< Nombres 34 >
1 Et le Seigneur parla à Moïse, disant:
BWANA akanena na Musa akasema,
2 Donne mes ordres aux fils d'Israël, et dis-leur: Vous allez entrer en la terre de Chanaan; cette terre, avec ses limites, vous appartiendra comme héritage.
“Waamuru watu wa Israeli na uwaambie, 'Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani, nchi ambayo itakuwa mali yenu, nchi ya Kanaani na mipaka yake, mpaka wenu wa kusini utaendelea kutoka nyika ya Sini hadi mpaka wa Edomu.
3 Au midi, vous la possèderez depuis le désert jusqu'au territoire d'Edom; de ce côté, la limite sera d'abord le rivage oriental de la mer Salée.
Mwisho wa mpaka wa kusini utakuwa mwisho wa bahari ya chumvi kuelekea mashariki.
4 Vos limites au midi tourneront autour de la montée d'Acrabin; elles traverseront Ennac (Senna), et elles descendront au delà de Cadès-Barné; puis, elles sortiront du village d'Arad, et elles passeront par Asémona.
Mpaka wenu utageukia kusini kutoka mlima kuelekea Akrabimu na kupitia nyika ya Sini. na kutokea huko utaelelkea kusini mwa Kadeshi Barinea na kuelekea Hazari Adari mpaka Azimoni.
5 A partir d'Asémona, elles suivront les contours du torrent d'Egypte, et finiront à la mer.
Kutoka huko, mpaka utageuka kutoka Azimoni kuelekea kijito cha Misri na kukifuata mpaka baharini.
6 Ensuite, vous aurez pour limites la mer, la grande mer vous limitera; ce sera la frontière occidentale.
Mpaka wa Magharibi utakuwa pwani ya bahari kuu. Huu ndio utakuwa mpaka wenuwa Magharibi.
7 Au nord, voici quelle sera votre limite: à partir de la mer, vous mesurerez pour vous la montagne, le long de la montagne.
Mpaka wenu wa kaskazini utaanzia kwenye bahari kuu hadi Mlima Hori,
8 Et vous mesurerez pour vous de montagne en montagne; votre frontière, après être entrée dans Emath, ira jusqu'à Saradac (Sadada).
kisha kutoka Mlima Hori hadi Lebo Hamathi, kisha Zedadi.
9 Ensuite, elle sortira de Déphron (Zéphronie), et finira en Arsenaïn (Enan): telle sera votre frontière du nord.
Mpaka utaendelea hadi Zifroni na kuishia Hazari Enani. Huu ndio utakuwa mpaka wenu wa kaskazini.
10 Et tous mesurerez votre frontière orientale d'Arsenaïn à Séphama;
Kisha mtaweka alama za mpaka wenu wa mashariki ambao utaanzia Hazari Enani kuelekea kusini Shefamu.
11 Elle descendra de Séphama en Béla (Rébla), au delà des frontières, et de Béla à l'extrémité de la rive orientale de la mer de Cénéreth (Génésareth).
Kisha mpaka wa kusini utaendelea kutoka Shefamu hadi Ribla, upande wa masharikia mwa Aini. Mpaka utaedelea upande huo wa mashariki hadi upande wa mashariki wa bahari ya Kinerethi.
12 Puis, elle suivra le cours du Jourdain, et elle finira par la mer Salée: telle sera votre terre, telles seront ses limites tout alentour.
Kisha mpaka utaendelea kuelekea kusini hadi mto Yorodani na hadi bahari ya chumvi. Hii ndiyo itakuwa nchi yenu, kwa kuifuata mipaka yake yote inayozunguka.'”
13 Moïse donna donc cet ordre aux fils d'Israël, disant: Voici la terre que vous vous partagerez au sort, comme l'a prescrit le Seigneur, pour la distribuer aux neuf tribus et à la demi-tribu de Manassé.
Kisha Musa akawaamuru watu wa Israeli akasema, “Hii ndiyo nchi ambayo mtaipokes kwa kura, ambayo BWANA ameamuru kuwapa wale makabila tisa na nusu.
14 Car les fils de Ruben, les fils de Gad, par familles paternelles, et une demi-tribu de Manassé, ont reçu leurs parts.
Kabila ya uzao wa Reubeni, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na uzao wa kabila la Gadi, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na nusu ya Manase wamepata ardhi yao.
15 Deux tribus et une demi-tribu ont pris leur part, vis-à-vis Jéricho, sur la rive orientale du Jourdain, au sud-est
Wale makabila mawili na nusu wameshapata mgawo wao ng'ambo ya mto Yorodani upande wa mashariki, kuelekea kule linakotokea jua.”
16 Et le Seigneur parla à Moïse, disant:
BWANA akanena na Musa akasema,
17 Voici les noms des hommes qui procèderont au partage de la terre: Eléazar le prêtre, et Josué, fils de Nau.
“Haya ndiyo majinaya watu watakaoigawa ardhi kwa ajili ya urithi wao: Eliazari kuhani na Joshua mwana wa Nuni.
18 Et vous prendrez par tribu un prince qui tirera au sort la part de la tribu.
Mtachagua kiongozi mmoja toka kila kabila ili kuigawa ardhi kwa koo zao.
19 Voici les noms de ces princes, pour la tribu de Juda: Caleb, fils de Jéphoné.
Haya ndiyo majina ya wanaume: Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.
20 Pour la tribu de Siméon: Samuel, fils d'Ammiud.
Kutoka kwenye kabila la uzao wa Simeoni, Shemueli mwana wa Amihudi.
21 Pour la tribu de Benjamin: Elidad, fils de Chaselon.
Kutoka kabila la Benjamini, Elidadi mwana wa Kisloni.
22 Pour la tribu de Dan: Bocchi, fils de Jogli.
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Dani, Buki mwana wa Jogili.
23 Pour les fils de Joseph, de la tribu de Manassé: Hanniel, fils d'Ephod;
Kiongozi kutoka uzao wa Yusufu, kwenye kabila la Manase, Hannieli mwana wa Efodi.
24 Pour la tribu d'Ephraïm: Camuel, fils de Sephthan;
Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Efraimu, Kemueli mwana wa Shiftani.
25 Pour la tribu de Zabulon: Elisaphan, fils de Pharnach.
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Zabuloni, Elizafani mwana wa Parinaki.
26 Pour la tribu d'Issachar: Phaltiel, fils d'Ozan.
Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Isakari, Palitieli mwana wa Azzani.
27 Pour la tribu d'Aser: Ahiud, fils de Salomi.
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Asheri, Ahihudi mwana wa Shelomi.
28 Et pour la tribu de Nephthali: Phédaël, fils d'Ammiudi
Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Naftali, Pedaheli mwana wa Amihudi.”
29 Tels furent ceux à qui le Seigneur ordonna de faire les parts des fils d'Israël, en la terre de Chanaan.
BWANA aliwaamuru wanaume hawa kuigawa nchi ya Kanaani na kuwapa kila kabla sehemu yao.