoko Yerusalemu na Yuda kitakuwa kitakatifu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote na wote wanaokuja kutoa dhabihu watachukua baadhi ya vyungu hivyo na kupikia. Katika siku hiyo hatakuwepo tena mfanyabiashara katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote.