< Nombres 33 >

1 Voici les stations des fils d'Israël, après que Moïse et Aaron les eurent fait sortir d'Egypte.
Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
2 Par les ordres du Seigneur, Moïse écrivit leurs départs et leurs campements. Or, voici ces stations:
Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
3 Ils partirent de Rhamessès le premier mois, le quinzième jour de la lune; le lendemain de la pâque, les fils d'Israël partirent sous une haute et puissante main, devant tous les fils de l'Egypte.
Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
4 Les Egyptiens ensevelirent chez eux tous les morts qu'avait frappés le Seigneur, tous les premiers-nés de la terre d'Egypte, et le Seigneur tira vengeance de leurs dieux.
waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
5 Partis de Rhamessès, les fils d'Israël campèrent en Soccoth.
Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
6 Partis de Soccoth, ils campèrent à Etham (Othom), qui est à l'extrémité du désert.
Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
7 Ils partirent d'Etham, et campèrent vers le golfe de Phihahiroth, qui est en face de Béelséphon, et ils étaient campés vis-à-vis Magdole.
Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
8 Partis de Phihahiroth, ils passèrent au milieu de la mer Rouge pour gagner le désert, et ils firent trois journées de marche dans le désert, et ils campèrent à Mara.
Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
9 Ils quittèrent Mara, et vinrent en Elim. Or, il y avait à Elim douze fontaines et soixante-dix tiges de palmiers; ils campèrent en ce lieu, à cause de l'eau.
Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
10 Puis, ils partirent d'Elim, et ils campèrent au bord de la mer Rouge.
Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
11 Et ils partirent de la mer Rouge, et ils campèrent dans le désert de Sin.
Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
12 Partis du désert de Sin, ils vinrent camper en Daphca.
Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
13 Et ils partirent de Daphca, et ils campèrent en Alus.
Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
14 Et ils partirent d'Alus, et ils campèrent à Rhaphidin; or, il n'y avait point là de l'eau pour que le peuple put boire.
Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
15 Ayant quitte Rhaphidin, ils dressèrent leurs tentes dans le désert de Sina.
Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
16 Du désert de Sina, ils vinrent camper aux Sépulcres de concupiscence.
Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
17 Ils s'éloignèrent des Sépulcres de concupiscence, et campèrent à Haseroth.
Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
18 Partis d'Haseroth, ils allèrent camper à Rethma.
Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
19 De Rethma, ils vinrent camper en Rhemmompharès.
Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
20 Ils partirent de Rhemmompharès, et ils campèrent en Lebna.
Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
21 Partis de Lebna, ils campèrent en Ressa.
Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
22 De Ressa, ils vinrent dresser leurs tentes en Céélatha.
Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
23 Et ils partirent de Céélatha, pour aller camper à Sépher.
Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
24 Ayant quitté Sépher, ils campèrent en Arada.
Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
25 Ils partirent d'Arada, et campèrent en Maceloth.
Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
26 De Maceloth, ils dressèrent leurs tentes en Thabath.
Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
27 Et ils partirent de Thabath, pour venir camper à Tharé.
Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
28 Partis de Tharé, ils campèrent à Methca.
Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
29 De Methca, ils vinrent camper à Hesmona.
Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
30 Et ils partirent de Hesmona, pour aller camper à Moserotb.
Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
31 Ayant quitté Moseroth, ils campèrent à Béné-Jaacan.
Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
32 Partis de Béné-Jaacan, ils vinrent camper en la montagne de Gadgad.
Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
33 De la montagne de Gadgad, ils vinrent camper à Jétébatba.
Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
34 Et ils partirent de Jétébatba, pour aller dresser leurs tentes en Hébrona.
Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
35 Puis, ayant quitté Hebrona, ils campèrent en Asion-Gaber.
Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
36 Partis d'Asion-Gaber, ils vinrent camper dans le désert de Sin, d'où, étant sortis, ils campèrent dans le désert de Pharan qui est Cadès.
Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
37 Partis de Cadès-Barné, ils vinrent camper sur la montagne de Hor, près de la terre d'Edom.
Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
38 Et Aaron monta sur la montagne par ordre du Seigneur, et il y mourut, en la quarantième année de la sortie d'Egypte, le cinquième mois, le premier de la lune.
Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
39 Aaron avait cent vingt-trois ans lorsqu'il mourut sur la montagne de Hor.
Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
40 Et, le Chananéen, roi d'Arad, qui demeurait en la terre de Chanaan, apprit que les fils d'Israël étaient en marche.
Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
41 Ils partirent ensuite de la montagne de Hor, et vinrent camper en Salmona.
Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
42 Ayant quitté Salmona, ils campèrent en Phunon.
Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
43 Partis de Phunon, ils dressèrent leurs tentes à Oboth.
Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
44 Puis, ils s'éloignèrent d'Obotb, pour venir camper à Gié-Abarim, au delà et près des frontières de Moab.
Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
45 Et ils partirent de Gié-Abarim, pour séjourner à Dibon-Gad.
Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
46 De Dibon-Gad, ils vinrent camper à Helmon-Déblathaïm.
Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
47 Partis de Helmon-Déblathaïm, ils campèrent sur les montagnes d'Abarim, en face de Nébo.
Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
48 Ayant quitté les montagnes d'Abarim, ils campèrent à l'Occident de Moab, sur le Jourdain, en face de Jéricho.
Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
49 Ensuite, ils campèrent aux bords du Jourdain de Beth-Simoth, à Abelsatim, à l'occident de Moab.
Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
50 Et le Seigneur parla à Moïse, à l'occident de Moab, sur le Jourdain, en face de Jéricho, et il lui dit:
Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
51 Parle aux fils d'Israël, et dis-leur: Vous allez traverser le Jourdain pour entrer en la terre de Chanaan.
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
52 Et, devant vous, vous exterminerez tous ceux qui habitent cette terre; vous détruirez leurs tours, leurs idoles jetées en fonte, et leurs colonnes.
wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
53 Vous détruirez tous les peuples de la terre promise, et vous l'habiterez; car je vous la donne pour héritage.
Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
54 Vous la partagerez entre vos tribus; donnant plus aux plus nombreux, et moins aux moindres en nombre. Quelle que soit la part qu'à chacun désignera le sort, chacun la possèdera; le partage se fera par tribus paternelles.
Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
55 Mais, si vous n'exterminez pas devant vous tous les habitants de la terre, ceux que vous aurez épargnés seront des traits en vos yeux, des flèches en vos flancs; ils seront vos ennemis sur la terre que vous habiterez.
“‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
56 Et alors, je vous traiterai vous-mêmes comme j'avais résolu de les traiter.
Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”

< Nombres 33 >