< Psaumes 78 >

1 Psaume de méditation d'Asaph. O mon peuple, attachez-vous à ma loi; inclinez votre oreille vers les paroles de ma bouche.
Utenzi wa Asafu. Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
2 J'ouvrirai ma bouche en paraboles; je dirai les choses qui ont existé dès le commencement,
Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale:
3 Telles que vous les avez ouïes et connues, et que vos pères vous les ont racontées.
yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, yale ambayo baba zetu walituambia.
4 Elles n'ont point été cachées à leurs enfants de la seconde génération, eux-mêmes leur ayant annoncé les louanges du Seigneur, et sa puissance et les merveilles qu'il a faites.
Hatutayaficha kwa watoto wao; tutakiambia kizazi kijacho matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, uweza wake, na maajabu aliyoyafanya.
5 Et il a suscité un témoignage en Jacob, et il a institué en Israël une loi qu'il a confiée à nos pères, pour qu'ils l'enseignassent à leurs enfants,
Aliagiza amri kwa Yakobo na akaweka sheria katika Israeli, ambazo aliwaamuru baba zetu wawafundishe watoto wao,
6 Afin que chaque génération les transmit à la suivante; les fils l'apprendront à ceux qui naîtront d'eux; et ils en porteront témoignage, et ils en instruiront leurs enfants:
ili kizazi kijacho kizijue, pamoja na watoto ambao watazaliwa, nao pia wapate kuwaeleza watoto wao.
7 Afin qu'ils mettent en Dieu leur espérance, et qu'ils n'oublient point ses œuvres, et qu'ils recherchent ses commandements,
Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, nao wasingesahau matendo yake, bali wangalizishika amri zake.
8 Et qu'ils ne soient point comme leurs pères, race perverse et provocatrice, qui n'a pas eu de droiture de cœur, et, en son esprit, n'a pas été fidèle à Dieu.
Ili wasifanane na baba zao, waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, ambao roho zao hazikumwamini.
9 Les fils d'Éphraïm tendant l'arc, lançant des flèches, le jour du combat ont tourné le dos.
Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, walikimbia siku ya vita.
10 Ils n'ont point gardé l'alliance de Dieu, et ils ont refusé de marcher dans sa loi.
Hawakulishika agano la Mungu na walikataa kuishi kwa sheria yake.
11 Et ils ont oublié ses bienfaits, et les miracles qu'il leur a montrés,
Walisahau aliyokuwa ameyatenda, maajabu aliyokuwa amewaonyesha.
12 Et les prodiges qu'il a faits devant leurs pères, en la terre d'Egypte et dans la plaine de Tanis.
Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, huko Soani, katika nchi ya Misri.
13 Il a séparé la mer, et il les a fait passer; il a contenu les eaux, comme dans une outre.
Aliigawanya bahari akawapitisha, alifanya maji yasimame imara kama ukuta.
14 Et il les a guidés le jour dans une nuée, et la nuit dans un luminaire de feu.
Aliwaongoza kwa wingu mchana na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha.
15 Il a fendu le rocher dans le désert, et il les a abreuvés comme avec l'eau d'un grand abîme.
Alipasua miamba jangwani na akawapa maji tele kama bahari,
16 Et de la pierre il a tiré et conduit l'eau comme un fleuve.
alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.
17 Et ils ont continué de pécher contre lui; ils ont provoqué le Très-Haut dans le désert;
Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.
18 Et ils ont tenté Dieu en leurs cœurs, en lui demandant des aliments pour leurs âmes.
Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.
19 Et ils ont parlé contre Dieu, et ils ont dit: Est-ce que Dieu pourra nous préparer une table dans le désert?
Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?
20 Il a frappé le rocher: l'eau a jailli; un torrent a coulé avec abondance. Mais Dieu pourra-t-il nous donner aussi du pain, ou préparer dans le désert une table à son peuple?
Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”
21 C'est pourquoi le Seigneur, les ayant entendus, différa, et un feu fut allumé contre Jacob, et sa colère monta contre Israël;
Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,
22 Parce qu'ils n'avaient pas eu foi en Dieu, et qu'ils n'avaient point espéré en sa protection.
kwa kuwa hawakumwamini Mungu, wala kuutumainia ukombozi wake.
23 Et d'en haut il donna ses ordres aux nues, et il ouvrit les portes du ciel.
Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu na kufungua milango ya mbingu,
24 Et il fit pleuvoir sur eux la manne pour les nourrir, et il leur donna le pain du ciel.
akawanyeshea mana ili watu wale; aliwapa nafaka ya mbinguni.
25 L'homme mangea le pain des anges; Dieu leur envoya des aliments en abondance.
Watu walikula mkate wa malaika, akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula.
26 Il chassa le vent du midi, et par sa puissance il amena le vent de l'occident.
Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake.
27 Et il fit pleuvoir pour eux de la chair comme des nuées de poussière, et des oiseaux emplumés comme le sable des mers.
Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, ndege warukao kama mchanga wa pwani.
28 Et ces oiseaux tombèrent au milieu de leur camp, autour de leurs tentes.
Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, kuzunguka mahema yao yote.
29 Et ils mangèrent, et ils furent rassasiés; et il satisfit leur désir.
Walikula na kusaza, kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani.
30 Rien ne leur manqua de ce qu'ils désiraient, et ils en avaient encore la bouche pleine.
Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao,
31 Et la colère du Seigneur s'éleva contre eux, et il mit à mort leurs riches, et il saisit les élus d'Israël.
hasira ya Mungu ikawaka juu yao, akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, akiwaangusha vijana wa Israeli.
32 Et malgré tout cela ils péchèrent encore, et ne crurent point à ses prodiges.
Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, licha ya maajabu yake, hawakuamini.
33 Et leurs jours défaillirent en vanité, et leurs années se précipitèrent.
Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili na miaka yao katika vitisho.
34 Quand il eut répandu parmi eux la mort, ils cherchèrent le Seigneur, et ils se convertirent à lui, et ils vinrent dès le matin vers Dieu.
Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta, walimgeukia tena kwa shauku.
35 Et ils se souvinrent que Dieu est leur champion, et que Dieu le Très-Haut est leur rédempteur.
Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao.
36 Et ils l'aimèrent de la bouche; mais leur langue lui mentait.
Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, wakisema uongo kwa ndimi zao,
37 Car leur cœur ne fut point droit envers lui, et ils ne furent point fidèles en son alliance.
mioyo yao haikuwa thabiti kwake, wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
38 Et cependant il est miséricordieux, et il leur remettra leurs péchés; et il ne les détruira point. Il détournera souvent sa colère, et son courroux ne s'enflammera pas tout entier.
Hata hivyo alikuwa na huruma, alisamehe maovu yao na hakuwaangamiza. Mara kwa mara alizuia hasira yake, wala hakuchochea ghadhabu yake yote.
39 Et il se souvint qu'ils étaient chair, un souffle qui passe et ne revient plus.
Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, upepo upitao ambao haurudi.
40 Combien de fois l'ont-ils provoqué dans le désert, et l'ont-ils irrité dans la terre sans eau!
Mara ngapi walimwasi jangwani na kumhuzunisha nyikani!
41 Et ils se convertissaient, et ils recommençaient à tenter Dieu, et ils aigrissaient encore le Saint d'Israël.
Walimjaribu Mungu mara kwa mara, wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli.
42 Ils avaient oublié sa main, et le jour où elle les avait tirés des mains de l'oppresseur;
Hawakukumbuka uwezo wake, siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi,
43 Et comment il avait fait ses miracles en Egypte, et ses prodiges dans la plaine de Tanis;
siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, maajabu yake huko Soani.
44 Et comment il avait changé en sang leurs fleuves et leurs pluies, afin qu'ils ne pussent boire;
Aligeuza mito yao kuwa damu, hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao.
45 Et comment il avait envoyé des mouches de chien qui les dévoraient, et des grenouilles qui les détruisaient.
Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, na vyura wakawaharibu.
46 Ils avaient oublié la nielle attachée à leurs fruits, et les sauterelles dont ils avaient souffert,
Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, mazao yao kwa nzige.
47 Et la grêle détruisant leurs vignes, et la gelée faisant périr leurs mûriers,
Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji.
48 Et les grêlons exterminant leur bétail, et le feu consumant leurs richesses,
Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi.
49 Et sa colère et son indignation tombant sur eux; colère, fureur, afflictions, envois d'anges exterminateurs;
Aliwafungulia hasira yake kali, ghadhabu yake, hasira na uadui, na kundi la malaika wa kuharibu.
50 Et la voie ouverte à son courroux, et son dessein de ne point épargner leur vie, et d'enclore leurs troupeaux, dans la mort;
Aliitengenezea njia hasira yake, hakuwaepusha na kifo, bali aliwaachia tauni.
51 Et le coup dont fut frappé tout premier-né en la terre d'Egypte, prémices de leurs peines sous leurs tentes de Cham;
Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.
52 Et le soin qu'il prit d'enlever son peuple comme des brebis, et de les conduire dans le désert, comme un troupeau;
Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani.
53 Et les espérances qu'il leur donna, et les craintes dont il les délivra, et la mer qui couvrit leurs ennemis.
Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, bali bahari iliwameza adui zao.
54 Et il les mena sur la montagne qu'il s'était consacrée, cette montagne que sa droite avait acquise. Et il chassa les nations devant leur face, et il leur distribua, à grandes mesures, la terre de leur héritage.
Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa.
55 Et il établit les tribus d'Israël dans les demeures des vaincus.
Aliyafukuza mataifa mbele yao, na kuwagawia nchi zao kama urithi, aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao.
56 Mais elles tentèrent et provoquèrent Dieu le Très-Haut; elles ne gardèrent point ses témoignages.
Lakini wao walimjaribu Mungu, na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, wala hawakuzishika sheria zake.
57 Et son peuple, se détournant de lui, s'endurcit comme ses pères; il devint comme un arc tortu.
Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, wakawa wasioweza kutegemewa kama upinde wenye kasoro.
58 Et ils provoquèrent la colère de Dieu sur leurs hauts lieux; et ils le rendirent jaloux par leurs images sculptées.
Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, wakachochea wivu wake kwa sanamu zao.
59 Dieu les entendit et les méprisa, et réduisit à néant Israël.
Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, akamkataa Israeli kabisa.
60 Et il répudia le tabernacle de Silo, son tabernacle où il résidait parmi les hommes.
Akaiacha hema ya Shilo, hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu.
61 Et il livra à la captivité leur force, aux ennemis leur beauté.
Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.
62 Et il exposa son peuple au glaive, et il dédaigna son propre héritage.
Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, akaukasirikia sana urithi wake.
63 La flamme dévora leurs jeunes hommes, et leurs vierges ne furent point pleurées.
Moto uliwaangamiza vijana wao, na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64 Leurs prêtres tombèrent sous le glaive, et leurs veuves ne furent point pleurées.
makuhani wao waliuawa kwa upanga, wala wajane wao hawakuweza kulia.
65 Et le Seigneur s'éveilla comme un homme endormi, ou comme un riche après l'ivresse.
Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo.
66 Et il frappa ses ennemis comme ils tournaient le dos, et il les couvrit d'un opprobre éternel.
Aliwapiga na kuwashinda adui zake, akawatia katika aibu ya milele.
67 Et il répudia le tabernacle de Joseph, et il ne choisit point la tribu d'Éphraïm.
Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, hakulichagua kabila la Efraimu,
68 Et il choisit la tribu de Juda, et la montagne de Sion, qu'il a aimée.
lakini alilichagua kabila la Yuda, Mlima Sayuni, ambao aliupenda.
69 Et il bâtit son sanctuaire, fort comme la corne des licornes, en la terre qu'il a fondée pour les siècles des siècles.
Alijenga patakatifu pake kama vilele, kama dunia ambayo aliimarisha milele.
70 Et il choisit David son serviteur, et il le tira de la garde des troupeaux; il le prit tandis qu'il surveillait les brebis mères,
Akamchagua Daudi mtumishi wake na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo.
71 Pour qu'il fût le pasteur de Jacob, son serviteur, et d'Israël, son héritage.
Kutoka kuchunga kondoo alimleta kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, wa Israeli urithi wake.
72 Et David prit soin d'eux en l'innocence de son cœur, et il les mena dans la voie selon l'intelligence de ses mains.
Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.

< Psaumes 78 >