< Zacharie 12 >
1 Parole du Seigneur concernant Israël; ainsi parle le Seigneur qui a tendu le ciel, fondé la terre et formé l'esprit de l'homme en lui
Hili ni tamko la neno la Yahwe kwa Israeli - Bwana asema, azitandaye mbingu na kuweka msingi wa dunia, aiumbaye roho ya mtu ndani yake,
2 Voilà que devant tout le peuple d'alentour Je ferai Jérusalem comme le linteau tremblant d'une porte; et en Judée même on assiégera Jérusalem.
“Tazama, nitaifanya Yerusalemu kuwa kikombe kiwafadhaishacho watu wote wamzungukao. Itakuwa hivyo hivyo pia kwa Yuda wakati wa kuhusuriwa kwa Yerusalemu.
3 Et voici ce qui arrivera: en ce jour Je ferai de Jérusalem une pierre que fouleront aux pieds tous les Gentils. Quiconque marchera sur elle s'en raillera, et toutes les nations de la terre se réuniront contre elle.
Katika siku hiyo, nitaifanya Yerusalemu kuwa jiwe zito kwa watu wa jamaa zote. Kila atakayejaribu kuliinua jiwe hilo atajihumiza sana, na mataifa yote ya dunia yatakusanyika kinyume cha mji huo.
4 En ce jour, dit le Seigneur tout-puissant, Je frapperai de stupeur le cheval, et de démence le cavalier. J'aurai les yeux ouverts sur la maison de Juda, et Je frapperai d'aveuglement les chevaux de tous les peuples.
Katika siku hiyo asema Yahwe - nitampiga kila farasi kwa ushangao na kila mpanda farasi kwa wendawazimu. Nitaiangalia nyumba ya Yuda kwa upendeleo na nami nitawapiga kwa upofu farasi wa majeshi.
5 Et les chefs de mille hommes de Juda diront en leur cœur: Puissions-nous trouver pour nous les habitants de Jérusalem revenus au Seigneur leur Dieu tout-puissant!
Ndipo watawala wa Yuda watakapojisemea mioyoni mwao, 'Wakaao Yerusalemu ndio nguvu yetu kwa sababu ya Yahwe wa majeshi, Mungu wao.'
6 En ce jour Je rendrai les chefs de mille hommes de Juda comme un tison enflammé dans un bûcher, comme une lampe allumée dans la paille; ils dévoreront, à droite et à gauche, tous les peuples d'alentour, et Jérusalem d'elle-même repeuplera encore Jérusalem.
Katika siku hiyo nitawafanya watawala wa Yuda kuwa kama mitungi ya moto katika miti na kama miali ya moto kati ya nafaka isimamayo, kwani utateketeza watu wote walio karibu upande wao wa kulia na kushoto. Yerusalemu atakaa mahali pake tena.
7 Et le Seigneur sauvera les habitants de Juda, comme dans les premiers jours; de telle sorte que l'orgueil de la maison de David et des hommes de Jérusalem ne s'élève point contre Juda.
Yahwe ataziokoa hema za Yuda kwanza, ili kwamba utukufu ya nyumba ya Daudi na utukufu wa wale waishio Yerusalemu hautazidi sehemu iliyosalia ya Yuda.
8 Et voici ce qui arrivera: en ce jour le Seigneur protégera les habitants de Jérusalem; et le faible chez eux sera, en ce jour-là, comme David, et la maison de David, comme la maison de Dieu, comme l'ange du Seigneur devant eux.
Katika siku hiyo Yahwe atakuwa mtetezi wa wakao Yerusalemu, na siku hiyo waliodhaifu miongoni mwao watakuwa kama Daudi, wakati nyumba ya Daudi watakuwa kama Mungu, kama malaika wa Yahwe mbele yao.
9 Et voici ce qui arrivera: en ce jour Je rechercherai pour les anéantir toutes les nations qui auront marché contre Jérusalem.
“Itakuwa kwamba katika siku hiyo nitaanza kuyaharibu mataifa yote yajayo kinyume cha Yerusalemu.
10 Et Je répandrai sur la maison de David et sur Jérusalem un esprit de grâce et de miséricorde; et ils tourneront les yeux vers Moi, parce qu'ils M'auront insulté; et ils se lamenteront sur le peuple, comme sur un enfant bien-aimé; et ils seront pénétrés de douleur, comme sur un fils premier-né.
Lakini nitamwaga roho ya huruma na kuiombea nyumba ya Daudi na wakao Yerusalemu, hivyo wataniangalia mimi, waliomchoma kwa mkuki. Wataniombolezea, kama amwombolezeaye mwana wa pekee; watamwombolezea kwa uchungu sana kama aombolezaye kifo cha mzaliwa wa kwanza.
11 En ce jour les gémissements redoubleront en Jérusalem: tel dans la campagne gémit, sous la hache du bûcheron, un bois de grenadiers.
Katika siku hiyo maombolezo huko Yerusalemu yatakuwa kama maombolezo ya Hadadi Rimoni katika tambarare za Megido.
12 Et la terre gémira famille par famille; la famille de la maison de David, et ses femmes à part; la famille de la maison de Nathan, et ses femmes à part;
Nchi itaomboleza, kila ukoo peke yao. Ukoo wa nyumba ya Daudi utakuwa peke yake na wake zao watakuwa peke yao mbali na wanaume. Ukoo wa nyumba ya Nathani utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume.
13 la famille de la maison de Lévi, et ses femmes à part; la famille de Siméon, et ses femmes à part.
Ukoo wa nyumba ya Lawi utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume. Ukoo wa Washimei utakuwa peke yao na wake zao watakuwa peke yao mbali na waume.
14 Et toutes les autres tribus, et leurs femmes à part.
Kila ukoo uliosalia - kila mmoja utakuwa peke yake na wake watakuwa pekee mbali na waume.