< Ruth 2 >
1 Il y avait un homme connu de Noémi et de son époux; cet homme, parent d'Elimélech, était riche et il se nommait Booz.
Basi Naomi alikuwa na jamaa wa upande wa mume wake, kutoka ukoo wa Elimeleki, mtu maarufu ambaye aliitwa Boazi.
2 Et Ruth la Moabite dit à Noémi: Je m'en vais aux champs, et je ramasserai des épis à la suite des moissonneurs, chez celui aux yeux de qui je trouverai grâce; et Noémi répondit: Va, ma fille.
Ruthu, Mmoabu, akamwambia Naomi, “Nitakwenda mashambani nikaokote mabaki ya nafaka nyuma ya yule nitakayepata kibali machoni pake.” Naomi akamwambia, “Nenda, binti yangu.”
3 Elle partit donc, et, étant arrivée, elle glana dans un champ, derrière les moissonneurs; elle était, tombée par aventure sur un endroit du champ de Booz, le parent d'Elimélech.
Basi akaenda, akaokota mabaki ya nafaka mashambani nyuma ya wavunaji. Ikatokea kwamba alijikuta anafanya kazi kwenye shamba lililokuwa mali ya Boazi, ambaye alitoka kwenye ukoo wa Elimeleki.
4 Et voilà que Booz vint de Bethléem, et il dit aux moissonneurs: Le Seigneur soit avec vous, et ils lui dirent: Que le Seigneur te bénisse.
Papo hapo Boazi akarudi kutoka Bethlehemu, akawasalimu wavunaji, akasema, “Bwana awe nanyi!” Nao wakamjibu, “Bwana akubariki.”
5 Et Booz dit à son serviteur, qui était placé au-dessus des moissonneurs: Qui est cette jeune fille?
Boazi akamuuliza msimamizi wa wavunaji, “Je, yule mwanamwali ni wa nani?”
6 Son serviteur, qui était placé au-dessus des moissonneurs, répondit: C'est la jeune Moabite, qui est revenue avec Noémi du champ de Moab.
Msimamizi akamjibu, “Ni yule Mmoabu aliyerudi kutoka nchi ya Moabu pamoja na Naomi.
7 Elle m'a dit: le glanerai et je recueillerai des épis derrière les moissonneurs; et elle a glané depuis le matin jusqu'au soir, et elle n'a pas pris dans le champ un moment de repos.
Yeye aliomba, ‘Tafadhali niruhusu niokote na kukusanya miongoni mwa miganda nyuma ya wavunaji.’ Naye ameshinda shambani tangu asubuhi pasipo kupumzika, isipokuwa kwa muda mfupi kivulini.”
8 Alors, Booz dit à Ruth: N'as-tu pas entendu, ma fille? Ne va pas glaner dans un autre champ; ne t'éloigne pas d'ici, et attache-toi aux pas de mes filles.
Kisha Boazi akamwambia Ruthu, “Binti yangu, nisikilize. Usiende kuokota mabaki ya mavuno katika shamba lingine, na usiondoke hapa. Kaa hapa na hawa watumishi wangu wa kike.
9 Les yeux fixés sur le champ où elles moissonnent, tu iras après elles; voilà que j'ai commandé à mes serviteurs de te respecter. Et quand tu auras soif, tu iras aux vaisseaux, et tu boiras où boivent mes serviteurs.
Angalia shamba wanaume wanamovuna, ufuate nyuma yao. Nimewaamuru wanaume hawa wasikuguse. Wakati wowote ukiona kiu, nenda kwenye mitungi ukanywe maji waliyoyateka wanaume hawa.”
10 Et, pour témoigner son respect, elle tomba la face contre terre, et elle lui dit: Comment ai-je trouvé grâce devant tes yeux pour que tu m'honores, moi qui suis une étrangère?
Kwa ajili ya hili, akasujudu mpaka nchi, akamwambia, “Jinsi gani nimepata kibali machoni pako, hata ukanijali mimi mgeni?”
11 Et il répondit: On m'a raconté tout ce que tu as fait pour ta belle mère après la mort de son mari, et comment tu as quitté ton père et ta mère et le lieu de ta naissance, et comment tu es venue chez un peuple qu'auparavant tu ne connaissais pas.
Boazi akamjibu, “Nimeambiwa yote uliyomtendea mama mkwe wako tangu mume wako alipofariki, na jinsi ulivyomwacha baba yako na mama yako na nchi yako ulimozaliwa, ukaja kuishi na watu ambao hukuwafahamu awali.
12 Que le Seigneur rémunère ta bonne action; que le Seigneur Dieu d'Israël, à qui tu es venue pour t'abriter sous ses ailes, t'accorde un salaire abondant.
Bwana na akulipe kwa yale uliyoyatenda. Ubarikiwe kwa wingi na Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye umekimbilia mabawani mwake.”
13 Et elle reprit: Que je trouve, seigneur, grâce devant tes yeux, puisque tu m'as consolée, et que tu as parlé au cœur de ta servante, et je serai comme l'une de tes servantes.
Kisha Ruthu akasema, “Naomba niendelee kupata kibali machoni pako, bwana wangu. Kwa maana umenifariji na umezungumza kwa ukarimu na mjakazi wako, hata ingawa mimi si bora kama mmoja wa watumishi wako wa kike.”
14 Et Booz lui dit: Voici le moment de manger, viens ici; tu mangeras du pain et tu tremperas la bouchée dans le vinaigre. Ruth s'assit donc auprès des moissonneurs, et Booz lui présenta des gâteaux de farine; elle mangea et elle fut rassasiée, et il lui en resta.
Wakati wa chakula, Boazi akamwambia Ruthu, “Karibia hapa. Kula mkate na uchovye ndani ya siki.” Alipoketi pamoja na wavunaji, akampa nafaka zilizookwa. Akala kiasi alichotaka na kusaza.
15 Ensuite, elle se leva, pour glaner, et Booz donna ses ordres à ses serviteurs, disant: Laissez-la glaner au milieu des Javelles et gardez-vous de la molester.
Alipoinuka ili kuokota mabaki ya nafaka, Boazi akawaagiza watu wake, “Hata kama atakusanya kati ya miganda, msimzuie.
16 En apportant les épis, apportez-en pour elle, et en les jetant à terre, jetez pour elle une part de ce que vous recueillez; elle glanera, elle mangera, et vous ne lui ferez aucun reproche.
Badala yake, toeni masuke katika miganda, mwachieni ayaokote, na msimkemee.”
17 Et elle glana jusqu'à la nuit, puis elle battit les épis qu'elle avait ramassés, et elle en tira près d'une mesure d'orge.
Basi Ruthu akaokota masazo shambani hata jioni. Akatwanga ile shayiri aliyokusanya, ikajaa efa moja.
18 Elle l'emporta et elle rentra dans la ville; sa belle-mère vit ce qu'elle avait recueilli, et Ruth lui donna les restes qu'elle avait rapportés des mets dont elle s'était rassasiée.
Akaibeba na kuelekea mjini, naye mama mkwe wake akaona jinsi alivyoweza kuokota nafaka nyingi. Pia Ruthu akachukua kile alichobakiza baada ya kula na kushiba, akampa.
19 Et sa belle-mère lui dit: Où as-tu glané aujourd'hui, où as-tu travaillé? Béni soit celui qui t'a accueillie. Et Ruth apprit à sa belle-mère où elle avait travaillé, et elle lui dit: L'homme chez qui j'ai glané aujourd'hui se nomme Booz.
Basi mkwewe akamuuliza, “Je, umeokota wapi leo? Umefanya kazi wapi? Abarikiwe mtu yule aliyekujali.” Ndipo Ruthu akamwambia mama mkwe wake juu ya yule ambaye yeye alikuwa amefanyia kazi katika shamba lake. Akasema, “Yule mtu niliyefanyia kazi kwake leo, anaitwa Boazi.”
20 Et Noémi dit à sa bru: Béni soit-il, au nom du Seigneur, parce que sa miséricorde n'a manqué ni aux vivants, ni aux morts. Et Noémi ajouta: L'homme nous est proche, c'est un de nos parents.
Naye Naomi akamwambia mkwewe, “Bwana ambariki! Hakuacha kuonyesha fadhili zake kwa walio hai na kwa waliokufa.” Pia akamwambia, “Huyo mtu ni mmoja wa jamaa yetu wa karibu anayestahili kutukomboa.”
21 Et Ruth reprit: C'est sans doute pour cela qu'il m'a dit: Attache-toi aux pas de mes filles jusqu'à ce qu'elles aient achevé toute ma moisson.
Kisha Ruthu, Mmoabu, akasema, “Hata aliniambia, ‘Kaa pamoja na watumishi wangu mpaka watakapomaliza kuvuna nafaka yangu yote.’”
22 Et Noémi dit à Ruth, sa bru: Bon, mon enfant, si tu marches avec ses filles, on ne te contrariera pas dans un autre champ.
Kisha Naomi akamwambia Ruthu mkwewe, “Binti yangu, itakuwa vyema wewe ufuatane na wasichana wake, kwa sababu katika shamba la mtu mwingine wanaweza kukudhuru.”
23 Ruth s'attacha donc aux pas des filles de Booz pour glaner jusqu'à la fin de la moisson des orges et des froments.
Kwa hivyo Ruthu akafuatana na watumishi wa kike wa Boazi, akaokota mpaka mwisho wa mavuno ya shayiri na ya ngano. Naye aliishi na mama mkwe wake.