< Psaumes 107 >

1 Alléluiah! Rendez gloire au Seigneur, parce qu'il est bon, parce que sa miséricorde est éternelle.
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 Qu'ainsi disent ceux qui ont été rachetés par le Seigneur, qu'il a délivrés de la main de leurs ennemis et rassemblés des contrées
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 Du levant et du couchant, de la mer et de l'aquilon.
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Ils ont erré dans le désert sans eau; ils n'y ont point trouvé le chemin d'une cité habitable,
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 Et ils avaient faim, ils avaient soif; et leur âme était défaillante.
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 Et, dans leur tribulation, ils crièrent au Seigneur, et il les retira de leur détresse.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7 Et il les conduisit dans le droit chemin, afin qu'ils arrivassent à une cité habitable.
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8 Qu'ils rendent gloire à la miséricorde du Seigneur et à ses prodiges en faveur des fils des hommes;
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 Car il a rassasié leur âme vide, et rempli de biens leur âme affamée.
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 Assis dans les ténèbres et à l'ombre de la mort, ils étaient enchaînés par la pauvreté et le fer;
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 Parce qu'ils avaient provoqué les voix du Seigneur, et avaient irrité le conseil du Très-Haut.
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 Et leur cœur fut humilié dans leurs labeurs, et ils furent sans force, et nul n'était là pour les secourir.
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 Et dans leurs tribulations ils crièrent au Seigneur, et il les retira de leur détresse.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 Et il les tira des ténèbres et de l'ombre de la mort, et brisa leurs chaînes.
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 Qu'ils rendent gloire au Seigneur de sa miséricorde et de ses prodiges en faveur des fils des hommes.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16 Car il a fait voler en éclats les portes d'airain; il a brisé les verrous de fer.
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Il les a aidés à sortir de la voie de leur iniquité; et, à cause de leurs infidélités, ils avaient été humiliés.
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
18 Leur âme avait pris en abomination tout aliment, et déjà ils étaient près des portes de la mort.
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 Et dans leurs tribulations ils crièrent au Seigneur, et il les sauva de leur détresse.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 Et il envoya sa parole, et il les a guéris, et il les arrachés de leur perdition.
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 Qu'ils rendent gloire au Seigneur de sa miséricorde et de ses prodiges en faveur des fils des hommes.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 Et qu'ils lui offrent des oblations de louanges, et qu'ils annoncent ses œuvres avec des transports d'allégresse.
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
23 Ceux qui voguent sur la mer dans leurs barques, et qui trafiquent au milieu des eaux,
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 Ceux-là ont vu les œuvres du Seigneur, et ses merveilles dans l'abîme.
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
25 Il dit, et le vent impétueux de la tempête s'est levé, et les vagues ont bondi.
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 Elles montent jusqu'aux cieux et descendent jusqu'aux abîmes, et l'âme des matelots succombe à la violence du mal.
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
27 Ils sont troublés, ils chancellent comme des hommes ivres, et toute leur sagesse a été engloutie.
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 Et dans leur tribulation ils ont crié au Seigneur, et il les a retirés de leur détresse.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
29 Et il a commandé à la tempête, et elle s'est changée en une brise légère, et les flots ont fait silence.
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 Et les hommes se sont réjouis de leur calme, et le Seigneur les a conduits au port désiré.
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
31 Qu'ils rendent gloire au Seigneur de sa miséricorde et de ses prodiges en faveur des fils des hommes.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
32 Qu'ils l'exaltent dans l'assemblée du peuple, et le louent sur le siège des anciens.
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
33 Il a changé des fleuves en un désert, et des eaux jaillissantes en une terre altérée;
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
34 Et une terre fertile en un lieu saumâtre, à cause de la malice de ceux qui l'habitaient.
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
35 Il a fait d'un désert un étang plein d'eau, et d'une terre sans eau des vallons arrosés.
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 Et il y a mis des affamés, et ils ont bâti des cités habitables.
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 Et ils ont ensemencé des champs, et ils ont planté des vignes, et ils en ont récolté les produits.
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 Et il les a bénis, et ils se sont prodigieusement multipliés, et il n'a pas amoindri le nombre de leur bétail.
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39 Puis ils ont déchu, et ils ont été maltraités par les tribulations, les maux et la douleur.
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 Et le mépris s'est répandu sur leurs princes, et Dieu les a laissés s'égarer en des lieux impraticables et sans voie.
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 Et il a délivré le pauvre de sa misère, et il a traité sa famille comme des brebis.
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 Les justes le verront et en seront réjouis, et toute iniquité fermera sa bouche.
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
43 Quel est le sage qui gardera ces choses, et comprendra les miséricordes du Seigneur?
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.

< Psaumes 107 >