< Proverbes 10 >
1 Le fils sage réjouit son père; le fils insensé est le chagrin de sa mère.
Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
2 Les trésors ne serviront de rien aux pervers; mais l'équité délivrera de la mort.
Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
3 Le Seigneur ne laissera pas mourir de faim l'âme du juste; mais Il détruira la vie des impies.
Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
4 L'indigence abaisse l'homme; mais des mains fortes enrichissent. Le fils bien enseigné sera sage, et il se fera servir par l'insensé.
Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
5 Le fils prudent n'a point à souffrir de la grande chaleur; mais le fils pervers est un épi consumé par le vent pendant la moisson.
Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
6 La bénédiction du Seigneur est sur la tête du juste; mais des deuils imprévus couvrent la tête des impies.
Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
7 La mémoire des justes a la louange pour elle; mais le nom des impies s'éteint.
Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
8 Le sage recueille les commandements en son cœur; mais l'homme aux lèvres indiscrètes prend des détours et trébuche.
Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
9 Celui qui marche en sa simplicité, marche avec confiance; celui qui se détourne dans ses voies sera découvert.
Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
10 Celui qui approuve d'un regard rusé prépare toute sorte de chagrins aux hommes; mais celui qui réprimande avec franchise est un pacificateur.
Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
11 Il y a une source de vie dans la main du juste; mais la perdition est cachée dans la bouche des impies.
Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
12 La haine suscite la discorde; l'amitié protège tous ceux qui n'aiment point les querelles.
Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
13 Celui dont les lèvres professent la sagesse frappe d'une verge l'homme privé de sens.
Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
14 Les sages cachent leur science; mais la bouche du téméraire le conduit à la confusion.
Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
15 La fortune des riches est leur forteresse, et la pauvreté est pour les impies le brisement du cœur.
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
16 Les œuvres des justes donnent la vie; mais les fruits des impies sont autant de péchés.
Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
17 L'instruction garde droites les voies de la vie; mais l'instruction superficielle égare.
Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
18 Les paroles bien mesurées recèlent la haine; mais ceux qui se répandent en injures sont des plus insensés.
Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
19 Par la multitude des paroles, tu n'éviteras pas le péché; par la discrétion des lèvres, tu seras sage.
Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
20 La langue du juste est de l'argent pur; mais le cœur de l'impie est sans valeur.
Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
21 Les lèvres des justes savent des vérités sublimes; les insensés meurent dans l'indigence.
Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
22 La bénédiction du Seigneur est sur la tête du juste; elle l'enrichit, et il ne s'y joindra aucune tristesse de cœur.
Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
23 L'insensé fait le mal en riant; la sagesse de l'homme enfante la prudence.
Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
24 L'impie est emporté dans sa perdition; mais le désir du juste est exaucé.
Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
25 Comme la tempête passe, ainsi l'impie disparaît; le juste s'en détourne, et il est sauvé pour tous les siècles.
Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
26 Comme le fruit vert nuit aux dents et la fumée aux yeux, de même l'iniquité nuit aux injustes.
Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 La crainte du Seigneur multiplie les jours; mais les années des impies sont abrégées.
Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
28 La joie du juste est durable; l'espérance des impies périra.
Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
29 La crainte du Seigneur est la forteresse du saint; mais l'affection vient à ceux qui font le mal.
Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
30 Le juste ne se relâchera jamais; mais les impies n'habiteront pas la terre.
Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
31 La bouche du juste distille la sagesse; la langue des impies périra.
Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
32 Les lèvres du juste distillent la grâce; la bouche des impies, la perversité.
Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.