< Nombres 33 >
1 Voici les stations des fils d'Israël, après que Moïse et Aaron les eurent fait sortir d'Egypte.
Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
2 Par les ordres du Seigneur, Moïse écrivit leurs départs et leurs campements. Or, voici ces stations:
Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
3 Ils partirent de Rhamessès le premier mois, le quinzième jour de la lune; le lendemain de la pâque, les fils d'Israël partirent sous une haute et puissante main, devant tous les fils de l'Egypte.
Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
4 Les Egyptiens ensevelirent chez eux tous les morts qu'avait frappés le Seigneur, tous les premiers-nés de la terre d'Egypte, et le Seigneur tira vengeance de leurs dieux.
Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
5 Partis de Rhamessès, les fils d'Israël campèrent en Soccoth.
Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
6 Partis de Soccoth, ils campèrent à Etham (Othom), qui est à l'extrémité du désert.
Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
7 Ils partirent d'Etham, et campèrent vers le golfe de Phihahiroth, qui est en face de Béelséphon, et ils étaient campés vis-à-vis Magdole.
Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
8 Partis de Phihahiroth, ils passèrent au milieu de la mer Rouge pour gagner le désert, et ils firent trois journées de marche dans le désert, et ils campèrent à Mara.
Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
9 Ils quittèrent Mara, et vinrent en Elim. Or, il y avait à Elim douze fontaines et soixante-dix tiges de palmiers; ils campèrent en ce lieu, à cause de l'eau.
Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
10 Puis, ils partirent d'Elim, et ils campèrent au bord de la mer Rouge.
Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
11 Et ils partirent de la mer Rouge, et ils campèrent dans le désert de Sin.
Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
12 Partis du désert de Sin, ils vinrent camper en Daphca.
Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
13 Et ils partirent de Daphca, et ils campèrent en Alus.
Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
14 Et ils partirent d'Alus, et ils campèrent à Rhaphidin; or, il n'y avait point là de l'eau pour que le peuple put boire.
Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
15 Ayant quitte Rhaphidin, ils dressèrent leurs tentes dans le désert de Sina.
Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
16 Du désert de Sina, ils vinrent camper aux Sépulcres de concupiscence.
Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
17 Ils s'éloignèrent des Sépulcres de concupiscence, et campèrent à Haseroth.
Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
18 Partis d'Haseroth, ils allèrent camper à Rethma.
Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
19 De Rethma, ils vinrent camper en Rhemmompharès.
Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
20 Ils partirent de Rhemmompharès, et ils campèrent en Lebna.
Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
21 Partis de Lebna, ils campèrent en Ressa.
Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
22 De Ressa, ils vinrent dresser leurs tentes en Céélatha.
Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
23 Et ils partirent de Céélatha, pour aller camper à Sépher.
Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 Ayant quitté Sépher, ils campèrent en Arada.
Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
25 Ils partirent d'Arada, et campèrent en Maceloth.
Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
26 De Maceloth, ils dressèrent leurs tentes en Thabath.
Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
27 Et ils partirent de Thabath, pour venir camper à Tharé.
Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
28 Partis de Tharé, ils campèrent à Methca.
Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
29 De Methca, ils vinrent camper à Hesmona.
Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
30 Et ils partirent de Hesmona, pour aller camper à Moserotb.
Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
31 Ayant quitté Moseroth, ils campèrent à Béné-Jaacan.
Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
32 Partis de Béné-Jaacan, ils vinrent camper en la montagne de Gadgad.
Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
33 De la montagne de Gadgad, ils vinrent camper à Jétébatba.
Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
34 Et ils partirent de Jétébatba, pour aller dresser leurs tentes en Hébrona.
Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
35 Puis, ayant quitté Hebrona, ils campèrent en Asion-Gaber.
Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
36 Partis d'Asion-Gaber, ils vinrent camper dans le désert de Sin, d'où, étant sortis, ils campèrent dans le désert de Pharan qui est Cadès.
Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
37 Partis de Cadès-Barné, ils vinrent camper sur la montagne de Hor, près de la terre d'Edom.
Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
38 Et Aaron monta sur la montagne par ordre du Seigneur, et il y mourut, en la quarantième année de la sortie d'Egypte, le cinquième mois, le premier de la lune.
Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
39 Aaron avait cent vingt-trois ans lorsqu'il mourut sur la montagne de Hor.
Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
40 Et, le Chananéen, roi d'Arad, qui demeurait en la terre de Chanaan, apprit que les fils d'Israël étaient en marche.
Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
41 Ils partirent ensuite de la montagne de Hor, et vinrent camper en Salmona.
Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
42 Ayant quitté Salmona, ils campèrent en Phunon.
Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
43 Partis de Phunon, ils dressèrent leurs tentes à Oboth.
Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
44 Puis, ils s'éloignèrent d'Obotb, pour venir camper à Gié-Abarim, au delà et près des frontières de Moab.
Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 Et ils partirent de Gié-Abarim, pour séjourner à Dibon-Gad.
Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
46 De Dibon-Gad, ils vinrent camper à Helmon-Déblathaïm.
Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
47 Partis de Helmon-Déblathaïm, ils campèrent sur les montagnes d'Abarim, en face de Nébo.
Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
48 Ayant quitté les montagnes d'Abarim, ils campèrent à l'Occident de Moab, sur le Jourdain, en face de Jéricho.
Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
49 Ensuite, ils campèrent aux bords du Jourdain de Beth-Simoth, à Abelsatim, à l'occident de Moab.
Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
50 Et le Seigneur parla à Moïse, à l'occident de Moab, sur le Jourdain, en face de Jéricho, et il lui dit:
Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
51 Parle aux fils d'Israël, et dis-leur: Vous allez traverser le Jourdain pour entrer en la terre de Chanaan.
“Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
52 Et, devant vous, vous exterminerez tous ceux qui habitent cette terre; vous détruirez leurs tours, leurs idoles jetées en fonte, et leurs colonnes.
ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
53 Vous détruirez tous les peuples de la terre promise, et vous l'habiterez; car je vous la donne pour héritage.
Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
54 Vous la partagerez entre vos tribus; donnant plus aux plus nombreux, et moins aux moindres en nombre. Quelle que soit la part qu'à chacun désignera le sort, chacun la possèdera; le partage se fera par tribus paternelles.
Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
55 Mais, si vous n'exterminez pas devant vous tous les habitants de la terre, ceux que vous aurez épargnés seront des traits en vos yeux, des flèches en vos flancs; ils seront vos ennemis sur la terre que vous habiterez.
Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
56 Et alors, je vous traiterai vous-mêmes comme j'avais résolu de les traiter.
Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”