< Psaumes 30 >
1 Jusqu'à la Fin, psaume et cantique de David à l'occasion de la dédicace de la maison. Je t'exalterai, Seigneur; car tu m'as relevé, tu n'as point fait de moi la joie de mes ennemis.
Utenzi wa kuweka wakfu hekalu. Zaburi ya Daudi. Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu.
2 Seigneur mon Dieu, j'ai crié vers toi, et tu m'as guéri.
Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya.
3 Seigneur, tu as ramené mon âme de l'enfer; tu m'as sauvé d'entre ceux qui descendent dans le sépulcre. (Sheol )
Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. (Sheol )
4 Chantez le Seigneur, vous ses saints; rendez-lui grâces au souvenir de sa sainteté.
Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu.
5 Car la colère naît de son indignation, mais la vie est en sa volonté; le soir, il y aura des pleurs, et à l'aurore l'allégresse.
Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha.
6 Pour moi, j'ai dit en ma prospérité: Je serai à jamais inébranlable.
Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.”
7 Seigneur, ta volonté sainte me maintenait en ma force et ma beauté; tu as détourné de moi ton visage, et j'ai été troublé.
Ee Bwana, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika.
8 Je crierai vers toi, Seigneur; j'adresserai mes prières à mon Dieu.
Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, kwa Bwana niliomba rehema:
9 De quelle utilité te serait mon sang, si je tombais en corruption? Ma cendre te rendrait-elle gloire? ferait-elle connaître ta vérité?
“Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako?
10 Le Seigneur m'a entendu, et il a eu pitié de moi; le Seigneur est devenu mon champion.
Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, Ee Bwana, uwe msaada wangu.”
11 Tu as changé mes lamentations en joie; tu as déchiré mon cilice; tu m'as environné d'allégresse;
Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe,
12 Afin que ma gloire chante tes louanges, et que la douleur ne me transperce plus. Seigneur mon Dieu, je te rendrai éternellement grâces.
ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.