< Psaumes 69 >

1 Jusqu'à la Fin, psaume en répons, de David. Sauves-moi, ô mon Dieu, car les flots sont entrés jusqu'à mon âme.
Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
2 Je suis enfoncé dans un abîme de fange où il n'y a point de fond; je suis plongé dans les profondeurs de la mer, et la tempête m'a submergé.
Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
3 Je me suis fatigué à crier; ma voix s'est enrouée; mes yeux se sont éteints, quand j'ai mis mon espoir en Dieu.
Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
4 Ceux qui me haïssent sans cause sont devenus plus nombreux que les cheveux de ma tête; mes ennemis, ceux qui me persécutent injustement, se sont fortifiés; j'ai payé ce que je n'avais point ravi.
Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
5 O Dieu, tu connais ma folie, et mes fautes ne te sont point cachées.
Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
6 Seigneur, Dieu des armées, que ceux qui t'attendent ne soient point humiliés en moi; ô Dieu d'Israël, que ceux qui te cherchent ne soient point en moi confondus.
Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
7 Car, pour l'amour de toi, j'ai supporté les outrages; la confusion a couvert ma face.
Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
8 Je suis devenu un étranger pour mes frères, un inconnu pour les fils de ma mère.
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
9 Parce que le zèle de ta maison m'a dévoré, et que les injures de ceux qui t'outrageaient sont tombées sur moi.
Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
10 Et j'ai dompté mon âme par le jeûne, et, par là, je me suis attiré des mépris.
Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
11 Et j'ai pris pour vêtement un cilice, et me voilà devenu leur fable.
Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
12 Les hommes assis vers la porte parlaient contre moi, et les buveurs de vin chantaient en me raillant.
Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
13 Et moi dans ma prière à toi, ô Seigneur, je disais: Mon Dieu, le temps de la bienveillance est venu; écoute-moi dans la plénitude de ta miséricorde, sauve-moi par ta vérité!
Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
14 Retire-moi de la fange, afin que je n'y demeure point enfoncé; délivre- moi de mes ennemis et de la profondeur des eaux.
Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
15 Qu'un flot soulevé par la tempête ne me submerge pas; que l'abîme ne m'engloutisse point; que la pierre du puits de l'abîme ne se ferme point sur moi.
Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
16 Exauce-moi, Seigneur, car ta miséricorde est bonne; jette un regard sur moi dans l'abondance de ta compassion.
Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
17 Ne détourne point ton visage de ton serviteur; je suis opprimé, exauce- moi promptement.
Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
18 Considère mon âme et rachète-la; sauve-moi de mes ennemis.
Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
19 Car tu connais leurs injures, et ma honte, et mon humiliation.
Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
20 Tous ceux qui m'affligent sont en ta présence; mon âme s'est résignée aux opprobres et à la misère; j'ai attendu quelqu'un qui fût contristé avec moi, et nul n'est venu; j'ai cherché un consolateur, et je ne l'ai point trouvé.
Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
21 Et ils m'ont donné du fiel pour nourriture, et dans ma soif ils m'ont abreuvé de vinaigre.
Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
22 Que leur table devienne pour eux un piège; qu'elle soit leur punition et leur scandale.
Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
23 Que leurs yeux soient obscurcis et qu'ils ne voient plus; et que leur dos soit perpétuellement courbé.
Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
24 Répands sur eux ton courroux; que le transport de ta colère les saisisse.
Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
25 Que leur maison des champs soit désolée, et que nul n'habite sous leur toit.
Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
26 Parce qu'ils ont persécuté celui que tu as frappé, et qu'ils ont ajouté à la douleur de mes blessures.
Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
27 Impute-leur iniquité sur iniquité; qu'ils n'entrent pas en ta justice!
Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
28 Qu'ils soient effacés du livre des vivants; qu'ils ne soient point inscrits parmi les justes.
Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
29 Pour moi, je suis pauvre et désolé; mais la protection de ta face m'a sauvé.
Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
30 Je louerai dans mes cantiques le nom de mon Dieu; je le glorifierai en mes louanges.
Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
31 Et cela plaira à Dieu, plus qu'un jeune veau montrant des ongles et des cornes.
Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
32 Que les pauvres voient et se réjouissent; cherchez Dieu, et vous vivrez.
Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
33 Car le Seigneur a exaucé les indigents, et jamais n'a méprisé ceux qui sont ses captifs.
Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
34 Qu'il soit loué des cieux, de la terre, de la mer, et de tous les êtres qui se meuvent en eux.
Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
35 Car le Seigneur sauvera Sion, et les villes de la Judée seront édifiées, et des hommes les habiteront, et l'obtiendront pour héritage.
Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
36 Et la postérité de ses serviteurs les possédera, et ceux qui aiment son nom y auront leurs demeures.
Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.

< Psaumes 69 >