< Psaumes 34 >

1 Psaume de David, quand il changea de contenance devant Abimélech, qui le laissa partir, et il partit. En tout temps je bénirai le Seigneur; sa louange sera en tout temps dans ma bouche.
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2 Mon âme se réjouira dans le Seigneur; que les doux écoutent et se réjouissent.
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
3 Glorifiez avec moi le Seigneur, et exaltons son nom tous ensemble.
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4 J'ai cherché le Seigneur, et il m'a exaucé; il m'a tiré de toutes mes afflictions.
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5 Approchez-vous de lui, éclairez-vous de sa lumière, et vos faces ne seront point confondues.
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6 Le pauvre a crié et le Seigneur l'a exaucé, et il l'a délivré de toutes ses afflictions.
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
7 L'ange du Seigneur veillera autour de ceux qui craignent Dieu, et il les sauvera.
Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
8 Goûtez et voyez combien le Seigneur est doux; heureux l'homme qui espère en lui.
Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
9 Craignez le Seigneur, vous tous qui êtes ses saints; car rien ne manque à ceux qui le craignent.
Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
10 Les riches sont devenus pauvres et ils ont eu faim; mais ceux qui cherchent le Seigneur ne manqueront d'aucun bien. Interlude.
Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
11 Venez, enfants, écoutez-moi; je vous enseignerai la crainte du Seigneur.
Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
12 Quel est l'homme qui veut la vie, qui désire voir des jours heureux?
Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
13 Que sa langue s'abstienne du mal, et ses lèvres du mensonge.
basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
14 Détourne-toi du mal, et fais le bien; cherche la paix et la poursuis.
Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
15 Les yeux du Seigneur sont sur les justes, et ses oreilles vers leurs prières.
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16 Le visage du Seigneur est tourné contre ceux qui font le mal, pour effacer de la terre leur souvenir.
Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17 Les justes ont crié, et le Seigneur les a exaucés; et il les a délivrés de toutes leurs afflictions.
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18 Le Seigneur est près de ceux dont le cœur est affligé; il sauvera les humbles d'esprit.
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Les afflictions du juste sont nombreuses, et de toutes le Seigneur le délivrera.
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20 Le Seigneur garde tous leurs os, pas un seul ne sera broyé.
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21 La mort des pécheurs est leur grand malheur, et ceux qui haïssent le juste périront.
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22 Le Seigneur affranchira les âmes de ceux qui le servent, et ceux qui espèrent en lui ne défailliront pas.
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.

< Psaumes 34 >