< Psaumes 29 >

1 Un psaume de David, à l'occasion de l'assemblée solennelle du Tabernacle. Apportez au Seigneur, enfants de Dieu, apportez au Seigneur les petits des béliers.
Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
2 Rendez au Seigneur gloire et honneur; glorifiez le nom du Seigneur; adorez le Seigneur en son saint parvis.
Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
3 La voix du Seigneur est sur les eaux; le Dieu de gloire a tonné; le Seigneur est sur les grandes eaux.
Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
4 La voix du Seigneur est puissante; la voix du Seigneur est pleine de magnificence.
Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
5 La voix du Seigneur brise les cèdres; le Seigneur va broyer les cèdres du Liban.
Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
6 Il les brisera comme un jeune taureau du Liban, comme le faon chéri de la licorne.
Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
7 C'est la voix du Seigneur qui divise la flamme et le feu.
Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
8 C'est la voix du Seigneur qui fait trembler le désert; le Seigneur ébranlera le désert de Cadès.
Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
9 C'est la voix du Seigneur qui a préparé la naissance des cerfs; elle découvrira les forêts, et dans le temple du Seigneur chacun dira sa gloire.
Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
10 Le Seigneur répandra sur la terre un déluge; le Seigneur est roi, et il siégera éternellement.
Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
11 Le Seigneur fortifiera son peuple; le Seigneur bénira son peuple en lui donnant la paix.
Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.

< Psaumes 29 >