< Zacharie 1 >

1 Le huitième mois de la seconde année; sous Darius; la parole du Seigneur vint à Zacharie; fils de Barachie; fils d'Addo; le prophète; disant:
Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:
2 Le Seigneur a été transporté d'un grand courroux contre vos pères.
“Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani.
3 Et tu diras au peuple: Voici ce que dit le Seigneur tout-puissant: Convertissez-vous à Moi; dit le Seigneur des armées, et Je reviendrai à vous, dit le Seigneur des armées.
Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
4 Et ne soyez pas comme vos pères, à qui les prophètes d'autrefois firent des reproches, disant: Voici ce que dit le Seigneur, Maître de toutes choses: Quittez vos mauvaises voies et vos œuvres criminelles; et ils n'écoutèrent pas, et ils ne s'empressèrent pas de M'obéir, dit le Seigneur.
Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana.
5 Où sont vos pères? Où sont les prophètes? Est-ce qu'ils vivront toujours?
Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele?
6 Accueillez donc Mes paroles et Mes ordonnances, et tout ce que par Mon Esprit J'ai intimé à Mes serviteurs les prophètes, qui ont repris vos pères; or ceux-ci ont répondu, et ont dit: le Seigneur nous a traités selon ce qu'Il avait résolu, et ainsi a-t-Il fait, à cause de nos voies et de nos œuvres.
Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?” “Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’”
7 Le vingt-quatrième jour du onzième mois, celui du Sabbat, la deuxième année du règne de Darius, la parole du Seigneur vint à Zacharie, fils de Barachie, fils d'Addo, le prophète, disant:
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.
8 J'ai eu la nuit une vision. Et voilà qu'un homme était monté sur un cheval fauve, et il se tenait entre des montagnes ombreuses, et il y avait derrière lui des chevaux roux, gris-pommelé, tachetés et blancs.
Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.
9 Et je dis: Qui sont ceux-là, Seigneur? Et l'ange qui parlait avec moi me dit: Je te montrerai ce que c'est.
Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?” Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”
10 Et l'homme qui se tenait debout entre les montagnes, parla, et il me dit: Ceux-là sont ceux que le Seigneur a envoyés pour aller par toute la terre.
Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”
11 Et ils parlèrent à l'ange du Seigneur qui se tenait entre les montagnes, et ils dirent: Nous sommes allés par toute la terre, et voilà que toute la terre est habitée, et elle est en repos.
Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”
12 Et l'ange du Seigneur répondit: Seigneur tout-puissant, dit-il, jusques à quand seras-Tu sans miséricorde pour Jérusalem et pour les villes de Juda, que Tu as délaissées depuis soixante-dix ans?
Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?”
13 Et le Seigneur tout-puissant répondit à l'ange qui parlait avec moi, et lui dit des paroles bonnes et consolantes;
Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.
14 et l'ange qui parlait avec moi me dit: Crie de toute ta force. Voilà ce que dit le Seigneur tout-puissant: Je suis pris d'un grand zèle pour Jérusalem et pour Sion;
Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni,
15 mais J'ai une grande colère contre les gentils qui se sont coalisés; car Me voyant un peu irrité contre elle, ils se sont coalisés pour lui faire du mal.
lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’
16 C'est pourquoi voici ce que dit le Seigneur: Je reviendrai à Jérusalem en Ma miséricorde, et Mon temple y sera réédifié, dit le Seigneur tout-puissant; et il étendra encore le cordeau sur Jérusalem.
“Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
17 Et l'ange qui parlait avec moi ajouta: Crie encore de toute ta force: Voilà ce que dit le Seigneur Tout-Puissant: Leurs villes seront de nouveau remplies de biens, et le Seigneur sera miséricordieux envers Sion, et Jérusalem sera Son élue.
“Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’”
18 Et je levai les yeux, et je regardai, et je vis quatre cornes.
Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne!
19 Et je dis à l'ange qui parlait avec moi: Qu'est cela, Seigneur? Et il me dit: Ce sont les cornes qui ont dispersé Juda, Israël et Jérusalem.
Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?” Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”
20 Et le Seigneur me montra quatre ouvriers.
Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne.
21 Et je dis: Que vont faire ceux-ci? Et Il dit: Voilà les cornes qui ont dispersé Juda et brisé Israël, sans que nul ait levé la tête; or ceux-ci sont venus pour les aiguiser de leurs mains, et les quatre cornes sont les nations qui ont levé la corne contre la terre du Seigneur, pour disperser Mon peuple.
Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?” Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”

< Zacharie 1 >