< Psaumes 112 >
1 Alléluiah! Heureux l'homme qui craint le Seigneur; il se complaira en ses commandements.
Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
2 Sa postérité sera puissante sur la terre; la génération des justes sera bénie.
Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3 La gloire et la richesse seront en sa demeure, et sa justice durera dans tous les siècles des siècles.
Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
4 La lumière s'est levée dans les ténèbres sur les cœurs droits; le Seigneur est tendre, compatissant et juste.
Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
5 L'homme bon est miséricordieux; il prête au pauvre; il dirigera ses discours avec discernement.
Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
6 Car il ne sera jamais ébranlé.
Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7 La mémoire du juste sera éternelle; il n'aura rien à craindre des discours méchants; son cœur est disposé à espérer dans le Seigneur,
Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8 En lui son cœur est affermi. Il ne craindra point à la vue de ses ennemis.
Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9 Il a distribué et donné ses biens aux pauvres; sa justice demeure dans les siècles des siècles; son front sera élevé en gloire.
Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
10 Le pécheur le verra, et s'en irritera; il grincera des dents, et sera consumé; le désir des pécheurs périra.
Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.