< Proverbes 11 >
1 Les balances fausses sont en abomination au Seigneur; le poids juste Lui est agréable.
Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
2 Où est l'orgueil, il y aura confusion; la bouche des humbles s'exercent à la sagesse.
Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
3 Le juste en mourant laisse des regrets; la mort des impies cause l'indifférence ou la joie.
Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
5 L'équité trace des voies irréprochables; l'impiété trébuche contre l'injustice.
Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
6 L'équité des hommes droits les sauve; les pervers sont pris dans leur propre perdition.
Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
7 L'espérance des justes ne meurt pas avec eux; l'orgueil des impies ne leur survit point.
Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
8 Le juste échappe aux chasseurs d'hommes; à sa place, l'impie leur est livré.
Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
9 La bouche de l'impie tend un piège aux citoyens; l'intelligence du juste les guide dans la bonne voie.
Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
10 Grâce aux justes, une cité prospère;
Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
11 au contraire, elle est renversée par la bouche des impies.
Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
12 L'insensé se joue des citoyens; un homme prudent ramène le calme.
Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
13 L'homme à la langue double divulgue les conseils de l'assemblée; l'homme fidèle garde le secret sur les affaires.
Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
14 Ceux qui n'ont point de gouvernail tombent comme des feuilles. Le salut réside dans une grande puissance.
Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
15 Le méchant fait le mal, même quand il se rapproche du juste; il n'aime pas son renom de fermeté.
Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
16 La femme gracieuse fait la gloire de son mari; la femme qui hait la justice est un trône de déshonneur. Les paresseux manquent de richesses; les forts travaillent à en amasser.
Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
17 L'homme charitable fait du bien à son âme; l'homme sans pitié perd son corps.
Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
18 L'impie fait des œuvres iniques; la race des justes recueille la récompense de la vérité.
Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
19 Un fils juste est né pour la vie; ce que poursuit l'impie mène à la mort.
Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
20 Les voies tortueuses sont en abomination au Seigneur; mais Il agrée tous ceux qui sont irréprochables dans leurs voies.
Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
21 Celui qui, dans une pensée injuste, met sa main dans la main d'autrui ne sera point impuni; au contraire, qui sème la justice en récoltera le digne salaire.
Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
22 Tel est un pendant d'oreille au museau d'une truie; telle est la beauté chez la femme sans sagesse.
Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
23 Le désir du juste est bon sans réserve; l'espérance des impies périra.
Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
24 Il en est qui, en distribuant leurs biens, les augmentent; il en est qui, même en s'amusant, s'appauvrissent.
Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
25 Toute âme simple est bénie; l'homme irascible n'est pas honoré.
Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
26 Que celui qui amasse du blé le tienne en réserve pour les peuples; la bénédiction est sur la tête de celui qui en fait part à autrui.
Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
27 Celui qui médite le bien cherche une grâce salutaire; celui qui songe au mal le recueillera pour lui-même.
Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
28 Celui qui se fie en sa richesse tombera; celui qui s'attache aux choses justes fleurira.
Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
29 Celui qui ne s'occupe pas de sa propre maison n'aura que le vent pour héritage; l'insensé sera le serviteur du sage.
Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
30 Du fruit de la justice naît l'arbre de vie; les âmes des pervers seront emportées avant le temps.
Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
31 Si le juste est difficilement sauvé, que penser de l'impie et du pécheur?
Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?