< Proverbes 13 >
1 Le fils habile obéit à son père; le fils indocile marche à sa perte.
Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
2 L'homme bon se nourrit des fruits de la justice; les âmes des pécheurs périront avant le temps.
Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
3 Veiller sur sa bouche, c'est garder son âme; avoir les lèvres téméraires, c'est se préparer des sujets de crainte.
Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
4 L'oisif est toujours dans les regrets; les mains de l'homme fort sont diligentes.
Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
5 Le juste hait les paroles injustes; l'impie sera confondu, et n'aura pas la liberté.
Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
6 La justice protège les hommes intègres, mais l'impiété entraîne les méchants dans le péché.
Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
7 Les uns se donnent pour riches, et n'ont rien; et d'autres se font humbles avec une grande richesse.
Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
8 La richesse d'un homme est la rançon de sa vie; le pauvre ne réside pas à une menace.
Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
9 La lumière brille perpétuellement sur les justes; la lumière des impies s'éteint. Les âmes artificieuses s'égarent dans le péché, tandis que les justes sont compatissants et miséricordieux.
Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
10 Le méchant fait le mal avec orgueil; pouvoir se juger soi-même, c'est être sage.
Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
11 La richesse rapidement acquise par le péché décroît; celui qui amasse avec piété s'enrichira. le juste est compatissant, et il prête au pauvre.
Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
12 Mieux vaut d'abord aider de bon cœur que promettre et donner de l'espérance. Un bon désir est un arbre de vie.
Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
13 Celui qui dédaigne une affaire sera dédaigné par elle; celui qui vénère les commandements aura la santé de l'âme. Au fils artificieux il n'arrivera rien de bon; au serviteur sage toute chose réussira; et sa voie sera constamment droite.
Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
14 La loi du sage est une source de vie; l'insensé mourra pris au piège.
Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
15 Un bon discernement attire la grâce; connaître la loi est d'une saine intelligence; la mépriser, c'est suivre une voie de perdition.
Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
16 Tout homme habile sait ce qu'il fait; l'insensé déploie sur lui-même le malheur.
Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
17 Un roi téméraire tombera dans l'adversité; un sage ministre le sauvera.
Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
18 La discipline éloigne la pauvreté et le déshonneur; celui qui est attentif aux réprimandes sera glorifié.
Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
19 Les désirs des hommes pieux charment l'âme; les œuvres des impies sont loin de la doctrine.
Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
20 En marchant avec les sages, tu seras sage; celui qui marche avec les insensés se fera bientôt reconnaître.
Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
21 Les calamités poursuivront les pécheurs; les justes sont maîtres de tous les biens.
Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
22 L'homme bon laissera pour héritiers les fils de ses fils; les richesses des impies sont des trésors pour les justes.
Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
23 Les justes passeront beaucoup d'années dans la richesse; les injustes périront rapidement.
Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
24 Celui qui épargne le bâton n'aime pas son fils; celui qui l'aime le châtie à propos.
Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
25 Le juste en mangeant rassasie son âme; les âmes des impies sont toujours à jeun.
Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.