< Nombres 2 >

1 Le Seigneur parla ensuite à Moïse, disant:
Bwana aliwaambia Mose na Aroni:
2 Que les fils d'Israël campent en face les uns des autres, chaque homme restant à son rang sous ses enseignes, avec sa maison paternelle; qu'ils campent autour du tabernacle du témoignage.
“Waisraeli watapiga kambi zao kuzunguka Hema la Kukutania kwa umbali fulani kutoka kwenye hema, kila mwanaume chini ya alama yake pamoja na bendera ya jamaa yake.”
3 Les premières tentes du côté de l'orient seront sous le commandement du camp de Juda, avec leur armée, et le chef des fils de Juda sera Nahasson, fils d'Aminadab.
Kwa upande wa mashariki kuelekea mawio ya jua, kambi ya makundi ya Yuda watapiga kambi chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Yuda ni Nashoni mwana wa Aminadabu.
4 Son armée, selon le recensement, est de soixante-quatorze mille six cents hommes.
Kundi lake lina watu 74,600.
5 A côté, campera la tribu d'Issachar; leur chef sera Nathanaël, fils de Sogar.
Kabila la Isakari watapiga kambi karibu na Yuda. Kiongozi wa watu wa Isakari ni Nethaneli mwana wa Suari.
6 Son armée, selon le recensement, est de cinquante-quatre mille quatre cents hommes.
Kundi lake lina watu 54,400.
7 A côté, campera la tribu de Zabulon; leur chef sera Eliab, fils de Chaïlon.
Kabila la Zabuloni litafuata. Kiongozi wa watu wa Zabuloni ni Eliabu mwana wa Heloni.
8 Son armée selon le recensement, est de cinquante-sept mille quatre cents hommes.
Kundi lake lina watu 57,400.
9 Tous les hommes recensés du camp de Juda forment un corps de cent quatre- vingt-six mille quatre cents hommes; ils lèveront le camp les premiers avec toutes leurs forces.
Wanaume wote walio katika kambi ya Yuda, kufuatana na makundi yao, ni 186,400. Wao watatangulia kuondoka.
10 Le camp de Ruben se rangera du côté du midi; et le chef des fils de Ruben sera Elisur, fils de Sédiur.
Kwa upande wa kusini kutakuwa kambi ya makundi ya Reubeni chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Reubeni ni Elisuri mwana wa Shedeuri.
11 Son armée, selon le recensement, est de quarante-six mille cinq cents hommes.
Kundi lake lina watu 46,500.
12 A côté, campera la tribu de Siméon; leur chef sera Salamiel, fils de Surisadaï.
Kabila la Simeoni watapiga kambi karibu na Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Surishadai.
13 Son armée, selon le recensement, est de cinquante-neuf mille trois cents hommes.
Kundi lake lina watu 59,300.
14 A côté, campera la tribu de Gad; leur chef sera Eliasaph, fils de Raguel.
Kabila la Gadi litafuata. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deueli.
15 Son armée, selon le recensement, est de quarante-cinq mille six cent cinquante hommes.
Kundi lake lina watu 45,650.
16 Tous les hommes recensés du camp de Ruben, forment un corps de cent cinquante-un mille trois cent cinquante hommes; ils décamperont les seconds avec toutes leurs forces.
Wanaume wote walio katika kambi ya Reubeni, kufuatana na makundi yao, ni 151,450. Nao watakuwa nafasi ya pili kuondoka.
17 Le tabernacle du Seigneur sera dressé, et le camp des lévites sera placé au centre des camps; on marchera dans le même ordre que l'on dressera les tentes, chacun restant au corps auquel il appartient.
Kisha Hema la Kukutania na kambi ya Walawi vitakuwa katikati ya kambi zote. Wao watasafiri kwa utaratibu ule ule kama walivyopiga kambi, kila mmoja mahali pake mwenyewe chini ya alama yake.
18 Le camp d'Ephraïm se rangera du côté de l'occident; le chef des fils d'Ephraïm sera Elisama, fils d'Emiud.
Upande wa magharibi kutakuwepo na kambi ya makundi ya Efraimu chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
19 Son armée, selon le recensement, est de quarante mille cinq cents hommes.
Kundi lake lina watu 40,500.
20 A côté, campera la tribu de Manassé; leur chef sera Gamaliel, fils de Phadasur.
Kabila la Manase litafuata baada ya Efraimu. Kiongozi wa watu wa Manase ni Gamalieli mwana wa Pedasuri.
21 Son armée, selon le recensement, est de trente-deux mille deux cents hommes.
Kundi lake lina watu 32,200.
22 A côté, campera la tribu de Benjamin; leur chef sera Abidan, fils de Gadéoni.
Kabila la Benyamini litafuata baada ya Manase. Kiongozi wa watu wa Benyamini ni Abidani mwana wa Gideoni.
23 Son armée, selon le recensement, est de trente-cinq mille quatre cents hommes.
Kundi lake lina watu 35,400.
24 Tous les hommes recensés du camp d'Ephraïm forment un corps de cent huit mille cent hommes; ils décamperont avec toutes leurs forces.
Wanaume wote walio katika kambi ya Efraimu kufuatana na makundi yao ni 108,100. Nao watakuwa nafasi ya tatu kuondoka.
25 Le camp de Dan se rangera du côté du nord; et le chef des fils de Dan sera Achiézer, fils d'Amisadaï.
Upande wa kaskazini kutakuwa na makundi ya kambi ya Dani, chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
26 Son armée, selon le recensement, est de soixante-deux mille sept cents hommes.
Kundi lake lina watu 62,700.
27 A côté, campera la tribu d'Aser; leur chef sera Phagéel, fils d'Echran.
Kabila la Asheri watapiga kambi karibu na Dani. Kiongozi wa watu wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okrani.
28 Son armée, selon le recensement, est de quarante-un mille cinq cents hommes.
Kundi lake lina watu 41,500.
29 A côté, campera la tribu de Nephthali; leur chef sera Achire, fils d'Enan.
Kabila la Naftali litafuata. Kiongozi wa watu wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
30 Son armée, selon le recensement, est de cinquante-trois mille quatre cents hommes.
Kundi lake lina watu 53,400.
31 Tous les hommes recensés du camp de Dan forment un corps de cent cinquante-sept mille six cents hommes; ils décamperont les derniers, selon leur rang.
Wanaume wote walio katika kambi ya Dani ni 157,600. Wao watakuwa wa mwisho kuondoka chini ya alama yao.
32 Tel est le dénombrement des fils d'Israël, par maisons paternelles; le total du recensement de leurs forces donne six cent trois mille cinq cent cinquante hommes.
Hawa ndio Waisraeli, wakiwa wamehesabiwa kufuatana na jamaa zao. Wote walio kambini kwa makundi yao ni watu 603,550.
33 Or, les lévites, comme le Seigneur l'avait prescrit à Moïse, ne furent point recensés avec eux.
Hata hivyo, Walawi hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
34 Et les fils d'Israël firent tout ce que le Seigneur avait prescrit à Moïse; ils campèrent dans l'ordre à eux assigné, ils marchèrent en continuant de se tenir les uns près des autres, rangés par familles et par tribus.
Kwa hiyo Waisraeli wakafanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose. Hivyo ndivyo walivyopiga kambi chini ya alama zao, pia hivyo ndivyo walivyoondoka, kila mmoja akiwa na ukoo wake na jamaa yake.

< Nombres 2 >