< Nombres 1 >

1 Et le Seigneur parla à Moïse dans le tabernacle du témoignage, au désert de Sina, le premier du second mois de la seconde année, après la sortie d'Egypte, disant:
Mungu alimwambia Musa katika hema ya kukutania walipokuwa katika jangwa la Sinai. Hii ilitokea katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili miaka miwili baadaya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Mungu alisema,
2 Prenez le nombre de toute la synagogue d'Israël, et comptez-les par familles, par maisons paternelles, par têtes et par leurs noms.
'fanya sensa ya wanaume wote wa Israel kutoka kila ukoo, katika familia za baba zao. Wahesabu kwa majina, wahesabu kila mume, kila mwanamume
3 Tout mâle de vingt ans et au-dessus, tout Israélite pouvant marcher au combat, comptez-le dans l'armée. Tu feras ce dénombrement avec Aaron.
kuanzia umri a miaka ishirini na zaidi. Uwahesabu wote wanaoweza kupigana kama askari wa Israel. Wewe na Haruni mtaandika idadi ya wanaume katika makundi ya majeshi yao.
4 Faites-vous seconder par les princes des diverses tribus et familles paternelles.
Kila mwanamume kwa kila kabila, kichwa cha ukoo, lazima atumike na wewe kama kiongozi wa kabila.
5 Voici les noms des hommes qui vous assisteront; parmi ceux de Ruben, Elisur, fils de Sédiur;
Haya ndiyo majina ya viongozi ambao watapigana pamoja na wewe: Kutoka kabila la Reubeni, Elizuri mwana wa Shedeuri;
6 Parmi ceux de Siméon: Salamiel, fils de Surisadaï;
kutoka kabila la Simeoni, Shelumiel mwana wa Zurishadai
7 Parmi ceux de Juda: Nahasson, fils d'Aminadab;
Kutoka kabila la Yuda, Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 Parmi ceux d'Issachar: Nathanaël, fils de Sogar;
Ktoka kabila la Isakari, Nethaneli mwana wa Zuari;
9 Parmi ceux de Zabulon: Eliab, fils de Chaïlon;
kutoka kabila Zebuluni, Eliabu mwana wa Heloni
10 Parmi ceux de Joseph et d'Ephraïm: Elisama, fils d'Emiud; et parmi ceux de Manassé: Gamaliel, fils de Phadasur;
kutoka kabila la Efraimu mwana wa Yusufu, Elishama mwana wa Ammihudi; kutoka kabila la Manase, Gamaliel mwan wa Pedazuri;
11 Parmi ceux de Benjamin: Abidan, fils de Gadéoni;
kutoka kabila la Benjamini mwana wa Ysufu, Abidani mwan wa Gidion;
12 Parmi ceux de Dan: Achièzer, fils d'Amisadaï;
Kutoka kabila la Dan, Ahizeri mwana wa Amishadai;
13 Parmi ceux d'Aser: Phagéel, fils d'Echran;
kutoka kabila Asheri, Pagieli mwana wa Okirani;
14 Parmi ceux de Gad: Eliasaph, fils de Raguel;
kutoka kabila la Gadi, Eliasafu mwana wa Deuli;
15 Et parmi ceux de Nephthali: Achire, fils d'Enan.
na kutoka kabila la Naftali, Ahira mwana wa Enani.”
16 Ce sont les plus illustres du peuple, les princes de leurs tribus selon leur origine paternelle, commandants de mille hommes en Israël.
Hawa ndio wanaume waliochaguliwa kutoka kwa watu. Waliongoza kabila za mababu zao. Walikuwa viongozi wa koo katika Israel.
17 Moïse et Aaron prirent donc les hommes nominativement désignés.
Musa na Haruni wakawachukua wale wanaume, waliokuwa wameandikwa kwa majina,
18 Puis, ils rassemblèrent tout le peuple, le premier jour du second mois de la seconde année, et ils firent le dénombrement; ils prirent les noms de tous les mâles de vingt ans et au-dessus, selon leur naissance, par familles et par têtes,
na pamoja na wanaume hao waliwakusanya wanume wote katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Kisha kila mwanume wa miaka ishirini na zaidi alitambua babu zake. Alitakiwa kutaja koo na famila kutoka katika ukoo.
19 Comme le Seigneur l'avait prescrit à Moïse; ils firent ce recensement dans le désert de Sina.
Kisha Musa akaandika hesabu yao huko katika nyika ya Sinai, Kama Mungu alivyokuwa amemwamuru kufanya.
20 Les fils de Ruben, premier-né d'Israël, de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à l'armée, furent comptés nominativement par familles, par branches, par maisons paternelles et par têtes,
Kutoka uzao wa Reubeni, mtoto wa kwanza wa Israel, yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka hesabu ya ukoo na familia.
21 Et le recensement de la tribu de Ruben donna quarante-six mille cinq cents hommes.
Waliwahesabu wanaume 46, 000 kutoka ukoo wa Reubeni.
22 Les fils de Siméon, de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à l'armée, furent comptés nominativement pat familles, par branches, par maisons paternelles et par têtes,
Kutoka uzao wa Simeoni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi au wenye uwezo wa kwenda vitani, kutokana na hesabu ya ukoo na familia.
23 Et le recensement de la tribu de Siméon donna cinquante-neuf mille trois cents hommes.
Walihesabu wanaume 59, 300 kutoka kabila la Simeoni.
24 Les fils de Juda, de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à l'armée, furent comptés nominativement par familles, par branches, par maisons paternelles, par têtes,
Kutoka uzao wa Gadi yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
25 Et le recensement de la tribu de Juda donna soixante-quatorze mille six cents hommes.
Walihesabu wanaume 45, 650 kutoka kabila la Gadi.
26 Les fils d'Issachar de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à l'armée, furent compter nominativement par familles, par branches, par maisons paternelles, par têtes,
Kutoka uzao wa Yuda yalihesabiwa majina yote ya wanaume wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
27 Et le recensement de la tribu d'Issachar donna cinquante-quatre mille quatre cents hommes.
walihesabiwa wanume 74, 000 kutoka kabila la Yuda.
28 Les fils de Zabulon, tous ceux qui pouvaient aller à l'armée, furent comptes nominativement par familles, par branches, par maisons paternelles, par têtes,
Kutoka uzao wa Isakari yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
29 Et le recensement de la tribu de Zabulon donna cinquante-sept mille quatre cents hommes.
Walihesabiwa wanaume 54, 000 kutoka kabila la Isakari.
30 Les fils de Joseph, fils d'Ephraïm, de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à l'armée, furent compter nominativement par familles, par branches, par maisons paternelles, par têtes,
Kutoka uzao wa Zabuloni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
31 Et le recensement de la tribu d'Ephraïm donna quarante mille cinq cents hommes.
Walihesabiwa wanume 57, 400 kutoka kabila la Zabuloni.
32 Les fils de Manassé, de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à l'armée, furent comptés nominativement par familles, par branches, par maisons paternelles, par têtes,
Kutoka uzao wa Efraimu mwana wa Yusufu yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
33 Et le recensement de la tribu de Manassé donna trente-deux mille deux cents hommes.
Walihesabiwa wanaume 40, 500 kutoka kabila la Efraimu.
34 Les fils de Benjamin, de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à l'armée, furent comptés nominativement par familles, par branches, par maisons paternelles, par têtes,
Kutoka uzao wa Manase mwana wa Yusufu yaliheabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
35 Et le recensement de la tribu de Benjamin donna trente-cinq mille quatre cents hommes.
Walihesabiwa wanaume 32, 000 kutoka kabila la Manase.
36 Les fils de Gad, de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à l'armée, furent comptés nominativement par familles, par branches, par maisons paternelles, par têtes,
Kutoka uzao wa Benjamini yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
37 Et le recensement de la tribu de Gad donna quarante-cinq mille six cent cinquante hommes.
Walihesabiwa wanaume 35, 000 kutoka kabila la Benjamini.
38 Les fils de Dan, de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à l'armée, furent comptés nominativement par familles, par branches, par maisons paternelles, par têtes,
Kutoka uzao wa Dani yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, Kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
39 Et le recensement de la tribu de Dan donna soixante-deux mille sept cents hommes.
Walihesabiwa wanaume 62, 000 kutoka kabila la Dani.
40 Les fils d'Aser, de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à l'armée, furent comptés nominativement par familles, par branches, par maisons paternelles, par têtes,
Kutoka uzao wa Asheri yalihesabiwa majina yote ya kila mwanume mwenye umri wa miaka ishirini au zadi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
41 Et le recensement de la tribu d'Aser donna quarante-un mille cinq cents hommes.
Walihesabiwa wanaume 41, 500 kutoka ukoo wa Asheri.
42 Les fils de Nephthali, de vingt ans et au-dessus, tous ceux qui pouvaient aller à l'armée, furent comptés nominativement par familles, par branches, par maisons paternelles, par têtes,
Kutoka ukoo wa Naftali yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
43 Et le recensement de la tribu de Nephthali donna cinquante-trois mille quatre cents hommes.
Walihesabiwa wanaume 53, 400 kutoka kabila la Naftari
44 Tel fut le dénombrement que fit Moïse avec Aaron, et les chefs d'Israël au nombre de douze, un homme par tribu, pris dans la tribu de sa maison paternelle.
Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote hawa, pamoja na wale wanaume kumi na wawili waliokuwa wakiongoza yale makabila kumi na mawili ya Israeli.
45 Et Le recensement total des fils d'Israël, de vingt ans et au-dessus, en état de porter les armes, donna
Kwa hiyo wanaume wote wa Israeli wenye umri wa miak ishirini au zaidi, wote wenye uwezo wa kwenda vitani, walihesabiwa kutoka kwenye familia zao.
46 Six cent trois mille cinq cent cinquante hommes.
Walihesabu wanaume 603, 550.
47 Mais les lévites de la tribu paternelle de Lévi ne furent point recensés parmi les fils d'Israël.
Lakini wanaume toka uzao wa Lawi hawakuhesabiwa,
48 Car le Seigneur avait parlé à Moïse, disant:
Kwa sababu BWANA alimwambia Musa,
49 Tu ne recenseras pas la tribu de Lévi, et tu n'en prendras pas le nombre parmi les fils d'Israël.
“usiwahesabu wale wa kabila la Lawi wala kuwajumuisha kwenye jumla ya watu wa Israeli.
50 Tu donneras aux lévites le soin du tabernacle du témoignage, de ses ornements et de tout ce qu'il renferme; et ils transporteront le tabernacle avec tous ses ornements; ils exerceront le sacerdoce dans le tabernacle, et ils camperont autour du tabernacle.
Badala yake, waagize Walawi kuliangalia hema la amri za agano, na kuangalia mapambo ya hema na vyote vilivyomo. Walawi watalazimika kulibeba hema na lazima wayabebe mapambo ya hema. Lazima waliangalie hema na kuyatengeneza mazingira yake. Wataiangalia masikani na kuzitengeneza kambi zinazolizunguka.
51 Lorsqu'il faudra enlever le tabernacle, les Lévites l'enlèveront, et lorsqu'il faudra dresser le tabernacle, ils, le dresseront; que l'homme d'une autre tribu qui s'en approcherait soit mis à mort.
Kila hema litakapotakiwa kuhamishiwa eneo jingine, Walawi ndio watakaolipeleka pale. Na kila hema litakapotakiwa kusimamishwa, Walawi ndio watakao lisimamisha. Na mgeni yeyote atakayelisogelea hema lazima auawe.
52 Lorsque les fils d'Israël camperont en corps d'armée, chacun au rang à lui assigné, selon la branche a laquelle il appartient,
Wakati watu wa Israeli watakaposimamisha hema zao, kila mwanaume lazima awe karibu na bango la jeshi lake.
53 Que les lévites campent en cercle, près du tabernacle du témoignage, et il n'y aura point de péché parmi les fils d'Israël. Les lévites seuls auront la garde du tabernacle du témoignage.
Hata hivyo Walawi lazima waweke hema zao kuizunguka hiyo masikani ya amri za agano ili kwamba hasira yangu isije ikawaka juu ya wana wa Israeli. Walawi lazima wailinde hiyo masikani ya amri za agano.”
54 Et tout ce que le Seigneur avait prescrit à Moïse et à Aaron, les fils d'Israël le firent.
Wana wa Israeli walifanya yote haya. Walifanya yote ambayo BWANA aliagiza kupitia Musa.

< Nombres 1 >