< Psaumes 106 >

1 Alléluiah! Rendez grâces au Seigneur, parce qu'il est bon, parce que sa miséricorde est éternelle.
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
2 Qui dira la puissance du Seigneur, qui fera entendre toutes ses louanges?
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
3 Heureux ceux qui gardent ses jugements et qui font justice en tout temps!
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
4 Souviens-toi de nous, Seigneur, avec ta bonté pour ton peuple; visite- nous avec ton salut;
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
5 Afin que nous puissions avoir part aux biens de tes élus, nous réjouir de la joie de ton peuple, te glorifier avec ceux de ton héritage.
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
6 Nous avons péché avec nos pères, nous avons violé ta loi, nous avons commis l'iniquité.
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
7 Nos pères en Egypte ne comprirent point tes prodiges, et ils ne se souvinrent pas de l'abondance de ta miséricorde; et ils te provoquèrent, en arrivant à la mer Rouge.
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
8 Et il les sauva pour la gloire de son nom, et pour manifester sa puissance.
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
9 Et il menaça la mer Rouge, et elle fut desséchée; et il les ramena dans l'abîme, comme dans le désert.
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
10 Et il les sauva des mains de ceux qui les haïssaient, et il les racheta de la main de l'ennemi.
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
11 L'eau couvrit ceux qui les opprimaient, et pas un d'eux n'échappa.
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
12 Et ils eurent foi en ses paroles, et ils chantèrent ses louanges.
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
13 Mais ils oublièrent bien vite ses œuvres; ils n'attendirent point son conseil.
Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
14 Et ils furent pris de concupiscence dans la solitude, et ils tentèrent Dieu dans le désert sans eau.
Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
15 Et il leur accorda ce qu'ils demandaient, et il envoya la satiété dans leur âme.
Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
16 Et ils irritèrent Moïse dans le camp, et Aaron le saint du Seigneur.
Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
17 La terre s'ouvrit, et elle engloutit Dathan, et engouffra le rassemblement d'Abiron.
Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
18 Et la flamme dévora leur synagogue, et le feu consuma les pécheurs.
Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
19 Et ils se firent un veau en Choreb, et ils adorèrent une image sculptée.
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
20 Et ils échangèrent leur gloire contre la statue d'un veau qui se repaît de fourrage.
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
21 Ils oublièrent le Dieu qui les avait sauvés, qui avait fait de grandes choses en Egypte,
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
22 Des prodiges en la terre de Cham, et des actions terribles sur la mer Rouge.
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
23 Et il dit qu'il les exterminerait, si Moïse, son élu, ne s'était placé devant lui, et n'eût brisé l'idole, pour détourner sa fureur et l'empêcher de les détruire.
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
24 Et ils méprisèrent comme rien la terre désirable, et n'eurent point foi en la parole de Dieu.
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
25 Et ils murmurèrent sous leurs tentes, et n'écoutèrent point la voix du Seigneur!
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
26 Et il leva la main sur eux pour les abattre dans le désert,
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
27 Et pour rejeter leur race parmi les nations, et les disperser en diverses régions.
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
28 Et ils se prostituèrent à Belphégor, et ils mangèrent des victimes sacrifiées aux morts.
Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
29 Et ils irritèrent Dieu par leurs désordres, et la ruine se multiplia chez eux.
Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
30 Et Phinéès se leva, et il apaisa le Seigneur, et la plaie cessa.
Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
31 Et cela lui fut imputé à justice, de génération en génération, dans tous les siècles.
Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
32 Et ils irritèrent Dieu vers les eaux de contradiction, et Moïse eut à souffrir de leur part;
Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
33 Parce qu'ils avaient rempli son esprit d'une amertume qui s'échappa de ses lèvres.
kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
34 Ils n'exterminèrent point les nations, comme le Seigneur le leur avait dit;
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
35 Et ils se mêlèrent aux Gentils, et ils apprirent leurs œuvres,
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
36 Et ils servirent leurs idoles, et ce fut pour eux un sujet de chute.
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
37 Et ils sacrifièrent aux démons leurs fils et leurs filles.
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
38 Et ils versèrent le sang innocent, le sang de leurs fils et de leurs filles, qu'ils immolèrent aux sculptures de Chanaan. Et la terre fut pleine de carnage et de sang.
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
39 Et elle fut souillée par leurs œuvres; et ils se prostituèrent en leurs passions.
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
40 Et le Seigneur s'enflamma de colère contre son peuple, et il eut en abomination son héritage.
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
41 Et il les livra aux mains de leurs ennemis, et ceux qui les haïssaient devinrent leurs maîtres.
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
42 Et leurs ennemis les opprimèrent, et ils furent humiliés sous leurs mains.
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
43 Souvent Dieu les sauva; mais ils l'irritèrent encore en leurs conseils, et ils furent humiliés dans leurs iniquités.
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
44 Et le Seigneur les vit en leurs tribulations, et il écouta leur prière.
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
45 Et il se souvint de son alliance, et il se repentit en la plénitude de sa miséricorde.
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
46 Et il leur accorda ses miséricordes, en face de ceux qui les retenaient captifs.
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
47 Sauve-nous, Seigneur notre Dieu, et rassemble-nous du milieu des Gentils, pour que nous proclamions ton saint nom et que nous mettions notre gloire à te louer.
Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
48 Béni soit le Seigneur, Dieu d'Israël, dans tous les siècles des siècles, et tout le peuple dira: Ainsi soit-il! Ainsi soit-il!
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.

< Psaumes 106 >