< Psaumes 81 >
1 Jusqu'à la Fin, psaume d'Asaph, sur les pressoirs. Réjouissez-vous en Dieu notre champion; criez joyeusement vers le Dieu de Jacob.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
2 Prenez un psaume, et faites résonner le tambour, la harpe mélodieuse et la cithare.
Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
3 Sonnez de la trompette à la nouvelle lune, au jour glorieux de notre fête.
Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
4 Car tel est le précepte en Israël, tel est le commandement du Dieu de Jacob.
hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
5 Il a mis ce témoignage en Joseph, quand celui-ci sortit de la terre d'Egypte; il entendit une langue qu'il ne connaissait pas.
Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
6 Il a ôté le fardeau des épaules de son peuple, quand ses mains tressaient des corbeilles, disant:
Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
7 Tu m'as invoqué en ton affliction, et je t'ai délivré; je t'ai entendu dans l'obscurité d'une tempête; je t'ai éprouvé dans l'eau de la contradiction.
Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
8 Ecoute, mon peuple; et je te parlerai, Israël, et je te prendrai à témoin. Si tu m'écoutes,
“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
9 Il n'y aura point chez toi de Dieu nouveau, et tu n'adoreras point de Dieu étranger.
Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
10 Car je suis le Seigneur ton Dieu, qui t'ai tiré de la terre d'Egypte; ouvre la bouche, et je la remplirai.
Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
11 Et mon peuple n'a point écouté ma voix, et Israël n'a point fait attention à moi.
“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
12 Et je les ai fait partir, selon les désirs de leurs cœurs; ils chemineront en leurs désirs.
Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
13 Si mon peuple m'avait écouté, si Israël avait marché dans mes voies,
“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
14 Certes j'eusse humilié jusqu'au néant leurs ennemis; j'eusse mis la main sur leurs oppresseurs.
ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
15 Les ennemis du Seigneur lui ont menti, et il y aura temps pour eux dans l'éternité.
Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
16 Et il les avait nourris de la fleur du froment, et les avait rassasiés du miel des rochers.
Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”