< Psaumes 114 >

1 Alléluiah! Lorsque Israël sortit d'Egypte, et la maison de Jacob d'un peuple barbare,
Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 Juda devint son peuple saint, Israël sa puissance.
Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
3 La mer le vit, et s'enfuit; le Jourdain retourna en arrière.
Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
4 Les montagnes bondirent comme des béliers, et les collines comme des agneaux.
milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
5 Qu'avais-tu en toi, ô mer, pour fuir ainsi, et toi, Jourdain, pour retourner en arrière?
Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6 Et vous, montagnes, pourquoi bondissiez-vous comme des béliers, et vous, collines, comme des agneaux?
enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 La terre a tremblé à la face du Seigneur, à la face du Dieu de Jacob,
Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
8 Qui a changé la pierre en nappes d'eau, et la roche en fontaines.
aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.

< Psaumes 114 >