< Psaumes 50 >

1 Psaume d'Asaph. Le Dieu des dieux, le Seigneur a parlé, et il a appelé la terre depuis l'Orient jusqu'à l'Occident
Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
2 De Sion vient la splendeur de sa beauté.
Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
3 Dieu, notre Dieu viendra manifestement, et ne gardera pas le silence; un feu sera allume en sa présence, et tout alentour un vent impétueux soufflera.
Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
4 Il convoquera le ciel et la terre, pour juger son peuple.
Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
5 Amenez-lui ses saints, ceux qui ont fait alliance avec lui, pour les sacrifices.
Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
6 Et les cieux annonceront sa justice; car Dieu est le juge.
Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
7 Écoute, mon peuple, et je parlerai; Israël, je te l'atteste: je suis Dieu, je suis ton Dieu.
Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
8 Je ne te réprimanderai point sur tes sacrifices; car tes holocaustes sont toujours devant mes yeux.
Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
9 Je ne prendrai pas de bœufs de ta maison, ni de boucs de tes menus troupeaux.
Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
10 Car toutes les bêtes de la forêt m'appartiennent, et le bétail des montagnes et les taureaux.
Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
11 Je connais tous les oiseaux du ciel, et la beauté des champs est à moi.
Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
12 Si j'ai faim, je ne te le dis pas; car toute la terre habitée m'appartient et sa plénitude.
Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
13 Est-ce que je mange la chair des taureaux? est-ce que je bois le sang des boucs?
Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
14 Immole à Dieu une victime de louanges; rends au Tout-Puissant tes vœux.
Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
15 Invoque-moi au jour de l'affliction, et je te sauverai, et tu me rendras grâces.
Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
16 Mais Dieu a dit au pécheur: Pourquoi publies-tu mes justices et as-tu mon alliance à la bouche,
Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
17 Quand tu n'aimes point ma discipline, et que tu as rejeté loin de toi ma parole?
wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
18 Si tu voyais un larron, tu courais avec lui; tu avais ta part avec les adultères;
Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.
19 Ta bouche abondait en méchanceté, et ta langue tramait la fraude.
Mwautoa mdomo wenu kwa mabaya, huelezea udanganyifu.
20 Assis, tu médisais de ton frère; tu scandalisais le fils de ta mère.
Mnakaa na kuongea dhidi ya ndugu yenu; na kukashfu mwana wa mama yenu.
21 Voilà ce que tu faisais, et j'ai gardé le silence; mais tu t'imaginais faussement que je serais semblable à toi. Je te convaincrai, et je mettrai tes offenses devant ta face.
Mmefanya mambo haya, lakini nimekaa kimya, hivyo mlidhani kuwa ni mtu flani nilliye kama ninyi mlivyo. Lakini nitawakaripia ninyi na kuwafunua, mbele ya macho yenu, mambo yote miliyofanya.
22 Comprenez donc ces choses, vous qui oubliez Dieu; de peur qu'un jour il ne vous ravisse, et que nul ne vous délivre.
Mlitilie maanani hili, ninyi mnao msahau Mungu, vinginevyo nitawakata ninyi vipande vipande, na hatakuwepo yeyote wakuja kuwasaidia!
23 C'est un sacrifice de louange qui m'honore, et la voie où je montrerai le salut de Dieu.
Yule atoaye sadaka ya shukurani hunitukuza, na yeyote apangaye njia zake katika namna iliyo sahihi nitamuonesha wokovu wa Mungu.”

< Psaumes 50 >